Tujiulize kwanini Samia haongelei Rushwa tena

Hivi zile kelele za Mwigulu anazosema Majizi Majizi anamuelekezea kidole yeye au hicho kidole anaelekezea wapi?
Inafikirisha! Mtu anasema majizi majizi, halafu hakuna majizi yanayokamatwa. Hayo majizi yasiyokamatika ni kina nani?
 
Kwani aliongelea rushwa lini?

Unayo mifano ya kutuonyesha akiongelea rushwa wakati wowote?

Hivi kweli ni lazima kuanzisha mada humu jukwaani?

Sasa hapa unataka tujadili kitu gani kitakachotusaidia kuondokana na balaa hili lililotukumba Tanzania wakati huu!

Ngoja nikupe dokezo la mada ambayo ukiitengeneza vyema wengi wetu tutachangia.

Anzisha mada ya uhakika kabisa inayoeleza jinsi Samia alivyo msaada mkubwa kwa Kenya katika kuidumaza Tanzania isiweze kushika nafasi yake sahihi kiuchumi Afrika Mashariki.

Mimi nadhani Samia Suluhu Hassan atakuwa ni wakala wa Kenya, aliyewekwa hapa maksudi kabisa kuididimiza nchi hii.

Nasubiri mada yako hiyo muhimu ili nami nije nichangie niliyo nayo juu yake. Ninayo mengi sana!
 
Mama Samia sio yule wa 2021-2022 ndiyo maana haongelei rushwa kabisa.

Maza hajawahi kuongelea rushwa. Sana sana aliihalalisha kwa kuwaruhusu watu wale kwa urefu wa kamba zao.
 
She has no moral ground to condemn anything evil anymore.

She embraced all the ugly vices that she is now part and parcel wa kila ovu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…