Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,443
- 40,537
Tangu baada ya Rais Magufuli kuhutubia Taifa kupitia kwa wazee wa Dar es salaam, nimeona kuna mabadiliko (Twist) kwenye mitizamo ya baadhi yetu humu JF. Tayari ile mitizamo mikali dhidi ya mawazo chanya ya wenzetu imebadilika.
Kuna wale waliokuwa wanaona Magufuli hawezi kukosea, nao wameanza kuona kumbe kwa kuwa Magufuli ni mwanadamu naye pia hukosea. Lakini wapo pia walionza kwa kuamini kwamba Magufuli atafanana kwa kila kitu na Kikwete kiutendaji na kimtazamo, nao pia wameanza kubadili misimamo yao.
Lakini Magufuli ndiye Rais wetu na anaoongoza serikali inayoendeshwa kwa Kodi zetu au inayotokana na dhamana ya nchi yetu. Kama taifa tusipojenga tabia ya kuyatazama matatizo yetu kwa jicho la kitanzania badala yake tukawa tuyachambua na kuyaangalia kwa jicho la misingi ya vyama vyetu hatutapiga hatua Abadan.
Tuangalie kama kweli tunataka kujenga viwanda ni viwanda vya aina gani vijengwe, malighafi yake itapatikana nchi mwetu, itaajiri kiasi gani cha watu wetu, kitaleta aina gani ya teknolojia mpya, kitalipa kodi kiasi gani na kitashiriki vipi kuujenga uchumi wa nchi yetu ili uwe imara?
Kama kuna nyanja mbali mbali tunazotaka ziwe bora kuliko zilivyo hivi sasa tunatakiwa tufanye nini ili ziboreke. Badala ya kurushiana vijembe kutwa kucha, ni wakati wa kutumia mbongo zetu kuibadili Tanzania yetu kwa faida ya sasa na kwa vizazi vijavyo!!
Hata hivyo mpishano wa tafakuri juu ya mambo hayo ni lazima utakuwepo!!
Kuna wale waliokuwa wanaona Magufuli hawezi kukosea, nao wameanza kuona kumbe kwa kuwa Magufuli ni mwanadamu naye pia hukosea. Lakini wapo pia walionza kwa kuamini kwamba Magufuli atafanana kwa kila kitu na Kikwete kiutendaji na kimtazamo, nao pia wameanza kubadili misimamo yao.
Lakini Magufuli ndiye Rais wetu na anaoongoza serikali inayoendeshwa kwa Kodi zetu au inayotokana na dhamana ya nchi yetu. Kama taifa tusipojenga tabia ya kuyatazama matatizo yetu kwa jicho la kitanzania badala yake tukawa tuyachambua na kuyaangalia kwa jicho la misingi ya vyama vyetu hatutapiga hatua Abadan.
Tuangalie kama kweli tunataka kujenga viwanda ni viwanda vya aina gani vijengwe, malighafi yake itapatikana nchi mwetu, itaajiri kiasi gani cha watu wetu, kitaleta aina gani ya teknolojia mpya, kitalipa kodi kiasi gani na kitashiriki vipi kuujenga uchumi wa nchi yetu ili uwe imara?
Kama kuna nyanja mbali mbali tunazotaka ziwe bora kuliko zilivyo hivi sasa tunatakiwa tufanye nini ili ziboreke. Badala ya kurushiana vijembe kutwa kucha, ni wakati wa kutumia mbongo zetu kuibadili Tanzania yetu kwa faida ya sasa na kwa vizazi vijavyo!!
Hata hivyo mpishano wa tafakuri juu ya mambo hayo ni lazima utakuwepo!!