maliyamungu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2011
- 564
- 412
Kwa niaba ya wafanyabiashara wenzangu wa Kariakoo na wote mjue biashara Kariakoo imekuwa sasa ni kama tunawafanyia TRA kipato. Kinachofanyika siku hizi wanashinda kwa transporter wa magari ya mikoani wanakagua risiti kila mzigo, jambo sio baya kukagua lakini kinachouma mzigo lazima wautafutie kosa na wanaukamata wanapeleka store kwao. Watakutisha mpaka utoe rushwa na rushwa zao kuanzia milioni au wanakwambia fine 4.5 milion.
Kinachouma bora pesa ziingie Serikalini lakini wao wanachukua rushwa tu inauma sana. TAKUKURU muangalie hilo jamani wafanyabiashara tunalia na kufirisika.
Naomba kuwasilisha.
Kinachouma bora pesa ziingie Serikalini lakini wao wanachukua rushwa tu inauma sana. TAKUKURU muangalie hilo jamani wafanyabiashara tunalia na kufirisika.
Naomba kuwasilisha.