Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,505
- 911,249
- Thread starter
-
- #1,321
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"]Ulimboka, Walulya watemwa Simba [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] Send to a friend [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"] Tuesday, 27 December 2011 20:51 [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] 0digg
Majuto Omary
SIMBA imewaengua beki wa kimataifa wa Uganda, Dereck Walulya na winga Ulimboka Mwakingwe na kuwajumuisha chipukizi watano kwenye kikosi cha wachezaji 24 kitachoshirki mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF.
Mbali ya Walulya na Mwakingwe mchezaji mwingine aliyeachwa kwa sababu za kiufundi ni mshambuliaji Rajabu Isihaka.Kuachwa kwa Walulya kunaifanya Simba kubaki na wachezaji wanne wa kigeni kwenye kikosi chake ambao ni Felix Sunzu, Gervais Kago, Emmanuel Okwi na Patrick Mafisango.
Akizungumza na gazeti hili mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Simba, Ibrahim "Maestro" Masoud alisema kwa sasa timu hiyo imepeleka usajili wa wachezaji 24 tu kwa ajili ya mashindano hayo ya pili kwa ukubwa kwa hatua za klabu barani Afrika.
Alisema uamuzi wa kuwaacha wachezaji hao watatu uliangalia vitu vingi na moja ni kutoa nafasi kwa klabu kusajili tena kama watafanikiwa kufuzu kwa hatua ya makundi ya mashindano hayo.
Katika kuimarisha timu hiyo kocha Milovan Cirkovic amependekeza majina ya wachezaji watano kutoka timu ya vijana na kujiunga na timu hiyo ya wakubwa.Chipukizi walioteuliwa ni pamoja na Hassan Khatibu, Jonas Mkude, Abdallah Seseme, Edward Christopher, Frank Sekule na Ramadhani Singano.
Kocha Milovan amevutiwa sana na kiwango kinachoonyeshwa na timu ya vijana na hakuna shaka kwamba baadhi ya chipukizi hao wakapata nafasi ya kucheza kwenye mashindano hayo.
Simba itaanza kampeni yake ya kusaka kurudia mafanikio yake ya mwaka 1993 kwenye michuano hiyo kwa kucheza na Kiyovu FC ya Rwanda ugenini kati ya Februari 17-19 na wiki mbili baadaye watarudiana hapa Dar es Salaam.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"]Ulimboka, Walulya watemwa Simba [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] Send to a friend [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"] Tuesday, 27 December 2011 20:51 [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] 0digg
Majuto Omary
SIMBA imewaengua beki wa kimataifa wa Uganda, Dereck Walulya na winga Ulimboka Mwakingwe na kuwajumuisha chipukizi watano kwenye kikosi cha wachezaji 24 kitachoshirki mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF.
Mbali ya Walulya na Mwakingwe mchezaji mwingine aliyeachwa kwa sababu za kiufundi ni mshambuliaji Rajabu Isihaka.Kuachwa kwa Walulya kunaifanya Simba kubaki na wachezaji wanne wa kigeni kwenye kikosi chake ambao ni Felix Sunzu, Gervais Kago, Emmanuel Okwi na Patrick Mafisango.
Akizungumza na gazeti hili mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Simba, Ibrahim "Maestro" Masoud alisema kwa sasa timu hiyo imepeleka usajili wa wachezaji 24 tu kwa ajili ya mashindano hayo ya pili kwa ukubwa kwa hatua za klabu barani Afrika.
Alisema uamuzi wa kuwaacha wachezaji hao watatu uliangalia vitu vingi na moja ni kutoa nafasi kwa klabu kusajili tena kama watafanikiwa kufuzu kwa hatua ya makundi ya mashindano hayo.
Katika kuimarisha timu hiyo kocha Milovan Cirkovic amependekeza majina ya wachezaji watano kutoka timu ya vijana na kujiunga na timu hiyo ya wakubwa.Chipukizi walioteuliwa ni pamoja na Hassan Khatibu, Jonas Mkude, Abdallah Seseme, Edward Christopher, Frank Sekule na Ramadhani Singano.
Kocha Milovan amevutiwa sana na kiwango kinachoonyeshwa na timu ya vijana na hakuna shaka kwamba baadhi ya chipukizi hao wakapata nafasi ya kucheza kwenye mashindano hayo.
Simba itaanza kampeni yake ya kusaka kurudia mafanikio yake ya mwaka 1993 kwenye michuano hiyo kwa kucheza na Kiyovu FC ya Rwanda ugenini kati ya Februari 17-19 na wiki mbili baadaye watarudiana hapa Dar es Salaam.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]