S.N.Jilala
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 540
- 507
Tafakuri
Na; Simon Jilala, 29/11/2015
Kama umeajiriwa kwenye Taasisi za umma usipoiba hata Bosi wako anaanza kukushangaa na kukutilia wasiwasi sana.
Na ukiendelea kubaki mtiifu na mzalendo katika Taasisi yoyote mara nyingi jiandae kuhamishwa, kutoshirikishwa katika mambo nyeti au kufukuzwa kazi kwa sababu ama wanahofia utaibua maovu yao au kwa sababu unawapinga kila wakitaka kupiga dili.
Kuna matukio mengi katika jambo hili, kwa mfano, mnakumbuka mtangazaji wa TBC Jerry Muro alivyoibua wala rushwa hasa askali barabarani kilimtokea nini?, Je wakubwa wa nchi walimtetea?, Mnakumbuka ya Mbunge Machachali David Kafulila katika mambo ya Escrow, kijana alijitoa sana, na mara nyingi akawa anashitakiwa na kutishiwa maisha.
Kwenye Taasisi zilizo nyingi kwa sababu ya mifumo ya rushwa, wasema kweli hawatakiwi kabisa. Na wengi wamefukuzwa kazi, wameshushwa vyeo, na cha kushangaza sana Taasisi nyingi unakuta eti wanachukia rushwa wakati huohuo ni wazuri sana wa kulea wala rushwa.
Serikali ikiamua kuwashugulikia wala rushwa kisawasawa hata tatizo la ajira litaisha kabisa Tanzania. Kiukweli watu wengi ni wala rushwa na watafukuzwa mno na vijana waliomaliza vyuo na hawana kazi watapata kazi kwa kujaza nafasi zao, nao watajiajiri kiurahisi maana wameiba sana, wana mahotel ya kifahari, majumba ya kifahari, mabasi, na wengine wana fedha lukuki kwenye mabenki. Na ukiamua kuwafilisi, na kuipeleka fedha kwenye huduma za kijamii, hakika watoto wao nao watakuja kufaidika sana.
Utajiri sawa, lakini umeupataje?. Imefikia mahala ukiiba unasifiwa kama umegundua kutengeneza ndege au umeenda mwezini. Hili ni lazima lishughulikiwe, na waizi Mimi sina nafasi nao washugulikiwe tu.
Kijana ameajiriwa leo, ukikutana naye baada ya mwaka utakuta ana gari la milioni 50 na anamalizia nyumba ya milioni 100 au 200, jibu lake ukimuuliza umepata wapi hela atakwambia humu mjini changamka, au atakwambia Mimi mpambanaji!!!! inamaana uizi siku hizi ni upambanaji.
Mimi nasema waizi wote washugulikiwe kwa mjibu wa sheria za nchi kwani wanafilisi Taifa letu na kuwanyima vijana wetu fursa za kujiajiri na kuajiriwa pia.
Mungu ni Mkubwa na huwa hapendelei. Mungu Bariki Taifa letu na watu wote.
Na; Simon Jilala, 29/11/2015
Kama umeajiriwa kwenye Taasisi za umma usipoiba hata Bosi wako anaanza kukushangaa na kukutilia wasiwasi sana.
Na ukiendelea kubaki mtiifu na mzalendo katika Taasisi yoyote mara nyingi jiandae kuhamishwa, kutoshirikishwa katika mambo nyeti au kufukuzwa kazi kwa sababu ama wanahofia utaibua maovu yao au kwa sababu unawapinga kila wakitaka kupiga dili.
Kuna matukio mengi katika jambo hili, kwa mfano, mnakumbuka mtangazaji wa TBC Jerry Muro alivyoibua wala rushwa hasa askali barabarani kilimtokea nini?, Je wakubwa wa nchi walimtetea?, Mnakumbuka ya Mbunge Machachali David Kafulila katika mambo ya Escrow, kijana alijitoa sana, na mara nyingi akawa anashitakiwa na kutishiwa maisha.
Kwenye Taasisi zilizo nyingi kwa sababu ya mifumo ya rushwa, wasema kweli hawatakiwi kabisa. Na wengi wamefukuzwa kazi, wameshushwa vyeo, na cha kushangaza sana Taasisi nyingi unakuta eti wanachukia rushwa wakati huohuo ni wazuri sana wa kulea wala rushwa.
Serikali ikiamua kuwashugulikia wala rushwa kisawasawa hata tatizo la ajira litaisha kabisa Tanzania. Kiukweli watu wengi ni wala rushwa na watafukuzwa mno na vijana waliomaliza vyuo na hawana kazi watapata kazi kwa kujaza nafasi zao, nao watajiajiri kiurahisi maana wameiba sana, wana mahotel ya kifahari, majumba ya kifahari, mabasi, na wengine wana fedha lukuki kwenye mabenki. Na ukiamua kuwafilisi, na kuipeleka fedha kwenye huduma za kijamii, hakika watoto wao nao watakuja kufaidika sana.
Utajiri sawa, lakini umeupataje?. Imefikia mahala ukiiba unasifiwa kama umegundua kutengeneza ndege au umeenda mwezini. Hili ni lazima lishughulikiwe, na waizi Mimi sina nafasi nao washugulikiwe tu.
Kijana ameajiriwa leo, ukikutana naye baada ya mwaka utakuta ana gari la milioni 50 na anamalizia nyumba ya milioni 100 au 200, jibu lake ukimuuliza umepata wapi hela atakwambia humu mjini changamka, au atakwambia Mimi mpambanaji!!!! inamaana uizi siku hizi ni upambanaji.
Mimi nasema waizi wote washugulikiwe kwa mjibu wa sheria za nchi kwani wanafilisi Taifa letu na kuwanyima vijana wetu fursa za kujiajiri na kuajiriwa pia.
Mungu ni Mkubwa na huwa hapendelei. Mungu Bariki Taifa letu na watu wote.