TTCL na huduma ya internet


Achana nao, sio lazima uwe na Internent ya TTCL kama mwanzo ndio huo kuna uwezekano wa kupata usumbufu zaidi hapo baadae! Tumia Zantel au Sasatel.
 
Achana nao, sio lazima uwe na Internent ya TTCL kama mwanzo ndio huo kuna uwezekano wa kupata usumbufu zaidi hapo baadae! Tumia Zantel au Sasatel.

Asante mkuu kwa ushauri. Tatizo tayari nimelipia connection fee, nimenunua modem na tayari nimelipia hiyo huduma kwa mwezi mzima Tshs. 60,000 sasa nikiachananao si itakuwa imekula kwangu? Najua itakuwa taabu kuwaambia warudishe pesa zangu ili niende kwa service provder mwingine. Nafikiri wananifanyia hivyo kwa kuwa tayari wana pesa yangu, lakini je kwenye biashara ya ushindani approach hii inafaa? Wataweza kudumu kwenye ushindani?

Tiba
 
mie ya kwangu net iko poa ila simu haifanyi kazi mwaka na nusu sasa nisharipoti weeee mpaka nimechoka juzi nimeenda mwenyewe pale plaza na wakampigia simu fundi mbele yangu na wakampa na namba zangu kama atapotea, hivi ninavyo sema nina wiki naendelea kumvumilia labda ana kazi nyingi sana
 
BOL haifanyi kazi vizuri hapa nilipo/nilipohamia kama ilivyokuwa kule nilipokuwa naishi zamani na wanasema hakuna coverage hivyo hakuna jinsi. Sasa nataka kuhama mtandao, nihamie wapi? Sitaki kurudi TTCL maana waliniboa sana na yale masimu ya HUAWEI, yalikuwa slow sana! Huwa siamini vipya vinyemi hivyo naogopa kwenda SASATEL! Sasa, je, nichague ipi kati ya hizi:

SIMBANET

AFRICAONLINE

IWAY

ZANTEL

VODACOM

?
 

Mkuu Waukae,

Sasa kama tatizo ni fundi si waongeze mwingine au watafute kwenye customer service centre nyingine kwa muda ili kukabiliana na matakwa ya wateja? Ningesikiliza ushauri wa rafiki yangu, nisingekuwa hapa nalalamika. Hivi landline kama haifanyi kazi bado internet inakuwa inafanya kazi?

Tiba
 
Pole, That is one isolated case, TTCL broadband is the fastest, cheapest na most reliable!. 40,000/= per month, you enjoy unlimited wireless 24/7.

Pasco, we mwenzetu unalipia wapi hizo 40,000/= per month unlimited TTCL wireless? Mimi natumia hiyo hiyo lakini nalipa 45,ooo/ per month na siku nyingine nalazimika kulipa 50,000/= kwa sababu hawana voucher za 5,000/=!!
 
Mkuu pole, hujafa hujaumbika. kwani wewe ni mgeni na utaratibu wetu ukitaka huduma ? hasa kwenye mashirika yetu haya? hebu tafakari kuna mahali UNAKOSEA.

kweli mkono mtupu aulambwi ndipo anapokosea tu
 

PIGA # 100 katika cmu yako landline omba watu wa broadband, utahudumiwa, wanajitahidi kwa kweli!!!!!!!!!!1111
 


kwa ushauri wangu nakushauri uchukue zantel evdo modem 226 zipo fasta zaidi ya ttcl nimejaribu hilo na wanapakeji nzuri
 


ndo kawaida yao ni wazembe ninachoshangaa kwann wanapoteza pesa nyingi kutanga
 
PIGA # 100 katika cmu yako landline omba watu wa broadband, utahudumiwa, wanajitahidi kwa kweli!!!!!!!!!!1111

Wakuu,

Kumbe JF inasadia mambo mengi sana. Kupiga kelele tu jana sasa hivi nimepigiwa simu mafundi wako nyumbani kwangu wanachakarika kufunga hiyo internet. Nawashukuru wote walionipa mchango wa mawazo. Nitawafahamisha performance yake ikoje nikishaanza kutumia.

Tiba
 
:smile-big: happy for u bro !
Sasa, vipi ? ina fanya kazi vizuri ?
mi natafuta kununuwa internet, lakini sijue kama ttcl ipo UNLIMITED ? na shs ngapi ?
plz can u advise ?
 
:smile-big: happy for u bro !
Sasa, vipi ? ina fanya kazi vizuri ?
mi natafuta kununuwa internet, lakini sijue kama ttcl ipo UNLIMITED ? na shs ngapi ?
plz can u advise ?

Duh! mzee, hii post ya February umeifufua! we mkali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…