Tujiendeleze sana chini ya Serikali ya awamu ya tano, awamu ya sita yaweza kula kwetu

Benmpo

JF-Expert Member
Mar 23, 2015
450
424
Habari za leo Wanajamvi,

Kwa kipindi kirefu Watanzania tulikuwa na shauku ya kupata Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu katika utendaji wake. Maamuzi ambayo yangelinufaisha Taifa huku pengine yakizua malalamiko kwa baadhi ya watu au lawama kwa baadhi ya ndugu na marafiki wa kiongozi huyo.

Kuna wakati Mh. Edward Lowassa akichangia Bungeni, huku akipigiwa makofi na Wabunge wengi, alipata kusema (nanukuu): “Tatizo la nchi hii mnazungumza mambo, mnazungumza hakuna utekelezaji. Tunazunguza lakini discipline ya Malaysia na hapa ni tofauti. Hapa kuna Uswahili mwingi wa kukaa bila kutekeleza mambo, mnaamua hamtekelezi. Inatakiwa chombo kinachoweza kufanya maamuzi magumu na yakawa maamuzi magumu yanayotekelezeka kweli kweli. Mkishakubaliana mambo yafanyike. Haiwezekani katika nchi kila mtu akawa analalamika, kiongozi analalamika, mwananchi analalamika” (mwisho wa kunukuu). Kutokana na hali ilivyokuwa, ya kutotekeleza makubaliano mara kwa mara EL pia alidai kuwa “Ni bora kufanya maamuzi na kulaumiwa kuliko kutofanya kabisa”. Aidha katika mchango wake huo EL aligusia maeneo mbalimbali yaliyohitaji maamuzi magumu kama vile foleni Jijini Dar, Reli ya Kati, na mengineyo.

Nilikubaliana na hoja za EL kwa asilimia 100%. Ni ukweli usiopingika kuwa miradi mingi ilizinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi kwa mbwembwe nyingi iwe na viongozi wa serikali, viongozi wa mbio za Mwenge na wengineo, lakini miradi hiyo haijatekelezwa hadi leo. Bungeni kulijaa maazimio yenye matumaini lakini yote hayo hayakutekelezwa. Miradi mingi imeozea kwenye madimbwi ya “Tupo kwenye upembuzi yakinifu (feasibility study)” na “Tupo kwenye mchakato (process)”. Ilikuwa ukisikia madimbwi hayo mawili unajua tu hakuna kitu kinachoendelea, na yalishamiri sana hasa kisiasa katika kuzipotezea mantiki hoja zenye mlengo wa kuhoji maendeleo yake. Ni upembuzi yakinifu au mchakato ambao ulikuwa huwezi kuona mtu au kitu chochote katika eneo la mradi (site) kwa miaka mingi. Kwa kweli hayo madimbwi yalichosha watu wengi sana.

Mwaka 2015 ulifanyika uchaguzi mkuu na kumpata Rais John Magufuli. Ni Rais aliyependwa na watu wengi sana, waliompa kura na wale ambao hawakumpa kura pia. Nasema hivyo kwa sababu watu wengi walikiri kuwa Rais Magufuli ana uwezo mkubwa lakini wasingempa kura kwa sababu chama alichopeperusha bendera yake hawakukipenda. Lakini yeye JPM aliwahakikishia watu kuwa baada ya kuchaguliwa angeweza kufanya “Total system overhaul”; hali iliyopelekea watu wengi pia kumwamini na kumchagua kuwa Rais wa awamu ya tano. Ni Rais aliyebeba matumaini ya wengi, na aina ya Rais aliyekuwa ni ndoto ya watu wengi akiwemo EL (rejea quotation ya EL hapo juu).

Baada ya Rais JPM kuapishwa wote tuliona bidii zake. Kuna wengine walisema zilikuwa ni nguvu za soda lakini tunaona huu ni mwaka wa pili yupo at constant speed. Ni Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu na sisi sote tunaoona ni vema na haki (it’s right and just) kuongea ukweli tunampongeza.

Katika utawala wake tumeona kuwa madimbwi ya “mchakato” na “upembuzi yakinifu” yamekuwa ya kiutendaji zaidi na si ya kuua miradi/mipango. Tumeshuhudia mawe ya msingi yakiwekwa au maagizo yakitolewa; mapema tunaowaona watu katika maeneo ya miradi au kazi nyinginezo. Kwa mfano tumeona siku moja baada ya Rais kuliagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kujenga ukuta kuuzunguka mgodi wa madini ya Tanzanite huko Mererani, watu wameonekana katika eneo la mradi wakifanya upembuzi yakinifu kwa hatua za utekelezaji. Kwa kweli ni suala la kupongezwa kwani kila aina ya uzembe au ubadhirifu kwa baadhi ya Viongozi au watendaji hauna nafasi kwake.

EL alizungumzia suala la foleni Jijini Dar. Mbali na miradi miwili mikubwa ya Ubungo Interchange na Flyovers pale TAZARA ambayo inaendelea kwa kasi baada ya kuzinduliwa na Rais JPM, pia kulikuwa na Mradi wa Magari yaendayo kasi maarufu kama “Mabasi ya Mwendokasi” - UDART. Kwa wakazi wa Dar mtakubaliana na mimi kwamba barabara za mradi huu kwa jinsi zilivyosasa zilikamilika muda mrefu sana, kukawa na ahadi zisizotekelezeka za uzinduzi wa huduma ya Mwendokasi. Tarehe zilikuwa zikibadilishwa kila kukicha hadi ikafikia hatua ya kuruhusu barabara hizo kutumiwa na magari mengine. Viongozi walikuwa na kigugumizi cha kuzindua huduma hiyo. Mapema baada ya Rais JPM kuingia madarakani akaamuru huduma hiyo ianze na kama kuna maboresho yafanyike huduma ikiendelea kutolewa. Cha ajabu hadi leo hakuna jipya kwenye mradi huo lililoongezwa na watu wanaendelea kufurahia huduma hiyo. Pengine Rais asingeamuru huduma hiyo kuanza, tungekuwa bado tunapewa tarehe za uzinduzi.

Kwa upande wa usafiri wa Treni ili kuokoa barabara zetu kama EL alivyosema Bungeni, tumeona mikataba ya ujenzi wa reli kwa kiwango cha “standard gauge” ikisainiwa, na michakato ya utekelezaji wa miradi hiyo ikionekana wazi katika maeneo ambapo miradi hiyo inajengwa. Na sasa mikataba ya Dar-Moro, na Moro-Makutopora imekwisha sainiwa na utekelezaji wake umeanza. Aidha katika kuziokoa barabara zetu mradi mkubwa wa bomba la mafuta toka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania umekwisha zinduliwa na utekelezaji umeanza. Kwa kifupi ni kuwa kuna miradi mingi sana ambayo inatekelezwa kwa spidi ya mwanga kiasi kwamba haitawezekana kuiorodhesha yote hapa; ikiwa ni pamoja na juhudi kubwa za kulinda rasilimali zetu kwa manufaa ya vizazi vyetu na vijavyo. Rais JPM hataki tena Tanzania kuwa “shamba la bibi” kwenye rasilimali zetu au kichwa cha mwendawazimu katika miradi mbalimbali.

Watanzania wote tunatamani Rais atufikishe Kanaani, nchi yenye maziwa na asali. Ni kweli kuwa ana jukumu la kutuongoza tufike huko. Lakini na sisi tuna wajibu zetu za kuzitimiza. Tunapaswa kushirikiana naye kwa nguvu zetu, na akili zetu zote ili kuhakikisha kuwa mipango inayowekwa na serikali inafanikiwa kwa kiasi kikubwa. Asipatikane mtu wa kusema “Je, si afadhali kwetu turudi Misri?”. Mtu wa aina hiyo tumkatae kwani atatuchelewesha katika kupiga hatua kubwa (au kusogea mbele) kimaendeleo. Kuna viwanda vinahitaji malighafi toka mashambani, basi wakulima limeni sana. Wawekezaji wa ndani wekezeni sana. Wafanyakazi katika sekta zote za umma na binafsi fanyeni kazi kwa bidii sana. Wafanyabiashara fanyeni biashara kwa bidii sana na kulipa kodi stahiki kwa hiari. Kila mmoja wetu afanye kitu kitakachosogeza maendeleo ya nchi mbele chini ya mazingira wezeshi yanayotengenezwa na serikali ya awamu ya tano.

Tukishindwa kufanya maendeleo makubwa chini ya Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu, kuna uwezekano wa kurudi nyuma au kutosogea mbele kabisa kwa muda mrefu kama awamu ya sita itakuwa na Rais mwoga katika kufanya maamuzi magumu. Tuitumie fursa hii kujiendeleza binafsi na kuiendeleza nchi yetu.

Benmpo
 
Magufuli anaturudisha nyuma kimaendeleo anataka watu tuishi kama mashetani,anafungia fungia vyombo vya habari yani anataka tuishi kama enzi za ujima,analeta sheria Kali kisa anaogopa kukosolewa,kama anaminya Uhuru kwa watu wake hayo yote anayofanya ni kazi bure,mpaka sasa bado sijamkubali kabisa magufuli naona anazingua tu

Sitaki povu hapa ,peleka kwa mkeo/mmeo kafulie chupi
 
Binafsi naisubiri kwa hamu awamu ya sita na naomba Mungu iwe kama ya nne. Japo awamu ya nne uozo mwingi ila mambo yalikuwa yanasonga, ila awamu hii uozo mwingi zaidi, mambo hayaendi, yaani kila kitu ovyo kabisa. Tumerudi nyuma kwa kasi ya ajabu sana, tupo enzi za ujima
 
Binafsi naisubiri kwa hamu awamu ya sita na naomba Mungu iwe kama ya nne. Japo awamu ya nne uozo mwingi ila mambo yalikuwa yanasonga, ila awamu hii uozo mwingi zaidi, mambo hayaendi, yaani kila kitu ovyo kabisa. Tumerudi nyuma kwa kasi ya ajabu sana, tupo enzi za ujima

Bro sasa hivi sasa sehemu nyingi zimeimarika balaa. Ukienda ofisi za umma unajiona kabisa kwamba wewe ni mteja. Zamani sijui walikuwa wanatuchukuliaje!! Zile mambo za njoo kesho, njoo lini zimeisha kabisa kwa sasa. Full heshima na kazi
 
Magufuli anaturudisha nyuma kimaendeleo anataka watu tuishi kama mashetani,anafungia fungia vyombo vya habari yani anataka tuishi kama enzi za ujima,analeta sheria Kali kisa anaogopa kukosolewa,kama anaminya Uhuru kwa watu wake hayo yote anayofanya ni kazi bure,mpaka sasa bado sijamkubali kabisa magufuli naona anazingua tu

Sitaki povu hapa ,peleka kwa mkeo/mmeo kafulie chupi
emoji41.png
emoji41.png
emoji41.png

Hakuna anayetoa povu mkuu, hayo nawe ni mawazo yako dhidi ya Mheshimiwa Rais. Lakini kwangu ukweli utabaki pale pale kwamba kwa sasa kila kinachoahidiwa nina matumaini kwamba kitatekelezwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali. Tumelishwa ahadi nyingi sana. Ni bora ukaahidi machache ukatekeleza kuliko kuahidi mengi ukatuchinjia baharini. Kwa upande wa hoja yako ya vyombo vya habari kufungiwa, kama kweli vimetenda makosa basi vinastahili kufungiwa ila kama vimefungiwa kimakosa sometimes lawama ziwaendee watendaji wake kwani si kila kitu kinaagizwa na Rais. Tumeona mara nyingi akitengua maamuzi ya Mawaziri na watendaji wengine serikalini.
 
Habari za leo Wanajamvi,

Kwa kipindi kirefu Watanzania tulikuwa na shauku ya kupata Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu katika utendaji wake. Maamuzi ambayo yangelinufaisha Taifa huku pengine yakizua malalamiko kwa baadhi ya watu au lawama kwa baadhi ya ndugu na marafiki wa kiongozi huyo.

Kuna wakati Mh. Edward Lowassa akichangia Bungeni, huku akipigiwa makofi na Wabunge wengi, alipata kusema (nanukuu): “Tatizo la nchi hii mnazungumza mambo, mnazungumza hakuna utekelezaji. Tunazunguza lakini discipline ya Malaysia na hapa ni tofauti. Hapa kuna Uswahili mwingi wa kukaa bila kutekeleza mambo, mnaamua hamtekelezi. Inatakiwa chombo kinachoweza kufanya maamuzi magumu na yakawa maamuzi magumu yanayotekelezeka kweli kweli. Mkishakubaliana mambo yafanyike. Haiwezekani katika nchi kila mtu akawa analalamika, kiongozi analalamika, mwananchi analalamika” (mwisho wa kunukuu). Kutokana na hali ilivyokuwa, ya kutotekeleza makubaliano mara kwa mara EL pia alidai kuwa “Ni bora kufanya maamuzi na kulaumiwa kuliko kutofanya kabisa”. Aidha katika mchango wake huo EL aligusia maeneo mbalimbali yaliyohitaji maamuzi magumu kama vile foleni Jijini Dar, Reli ya Kati, na mengineyo.

Nilikubaliana na hoja za EL kwa asilimia 100%. Ni ukweli usiopingika kuwa miradi mingi ilizinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi kwa mbwembwe nyingi iwe na viongozi wa serikali, viongozi wa mbio za Mwenge na wengineo, lakini miradi hiyo haijatekelezwa hadi leo. Bungeni kulijaa maazimio yenye matumaini lakini yote hayo hayakutekelezwa. Miradi mingi imeozea kwenye madimbwi ya “Tupo kwenye upembuzi yakinifu (feasibility study)” na “Tupo kwenye mchakato (process)”. Ilikuwa ukisikia madimbwi hayo mawili unajua tu hakuna kitu kinachoendelea, na yalishamiri sana hasa kisiasa katika kuzipotezea mantiki hoja zenye mlengo wa kuhoji maendeleo yake. Ni upembuzi yakinifu au mchakato ambao ulikuwa huwezi kuona mtu au kitu chochote katika eneo la mradi (site) kwa miaka mingi. Kwa kweli hayo madimbwi yalichosha watu wengi sana.

Mwaka 2015 ulifanyika uchaguzi mkuu na kumpata Rais John Magufuli. Ni Rais aliyependwa na watu wengi sana, waliompa kura na wale ambao hawakumpa kura pia. Nasema hivyo kwa sababu watu wengi walikiri kuwa Rais Magufuli ana uwezo mkubwa lakini wasingempa kura kwa sababu chama alichopeperusha bendera yake hawakukipenda. Lakini yeye JPM aliwahakikishia watu kuwa baada ya kuchaguliwa angeweza kufanya “Total system overhaul”; hali iliyopelekea watu wengi pia kumwamini na kumchagua kuwa Rais wa awamu ya tano. Ni Rais aliyebeba matumaini ya wengi, na aina ya Rais aliyekuwa ni ndoto ya watu wengi akiwemo EL (rejea quotation ya EL hapo juu).

Baada ya Rais JPM kuapishwa wote tuliona bidii zake. Kuna wengine walisema zilikuwa ni nguvu za soda lakini tunaona huu ni mwaka wa pili yupo at constant speed. Ni Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu na sisi sote tunaoona ni vema na haki (it’s right and just) kuongea ukweli tunampongeza.

Katika utawala wake tumeona kuwa madimbwi ya “mchakato” na “upembuzi yakinifu” yamekuwa ya kiutendaji zaidi na si ya kuua miradi/mipango. Tumeshuhudia mawe ya msingi yakiwekwa au maagizo yakitolewa; mapema tunaowaona watu katika maeneo ya miradi au kazi nyinginezo. Kwa mfano tumeona siku moja baada ya Rais kuliagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kujenga ukuta kuuzunguka mgodi wa madini ya Tanzanite huko Mererani, watu wameonekana katika eneo la mradi wakifanya upembuzi yakinifu kwa hatua za utekelezaji. Kwa kweli ni suala la kupongezwa kwani kila aina ya uzembe au ubadhirifu kwa baadhi ya Viongozi au watendaji hauna nafasi kwake.

EL alizungumzia suala la foleni Jijini Dar. Mbali na miradi miwili mikubwa ya Ubungo Interchange na Flyovers pale TAZARA ambayo inaendelea kwa kasi baada ya kuzinduliwa na Rais JPM, pia kulikuwa na Mradi wa Magari yaendayo kasi maarufu kama “Mabasi ya Mwendokasi” - UDART. Kwa wakazi wa Dar mtakubaliana na mimi kwamba barabara za mradi huu kwa jinsi zilivyosasa zilikamilika muda mrefu sana, kukawa na ahadi zisizotekelezeka za uzinduzi wa huduma ya Mwendokasi. Tarehe zilikuwa zikibadilishwa kila kukicha hadi ikafikia hatua ya kuruhusu barabara hizo kutumiwa na magari mengine. Viongozi walikuwa na kigugumizi cha kuzindua huduma hiyo. Mapema baada ya Rais JPM kuingia madarakani akaamuru huduma hiyo ianze na kama kuna maboresho yafanyike huduma ikiendelea kutolewa. Cha ajabu hadi leo hakuna jipya kwenye mradi huo lililoongezwa na watu wanaendelea kufurahia huduma hiyo. Pengine Rais asingeamuru huduma hiyo kuanza, tungekuwa bado tunapewa tarehe za uzinduzi.

Kwa upande wa usafiri wa Treni ili kuokoa barabara zetu kama EL alivyosema Bungeni, tumeona mikataba ya ujenzi wa reli kwa kiwango cha “standard gauge” ikisainiwa, na michakato ya utekelezaji wa miradi hiyo ikionekana wazi katika maeneo ambapo mradi hiyo inajengwa. Na sasa mikataba ya Dar-Moro, na Moro-Makutopora imekwisha sainiwa na utekelezaji wake umeanza. Aidha katika kuziokoa barabara zetu mradi mkubwa wa bomba la mafuta toka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania umekwisha zinduliwa na utekelezaji umeanza. Kwa kifupi ni kuwa kuna miradi mingi sana ambayo inatekelezwa kwa spidi ya mwanga kiasi kwamba haitawezekana kuiorodhesha yote hapa; ikiwa ni pamoja na juhudi kubwa za kulinda rasilimali zetu wa manufaa za vizazi vyetu na vijavyo. Rais JPM hataki tena Tanzania kuwa “shamba la bibi” kwenye rasilimali zetu au kichwa cha mwendawazimu katika miradi mbalimbali.

Watanzania wote tunatamani Rais atufikishe Kanaani, nchi yenye maziwa na asali. Ni kweli kuwa ana jukumu la kutuongoza tufike huko. Lakini na sisi tuna wajibu zetu za kuzitimiza. Tunapaswa kushirikiana naye kwa nguvu zetu, na akili zetu zote ili kuhakikisha kuwa mipango inayowekwa na serikali inafanikiwa kwa kiasi kikubwa. Asipatikane mtu wa kusema “Je, si afadhali kwetu turudi Misri?”. Mtu wa aina hiyo tumkatae kwani atatuchelewesha katika kupiga hatua kubwa (au kusogea mbele) kimaendeleo. Kuna viwanda vinahitaji malighafi toka mashambani, basi wakulima limeni sana. Wawekezaji wa ndani wekezeni sana. Wafanyakazi katika sekta zote za umma na binafsi fanyeni kazi kwa bidii sana. Wafanyabiashara fanyeni biashara kwa bidii sana na kulipa kodi stahiki kwa hiari. Kila mmoja wetu afanye kitu kitakachosogeza maendeleo ya nchi mbele chini ya mazingira wezeshi yanayotengenezwa na serikali ya awamu ya tano.

Tukishindwa kufanya maendeleo makubwa chini ya Rais mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu, kuna uwezekano wa kurudi nyuma au kutosogea mbele kabisa kwa muda mrefu kama awamu ya sita itakuwa na Rais mwoga katika kufanya maamuzi magumu. Tuitumie fursa hii kujiendeleza binafsi na kuiendeleza nchi yetu.

Benmpo

Kwa kweli umeongea ukweli mtupu. Nimepita vijijini huko full umeme. REA wanasambaza umeme kwa kasi kubwa sana. Unaona kabisa watu wanavyofurahia maisha. Awamu za nyuma zimeviacha vijiji vingi sana vikiwa gizani lakini kwa huu muda mfupi tu wa JPM madarakani unaona tofauti kubwa sana. Zamani ilikuwa ukiingia hospitali hakuna anayekutazama kama mgonjwa kweli, ila kwa sasa ili CUSTOMER CARE unaiona kabisa, na ofisi nyingi tu. Watu tunaheshimiana sana. Hata kama ni kwa woga sasa hivi, but tukifanya kwa muda mrefu itabadilika na kuwa tabia yetu ya kudumu kwani watoto wetu wanajifunza hata kwa kuona. BRAVO MAGU!!!
 
Watu wa ufipa hapa utawaona tuu.MANYUMBU MANYUMBU MKO WP!!!??? NJONI NA MATUSI YENU, WAZEE WA KILALAMIKA,

Ila ingependeza sana kama wangekuja na challenges na siyo kutukana. But kwa watu fulani hivi ukiweka uzi tegememea matusi toka kwao
 
Wakati Edward Lowassa akitoa maneno hayo hakuna sehemu aliyosema maamuzi magumu yafanyike kwa kuvunja sheria.
Unaweza toa maamuzi magumu kwa kufwata sheria na hapo wala usingeona mtu analalamika.
Shida ya Magu ni kuafanya maamuzi hata ya kuvunja sheria na Bahati mbaya hata akiambiwa kuwa hapa umekosea yeye humuona mtu msaliti sasa kiongozi wa namna hiyo hatufai.
Uongozi ni shirikishi lkn yeye hufikili anajua kila kitu na yeye ndiye mwenye haki ya kila kitu.
Hakika nakwambia pamoja na nia nzuri ya Raisi yuko njiani kushindwa kabisa tena huyu utakua Raisi atakaeshindwa vibaya na watu watashangaa sana.
MTU AJIDHANIAE KUA AMESIMAMA ANGALIE ASIANGUKE KWANI AKIANGUKA ANGUKO LAKE LITAKUA ANGUKO KUU NA HATA AMKA TENA
 
Hakuna anayetoa povu mkuu, hayo nawe ni mawazo yako dhidi ya Mheshimiwa Rais. Lakini kwangu ukweli utabaki pale pale kwamba kwa sasa kila kinachoahidiwa nina matumaini kwamba kitatekelezwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali. Tumelishwa ahadi nyingi sana. Ni bora ukaahidi machache ukatekeleza kuliko kuahidi mengi ukatuchinjia baharini. Kwa upande wa hoja yako ya vyombo vya habari kufungiwa, kama kweli vimetenda makosa basi vinastahili kufungiwa ila kama vimefungiwa kimakosa sometimes lawama ziwaendee watendaji wake kwani si kila kitu kinaagizwa na Rais. Tumeona mara nyingi akitengua maamuzi ya Mawaziri na watendaji wengine serikalini.
Millioni 50 kila kijiji VP mkuu
Mikopo iliyo stahiki kwa wanafunzi vyuo vikuu VP mbona inatolewa kiubaguz na haitoshi
Laptop kwa kila mwalimu VP mkuu au hamjamkumbusha
Mahakama ya mafisadi nayo
Vingi ulivyoongea hapo ni project za rais mstaafu jk
Labda miradi yake kama yake mipya ni miwili (hayo ya uwanjawa ndege chato sitoliongelea)..ni ukuta wenu wa mererani na hiz hostel za hapa mabibo na hata barabara ya mwenge-moroco tulipigwà changa LA macho kumbe ni msaada kutoka kwa wajapani (ambapo jk aliacha keshaweka mambo sawa ni utekelezaji tu)....kwangu mm alilofanya mpaka sasa zaidi ya miaka miwili kurudisha nidhamu utumishi wa umma na kufanya wafanyabiashara na hasa wenye viwanda kuwa na adabu na wafanyakazi weusi...sio siri kupitia kauli na amri za magufuli nimefanikiwa kuajiliwa kwa mkataba mzur kwenye kiwanda ninachofanyia kazi na wazirhakauki kuja hapa wakati utawala wa jk tulikuwa tunatukanwa hatukusoma japo tunaoperate production lkn ktk malipo wanaotusimamia ambao ni wahindi ndo walokuwa wanathaminika lkn kwa sasa hali ni tofauti....tatizo langu mm na magu demokrasia ndo ugomvi wangu mi na yeye...kufinya demokrasia ndo kumezalisha kila aina ya mtafaruku nchi hii...wakati huo huo hiyo demokrasia ndo iliyomfikisha hapo alipo inakuaje anaichukia..na hasa kumkosoa kwani yeye mungu asikosolewe...hata mungu mwenyewe wakati mwingine anakosolewa sembuse yeye....
 
Maamuzi magumu yaweza kuwa kwa mujibu wa sheria au mujibu wa udikteta!
Ninachoona hapa, umeshaanza kuisoma namba. Si ajabu huko mbeleni ukaja na mtazamo mwingine!
 
Maamuzi magumu yaweza kuwa kwa mujibu wa sheria au mujibu wa udikteta!
Ninachoona hapa, umeshaanza kuisoma namba. Si ajabu huko mbeleni ukaja na mtazamo mwingine!

Naweza kuisoma kwa mambo fulani lakini si yote. Ukweli lazima usemwe. Kama mambo yatabadilika nami nitasema tofauti, lakini kwa sasa nitasimamia msimamo wangu. In fact huwezi furahishwa na yote lakini kwa kiasi kikubwa amerekebisha uozo uliokuwepo awali
 
Kwa kweli umeongea ukweli mtupu. Nimepita vijijini huko full umeme. REA wanasambaza umeme kwa kasi kubwa sana. Unaona kabisa watu wanavyofurahia maisha. Awamu za nyuma zimeviacha vijiji vingi sana vikiwa gizani lakini kwa huu muda mfupi tu wa JPM madarakani unaona tofauti kubwa sana. Zamani ilikuwa ukiingia hospitali hakuna anayekutazama kama mgonjwa kweli, ila kwa sasa ili CUSTOMER CARE unaiona kabisa, na ofisi nyingi tu. Watu tunaheshimiana sana. Hata kama ni kwa woga sasa hivi, but tukifanya kwa muda mrefu itabadilika na kuwa tabia yetu ya kudumu kwani watoto wetu wanajifunza hata kwa kuona. BRAVO MAGU!!!
Kwani REA ni project aloileta maguful nyie mbona hamfuatilii mambo ya nchi yenu au tunacomments kwa kuwa bandle ni la kwetu
 
Wakati Edward Lowassa akitoa maneno hayo hakuna sehemu aliyosema maamuzi magumu yafanyike kwa kuvunja sheria.
Unaweza toa maamuzi magumu kwa kufwata sheria na hapo wala usingeona mtu analalamika.
Shida ya Magu ni kuafanya maamuzi hata ya kuvunja sheria na Bahati mbaya hata akiambiwa kuwa hapa umekosea yeye humuona mtu msaliti sasa kiongozi wa namna hiyo hatufai.
Uongozi ni shirikishi lkn yeye hufikili anajua kila kitu na yeye ndiye mwenye haki ya kila kitu.
Hakika nakwambia pamoja na nia nzuri ya Raisi yuko njiani kushindwa kabisa tena huyu utakua Raisi atakaeshindwa vibaya na watu watashangaa sana.
MTU AJIDHANIAE KUA AMESIMAMA ANGALIE ASIANGUKE KWANI AKIANGUKA ANGUKO LAKE LITAKUA ANGUKO KUU NA HATA AMKA TENA
Ukitaka kuwa msafi ni lazima ujitazame kwenye kioo ili upate taswira ya mahala palipo haribika upate kurekebisha!
Hakuna aliye mkamilifu katika dunia hii.
Ni kosa kubwa na ni anguko kuu kujikweza na kukataa kukosolewa. Kufanya hivyo ni kujipunguzia maarifa.
Ni makosa pia kutaka kufanya kila neno litokalo kinywani liwe sheria.
 
Bro sasa hivi sasa sehemu nyingi zimeimarika balaa. Ukienda ofisi za umma unajiona kabisa kwamba wewe ni mteja. Zamani sijui walikuwa wanatuchukuliaje!! Zile mambo za njoo kesho, njoo lini zimeisha kabisa kwa sasa. Full heshima na kazi

mkuu unahudumiwa sehemu zipi z umma?

TRA?
BRELA?
MAHAKAMA?
HALIMASHAURI?

NIPEFORMULA UNAYOTUMIA KUHUDUMIWA KAMA MTEJA SEHEMU HIZO
 
Uzi wako ni mrefu sana, ntausoma nikiwa kaunta bar badae jioni,

Kila la kheri mkuu. Ila urefu wake umetokana na mambo mengi mazuri yaliyofanywa ambayo watu hawataki kuyasema. Hata hivyo nime-summerise sana. Nimeona kuna mdau amezungumzia REA hapo, niliikumbuka lakini nikaona nikiiandika uzi utazidi urefu na mambo mengine mengi. Nadhani kila mmoja analo la kushuhudia
 
Back
Top Bottom