Zamiluni Zamiluni
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 13,996
- 15,118
Dubai ndiyo inaongoza kwa wingi wa mahoteli !! ivyo tusema nao ndo kama Bongo?
Hebu fikiri kwanza....Mahoteli kila kukicha yanajengwa...Ubungo, sinza, kinondoni karibu kila baada ya mitaa miwili mahoteli na Guests je fikiria mwenyewe...Tuna wageni gani hasa wanaokuja kutoka nje ya mkoa wa kulala hoteli hizo?
Kwani sie tumekuwa Brazil kombe la dunia lipo kwetu wageni kila kona ya nchi wanakuja?
Fahamu kuwa hoteli hizi ni za kulala sisi sisi japo tunamajumba yetu...Mwanaume wa kileo km hachepuki anajambo
Kumekuwepo mahotel mengi yanajenjwa kila kukicha walengwa wakiwa wageni, lakini kumekuwa tofauti wenyeji ndio wanakuwa wageni, eti mtu anatoka kinondoni manyanya anakwenda magomeni mapipa.
Mgeni huyu anasingizia stress lakini huku akiwa na mke wa mtu aliyeagwa uwanja wa ndege au ubungo kwenda mikoani na kusindikizwa kwa mbwembwe , kumchumu na kumwombea safari njema.
Ghafula Mama anatafutwa mmewe kapata ajari kibaha katibiwa na kuruhusiwa jioni huku mke akilalamikia simu kuishiwa chaji, asubuhi anamkuta Mme anajiandaa kurejea kwenye vipimo.
Ikiwa kila Nyumba ya wageni inawekewa mite go ndoa zitabaki ngapi kwenye hili jiji la raha na karaha.