KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,215
- 56,855
Hii ndio hali halisi, Rushwa itangazwe kuwa ni janga kubwa linalotakiwa kutazamwa kwa jicho pevu. Kwa upigaji Tanzania hatuwezi kushika mkia ni namba za mwanzoni, binafsi nimeanza kuona kila Mtanzania ni mpiga dili tu nikiwemo na mimi! Ukikaa vibaya halafu hela nje nje inakula kwako. Si Escrow au EPA Tanzania lina watu wapigaji hata tusipoangalia kabila n.k
Hili tatizo bado halijapata muarobaini hasa ngazi za juu! Naona Mambo ndo yanazidi kuharibika. Ni dhahiri kunahitajika intelligence juu ya haya mambo lasivyo tutakufa maji. Hakuna cha kusema ni CCM wala nini hili ni tatizo! Na linatakiwa kudhibitiwa hata chama chochote kitakachoingia madarakani kikute tatizo limetibiwa sio nao waje warithi twafa.
Hili tatizo bado halijapata muarobaini hasa ngazi za juu! Naona Mambo ndo yanazidi kuharibika. Ni dhahiri kunahitajika intelligence juu ya haya mambo lasivyo tutakufa maji. Hakuna cha kusema ni CCM wala nini hili ni tatizo! Na linatakiwa kudhibitiwa hata chama chochote kitakachoingia madarakani kikute tatizo limetibiwa sio nao waje warithi twafa.