Tuanze na Ufumbuzi Wa Kudumu

Pius J. Kiwarya Lema

JF-Expert Member
Nov 14, 2013
1,096
562
Msukumo Wa Kuendelea Mbele na Rasilimali za Taifa:

Tuanze na Ufumbuzi wa Kudumu :

Watanzania Tunarudià Makosa yaleyale !

Kinachoonekana kwa SAA chache mara baada ya ripoti kutolewa, kunadhiirisha kutokujitambua kwetu kama MTU mmojammoja.

Tujue Hakuna chochote kitakachofanyika kama wale waliotufikisha hapa wanashangilia .
Sisi Watanzania ndio tuliolifikisha Taifa letu hapa lilikofika ,kwa sababu hatujui tunataka nini ?
Ukitazama maoni yetu kwa dakika hizi chache tu utaona tunataja majina ya watu yachukuliwe hàtua ! lakinj sio ufumbuzi wa kudumu

Kwa maoni yangu Watanzania kuanza kushabikia kutaja majina ili wachukuliwe hatua hakujawahi kutusaidia wakati wowote .
Nchi ambayo katiba inatoa haki Kwa mkono Wa kulia ( sheria mama) na kuipoka Kwa mkono wa kushoto (kanuni zinazotungwa na hao hao) tusahau kama hakuna Strong Institution !

Kazi yetu ya kwanza inapaswa iwe ni kuhimiza namna bora ya kuwa na "strong institution " haraka iwezekanvyo ! Yaani katiba ya wananchi

Tuachane na kazi ya Majina au kupongeza na kusifia mambo ambayo tumeyapigia makelele miaka yote lakini hatukusikilizwa .. .....

Ukitaja majina nani atabakia toka 1998 ? Yatakuwa kama yale ya EPA na ESCROW ! Majina yalitajwa kiko wapei ?

Najiuliza swali moja leo kuna agizo limetolewa mikataba ipitiwe upya hilo ni zuri ;
Lakini Nchi inaongozwa Kwa sheria ;na sheria ya mikataba inasema mikataba ni siriI!
Je Mswada ukipelekwa bungeni leo ili kufanya sheria itakayoondoa usiri huo
Je ni wabunge wake wale watoka 1998,,watakoipitisha au kuna wengine tumewachagua ?

Ndiyoooooo ??

Bila Strong institution tutakesha !tukitegemea utashi Wa mtu mmoja
tunajidanganya !

Tuanze na mambo ya Kudumu na ya Msingi !

Strong Instution
Katiba ya watanzania
 
Tatizo ni kwamba wewe kama mtanzania mmoja unaweza kufanya jambo gani mbele ya manyangumi yenye mapembe na mijino ngiiiii
kumbuka chupi haina mpasuo
[HASHTAG]#HappyAnniversaryToMeInJF[/HASHTAG]
 
Nakuambia sijawahi kubebwa na ushabiki kama huuu unaoendelea waliotuletea haya ndio walioyatengeneza halafu
Wananataka tuwaunge mkono kabla ya kutekeleza matakwa yetu.!

Tuwe na subira kabla ya kushangilia ahadi zile zile za kila siku.

Ni Mara ngapi tumeahidiwa mikataba itapitiwa lakini wakishapata kiki wanapotezea ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom