Trafic eneo la vingunguti muogopeni Mungu

Trafic eneo la vingunguti muogopeni Mungu

Anold

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2010
Posts
1,456
Reaction score
615
Kwa mtu anayetumia barabara ya Nyerere huenda atakuwa ameliona au ameshawahi kukutana na dhahma hii hasa madereva. Unapotokea uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere unapofika eneo la vingunguti utakuta alama za zebra ambazo huonyesha eneo ambalo waenda kwa miguu wanatakiwa walitumie kuvukia ambapo mbele yake kuna taa za kuongozea magari.

Eneo hilo askari wa usalama barabarani wanalitumia vibaya kuwaonea wananchi ambao wanatumia barabara hiyo kwani endapo utafika eneo hilo la kuvukia watu ukasimamisha gari na baada ya kujiridhisha ukaaamua kwenda mbele ukikuta taa haziruhusu kupita basi ujue trafiki watakuja na kukutoa nje ya barabara na kukupiga faini huku wakijua wazi kuwa wanakuonea.

Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es Salaam tafadhari umulike eneo hili kwani hawa askari pamoja na ukweli kuwa wanaleta hizo faini kwako lakini nyingi hazijapatikana kwa halali na ni za uonevu. Ni kweli kuwa huenda sifa itapatikana mkitoa hesabu ya makusanyo ya faini ila hela ya dhulma italeta laana katika nchi pamoja na askari anayeisimamia. Ninaomba sana mkuu wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa wa Dar es Salaam Mkuu wa mkoa Paulo Makonda afanye utafiti wake eneo hili ili aone uonevu unaofanywa na hawa askari ambao wamekaa eneo hilo kuonea watu ambao wengine hawana kosa walilolifanya.
 
Hujaeleweka ndugu embu nyoosha maelezo, kama taa hazijaruhusu unataka upite hivyo hivyo au kosa ni nn ni hilo la kusimama hapo kwenye zebra...
 
Askari wetu wengi wa barabarani hawajui sheria wanazokomaa kuzisimamia. Wanageuka kuwa kero kubwa.
 
Hujaeleweka ndugu embu nyoosha maelezo, kama taa hazijaruhusu unataka upite hivyo hivyo au kosa ni nn ni hilo la kusimama hapo kwenye zebra...
Ni kwamba ukisimama pale kwenye zebra wao wanajua umezuia njia so wanakusubiri pale mbele kwenye mataa wakukamue 30,000
 
Ni kwamba ukisimama pale kwenye zebra wao wanajua umezuia njia so wanakusubiri pale mbele kwenye mataa wakukamue 30,000
Sasa umeblock zebra alafu wakuache tena hilo ni kosa la dhahiri kabisa, nadhani tuache kulia lia tifuate sheria za barabarani
 
mtoa mada una point lakini huwezi kujieleza

pale vingunguti ni kwamba unapaswa usimame nyuma ya zebra... ukisimama mbele ya zebra hata kama hujaiziba zebra... wanakuchukua na kukupiga faini..

ikatokea taa nyekundu ikawaka huku wewe umeshaipita zebra ukisimama tu kwao ni kosa.. hata kama hujaiziba wala kuikanyaga zebra
 
Wee mtoa mada, udereva ulisomea wapi...?
Kuna mambo mengine kweli trafic wanaonea sana raia, lakini mambo mengine huwa sisi tunajitakia wenyewe!
 
K
mtoa mada una point lakini huwezi kujieleza

pale vingunguti ni kwamba unapaswa usimame nyuma ya zebra... ukisimama mbele ya zebra hata kama hujaiziba zebra... wanakuchukua na kukupiga faini..

ikatokea taa nyekundu ikawaka huku wewe umeshaipita zebra ukisimama tu kwao ni kosa.. hata kama hujaiziba wala kuikanyaga zebra
Kweli kabisa ulichoandika kiongozi. Kuna uonevu sana pale.
 
Sasa umeblock zebra alafu wakuache tena hilo ni kosa la dhahiri kabisa, nadhani tuache kulia lia tifuate sheria za barabarani
sio amezuia zebra amesimama ili kupisha wapita kwa miguu wapite then aendelee na safari ila sasa wale askari wanatafsiri kama amezuia njia
 
Hujaeleweka ndugu embu nyoosha maelezo, kama taa hazijaruhusu unataka upite hivyo hivyo au kosa ni nn ni hilo la kusimama hapo kwenye zebra...
wewe ndiyo hujaelewa ngoja nikutoe ujinga: Umekuta zebra umesimama baada ya gari mbili zilizopo mbele yako kusimama, mara wa mbele anaenda kwa mwendo anaoujua, unavuka zebra mara taa nyekundu zimewaka hivyo kulazimika kusimama baada ya kuvuka zebra halafu trafiki anakuja anakuambia umevunja sheria maana umesimama baada ya zebra: kwa anayejua sheria za barabarani anaelewa kuwa hili jambo halipo ila kwa mbumbumbu wa sheria za barabarani kama wewe tutakesha
 
Back
Top Bottom