Dumbuya
JF-Expert Member
- Jan 23, 2014
- 596
- 880
Wakuu ,
Napenda kudeclare interest kwenye ishu inayoendelea mitandaoni na hata katika jamii ya Tanzania kwa ujumla.Sina uanachama wa chama chochote,sishabikii uhalifu,sishabikii uminywaji wa haki za kibinadamu na za kikatiba,sishabikii uvunjifu wa sheria na katiba ya JMT.Mimi ni mtanzania,raia safi na mtii wa sheria bila shurti.
Naungana na watanzania wenzangu kuomboleza kifo cha binti aliyefikwa na mauti pamoja na wengineo katika harakati za uchaguzi katika jimbo la kinondoni.Mungu azipumzishe roho zao pema peponi !
Uchunguzi unaendelea na siyo vizuri kuingilia uchunguzi wa kipolisi kwa kuwa jambo lipo kwenye mikono ya dola tayari.Lakini umma wa watanzania umejawa na maswali mengi.Wadadisi wanasema ili kupata jibu sahihi ni lazima kuuliza swali sahihi.
Naomba tuandike maswali ambayo pengine yakipatiwa majibu yatasaidia kuelezea mnyororo wa matukio yaliyotokea :
1.Ni kwanini mkurugenzi kwa kujua na kutambua umuhimu na unyeti wa zoezi la uchaguzi,acheleweshe barua za mawakala?
2.Je,ni kwanini kama vyama vya siasa(husika) vilikuwa na shida,Mkurugenzi asitoe muongozo mapema kabla ya uchaguzi kusudi watu wapige kura kwa amani na kumchagua kiongozi wao?
Endelea ;
Napenda kudeclare interest kwenye ishu inayoendelea mitandaoni na hata katika jamii ya Tanzania kwa ujumla.Sina uanachama wa chama chochote,sishabikii uhalifu,sishabikii uminywaji wa haki za kibinadamu na za kikatiba,sishabikii uvunjifu wa sheria na katiba ya JMT.Mimi ni mtanzania,raia safi na mtii wa sheria bila shurti.
Naungana na watanzania wenzangu kuomboleza kifo cha binti aliyefikwa na mauti pamoja na wengineo katika harakati za uchaguzi katika jimbo la kinondoni.Mungu azipumzishe roho zao pema peponi !
Uchunguzi unaendelea na siyo vizuri kuingilia uchunguzi wa kipolisi kwa kuwa jambo lipo kwenye mikono ya dola tayari.Lakini umma wa watanzania umejawa na maswali mengi.Wadadisi wanasema ili kupata jibu sahihi ni lazima kuuliza swali sahihi.
Naomba tuandike maswali ambayo pengine yakipatiwa majibu yatasaidia kuelezea mnyororo wa matukio yaliyotokea :
1.Ni kwanini mkurugenzi kwa kujua na kutambua umuhimu na unyeti wa zoezi la uchaguzi,acheleweshe barua za mawakala?
2.Je,ni kwanini kama vyama vya siasa(husika) vilikuwa na shida,Mkurugenzi asitoe muongozo mapema kabla ya uchaguzi kusudi watu wapige kura kwa amani na kumchagua kiongozi wao?
Endelea ;