Tujihadhari na matapeli katika ajira?

Tujihadhari na matapeli katika ajira?

nzigo

Member
Joined
Sep 15, 2011
Posts
8
Reaction score
4
Jamani tuwe macho na matapeli katika ajira. Mimi nimenusurika. Hebu soma hii:
Siku moja nilipigiwa simu na mtu mmoja aliyejitambulisha kuwa ni Dr Joseph Mwakabonga kutoka WHO, Tanzania. Alijifanya kuwa ananifahamu kabisa na aliniita kwa jina japo mimi simfahamu kabisa na sikumbuki kama nimeshawahi kukutana na mtu mwenye jina hilo. Mtu huto aliniambia kuwa WHO wana mradi ambao wanauanzisha hivi karibuni jijiji Dar na hivyo alinipigia kuniuliza kama nitapenda kufanya kazi katika mradi huo. Akanieleza kuwa nitakuwa ninalipwa dola za Marekani 3000 kwa mwezi, nitapewa gari ya kutembelea (Landcruiser VX), nyumba pamoja na marupurupu mengine. Wakati ananipigia alisema alikuwa mkoani Rukwa na alitegemea kuja Dar kwa ndege siku hiyo jioni na akaniomba tuonane kwa mazungumzo zaidi ambapo atangenikutanisha na boss wake na alisema akifika tu Dar atanitafuta.Mimi sikuamini kuhusu hilo dili lakni nilikubali tukutane ili nimsikilize ana kwa ana ili niweze kubaini kama hilo dili ni la kweli au ni usanii .Hata hivyo siku hiyo hakunitafuta. Kesho yake nilimpigia akaniambia yuko Mkuranga kwenye eneo mojawao la miradi ya WHO na akasema angenipigia baadaye. Lakini cha ajabu mtu huyo hajanitafuta tena tangu siku ile na ni zaidi ya mwezi umeshaisha.Siku hizi hata simu yake haipatikani kabisa.

Kilichonitia wasiwasi, siku ya kwanza wakati tunaongea kwa simu aliniuliza kama nina gari na kama nitakuja nayo. Nilimwambia kuwa gari ninayo lakini kwa sababu tulikubaliana kukutana jioni au usiku nilimwambia sitakuja nayo kwa sababu ya kuogopa usumbufu wa foleni. Ninahisi mtu yule alikuwa mwizi wa magari na alipogundua kuwa sitakuja na gari akaona dili limeharibika!

Je, kuna mdau anamfahamu mtu huyo, au kuna mdau mwingine amewahi kukutana na kisa kama hiki?
 
mimi amenipigia leo anajityambulisha anaitwa Dr. Joseph Martin Mwakabonga na kuwa amenichagua kuwa Coordinator wa mradi wa watoto yatima na wajane. Aisee kabla sijanda kumuona nika mgoogle ndo nikakutana na hii thread. Tuwe makini wanatumia mpaka wazungu.
 
Umenisaidia sana kuandika hiki kisa maana mimi leo amenipigia simu na kunieleza exactly kama alivyokuambia wewe ila tofauti ni kwamba mradi huo tutaanzisha hapa Loliondo ninapoishi. Benefits ni hizo hizo. Watakuja kwa ndege leo Arusha halafu Loliondo kwa gari la WHO la ofisi ya Arusha watakuja kesho. Mimi bado nawasubiri yeye na mzungu wake Mjerumani anaitwa Mombeck. Bahati nzuri kabla ya kufanya lolote nika-google jina lake ndio nikapata hii coincidence. Nashukuru sana maana sasa na aje tu. Sijui kwa nini habadili jina!
 
Hawa watu dawa yao ni kuwapeleka tu polisi ..hapo hatujui wameshatapeli watu wangapi hadi sasa sababu sio wote wataweza kuepukana na utapeli huu.
 
Back
Top Bottom