Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 17,572
- 27,320
Historia inajirudia na hakuna kipya chini ya jua; Ukiona jambo jipya basi ni Historia ambayo wewe huifahamu. Sasa kuepuka na kuingia mitegoni taweka tu mifano minne ambapo mamlaka ilitumia propaganda kuzima sauti za wadai haki au kuwaondoa wasio na kosa ili kufanikisha malengo yao...
Uhuru na Raila / Ruto na Raila: Raila alikuwa mzee wa Maandamano na kuna kipindi alisema kutakuwa na maandamano kila wiki, watawala walitumia mbinu za kuwashawishi mama mboga na wafanyabiashara kulalamika mpaka kwenye Luninga - ni vipi huyu mzee anawaharibia biashara zao na wao kushindwa kujipatia mkate wao ?
Ruto na Gen - Z: Kwakweli sikuwahi kuona maandamano organized kama ya Gen - Z Kenya vijana wadogo wana bendera ya taifa na maji huku wana simu zao wakirekodi na kumwaga nondo ni vipi Ruto anawakosea, ingawa baadhi walivamia Parliament (na hapo ni baada ya mswada ambao walikuwa wanasema usipite wabunge wakapitisha) Ruto akapitia humo humo jioni yake kwamba wale ni Magaidi na sio waandamanaji wala wadai haki, ingawa picha / video nyingi zilionyesha jambo tofauti, vijana wanadai haki yao bila vurugu Ruto ikabidi apoe na kuomba kukutana nao.... (Ingawa madogo walijua kwa kukutana na Mamlaka ni mwanzo wa watu kupenyezewa Rupia kwenye Udhia) madogo wakakataa
Ruto / Mamlaka (Goons) Vs Gen-Z
Maandamano yaliyofuata kulitokea watu kuchoma vitu na kuiba mali za watu (kuna uthibitisho usio na shaka kwamba hao waliofanya hivyo walikuwa ni mamlaka (wahuni waliolipwa na mamlaka) ili wafanye fujo na kuonyesha Gen-Z ni watu wasio na adabu na waharibu mali za Umma; Kuna video ilishikwa na NTV ya watu wakipanga watu wa kuwaibia simu na kuwapiga wanawake sababu hao kelele zao ndio zitakuwa backlash kubwa, au Sakaja Governor wa Nairobi alipata tuhuma za kupanga ma-goons wafanye fujo;
Magari yalichomwa moto - Roto akaja na Kauli ya Shoot in Leg (ambayo mpaka leo anaitetea); pia Kwenye mitandao kulikuwa na Chat nyingi sana za Occupy State House - Muandamanaji na mtetezi Gwiji (Boniface Mwangi) alisema kuna uthibitisho usio na shaka wengi waliokuwa wanasema hivyo ni vijana waliolipwa na mamlaka ili kuwapa sababu ya kuyavunja maandamano (kwamba sio waandamanaji wadai haki bali ni magaidi wanaotaka kupindua serikali)
USA / CIA na UK Vs Mohamed Mosadeign wa IRAN
Baada ya UK kuona kuna uwezekano wa serikali ya Iran kubinafisha mafuta walifanya kila wanaloweza kwa kushirikiana na wenzao USA ili kuangusha Serikali ya Mosadeign wa Iran na kumpatia nguvu kibaraka wao (Mfalme); mbinu zote zilishindikana; ndio hapo CIA wakapata wazo la kuwapa wahuni wengi pesa ambao walijifanya ni wafuasi wa Mosadeign, kila ijumaa baada ya Kuswali wafuasi hao (Kenge) waliandamana huku wanamsifia Mosadeign na safari yao kumalizikia kwenye maduka ya watu na kufanya looting, wananchi wakachoka na kuanza kulalamika jeshi likashindwa cha kufanya bali kumuondoa Mosadeign.
Moral of the Story
Kwenye hizi sintofahamu za Kenge wengi ni vema kila story ikija kuiangalia mara mbili na kujiuliza inamsaidia nani (Sisi wadai Haki au inajifanya tunasaidiana Kudai Haki lakini mwisho wake inamsaidia Mtawala) - Nimeanza kusikia mengi sijui silaha zinaingizwa; mwingine anasema sehemu za kuchoma n.k. nashindwa kuelewa hawa ni wenzetu au mapandikizi wanaowapa watawala Sababu kwamba walikuwa hawapambani na wenye nchi bali watakia mabaya nchi.... Unadhani hata huyu anayekutetea leo, kesho akiambiwa kibarua chako kimeota mizizi au usafiri hakuna sababu wa wahuni kesho atakutetea (Ingawa anaweza kudhani ni wewe mdai haki ndio umefanya hivyo kumbe ni Mamluki anayekuchafulia Harakati zako)
Uhuru na Raila / Ruto na Raila: Raila alikuwa mzee wa Maandamano na kuna kipindi alisema kutakuwa na maandamano kila wiki, watawala walitumia mbinu za kuwashawishi mama mboga na wafanyabiashara kulalamika mpaka kwenye Luninga - ni vipi huyu mzee anawaharibia biashara zao na wao kushindwa kujipatia mkate wao ?
Ruto na Gen - Z: Kwakweli sikuwahi kuona maandamano organized kama ya Gen - Z Kenya vijana wadogo wana bendera ya taifa na maji huku wana simu zao wakirekodi na kumwaga nondo ni vipi Ruto anawakosea, ingawa baadhi walivamia Parliament (na hapo ni baada ya mswada ambao walikuwa wanasema usipite wabunge wakapitisha) Ruto akapitia humo humo jioni yake kwamba wale ni Magaidi na sio waandamanaji wala wadai haki, ingawa picha / video nyingi zilionyesha jambo tofauti, vijana wanadai haki yao bila vurugu Ruto ikabidi apoe na kuomba kukutana nao.... (Ingawa madogo walijua kwa kukutana na Mamlaka ni mwanzo wa watu kupenyezewa Rupia kwenye Udhia) madogo wakakataa
Ruto / Mamlaka (Goons) Vs Gen-Z
Maandamano yaliyofuata kulitokea watu kuchoma vitu na kuiba mali za watu (kuna uthibitisho usio na shaka kwamba hao waliofanya hivyo walikuwa ni mamlaka (wahuni waliolipwa na mamlaka) ili wafanye fujo na kuonyesha Gen-Z ni watu wasio na adabu na waharibu mali za Umma; Kuna video ilishikwa na NTV ya watu wakipanga watu wa kuwaibia simu na kuwapiga wanawake sababu hao kelele zao ndio zitakuwa backlash kubwa, au Sakaja Governor wa Nairobi alipata tuhuma za kupanga ma-goons wafanye fujo;
Magari yalichomwa moto - Roto akaja na Kauli ya Shoot in Leg (ambayo mpaka leo anaitetea); pia Kwenye mitandao kulikuwa na Chat nyingi sana za Occupy State House - Muandamanaji na mtetezi Gwiji (Boniface Mwangi) alisema kuna uthibitisho usio na shaka wengi waliokuwa wanasema hivyo ni vijana waliolipwa na mamlaka ili kuwapa sababu ya kuyavunja maandamano (kwamba sio waandamanaji wadai haki bali ni magaidi wanaotaka kupindua serikali)
USA / CIA na UK Vs Mohamed Mosadeign wa IRAN
Baada ya UK kuona kuna uwezekano wa serikali ya Iran kubinafisha mafuta walifanya kila wanaloweza kwa kushirikiana na wenzao USA ili kuangusha Serikali ya Mosadeign wa Iran na kumpatia nguvu kibaraka wao (Mfalme); mbinu zote zilishindikana; ndio hapo CIA wakapata wazo la kuwapa wahuni wengi pesa ambao walijifanya ni wafuasi wa Mosadeign, kila ijumaa baada ya Kuswali wafuasi hao (Kenge) waliandamana huku wanamsifia Mosadeign na safari yao kumalizikia kwenye maduka ya watu na kufanya looting, wananchi wakachoka na kuanza kulalamika jeshi likashindwa cha kufanya bali kumuondoa Mosadeign.
Moral of the Story
Kwenye hizi sintofahamu za Kenge wengi ni vema kila story ikija kuiangalia mara mbili na kujiuliza inamsaidia nani (Sisi wadai Haki au inajifanya tunasaidiana Kudai Haki lakini mwisho wake inamsaidia Mtawala) - Nimeanza kusikia mengi sijui silaha zinaingizwa; mwingine anasema sehemu za kuchoma n.k. nashindwa kuelewa hawa ni wenzetu au mapandikizi wanaowapa watawala Sababu kwamba walikuwa hawapambani na wenye nchi bali watakia mabaya nchi.... Unadhani hata huyu anayekutetea leo, kesho akiambiwa kibarua chako kimeota mizizi au usafiri hakuna sababu wa wahuni kesho atakutetea (Ingawa anaweza kudhani ni wewe mdai haki ndio umefanya hivyo kumbe ni Mamluki anayekuchafulia Harakati zako)