TRA hapa mtapata wakwepa kodi wadogo tu

Inkoskaz

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
6,372
2,374
Nimesikia Tamko la Kamishna wa elimu kwa mlipa kodi Bw.Kayombo akisema TRA watatoa zawadi ya asilimia 3 kwa watoa taarifa za ukwepaji kodi
Taarifa yake mbeleni inajifunga kwa kutoa maximum limit ya zawadi hiyo kuwa Ni milioni ishirini tu
Hii inamaanisha stahiki italipwa kwa kufichua kodi hafi milioni 670 tu zaidi ya hapo mtoa siri hatopata zaidi hata kama amefichua ukwepaji wa mabilioni
Mtazamo wangu ni kuwa wanatengeneza nafasi kati ya mfichuaji ukwepaji kula njama na mkwepa kodi na kulipana kiasi zaidi ya hiyo 20m na kuiacha solemba serikali
Ni fusk kwa mtoa taarifa ya ukwepaji mabilioni ya fedha halafu yeye akaambulia dola 9000 tu
 
Mbona hatoi Elimu kwa watumia kodi baada ya kukusanywa kila kukicha utasikia Lugumi..escrow 2..mishahara hewa na matakataka mengine ndio izo izo hela anazozitolea Elimu huku zikitafunwa vibaya na huko toa Elimu bhana...
 
Wao wanalipa au sababu wapo vitengo wanaangalia wengine tu ndo wanaotakiwa kulipa kodo?.
 
Wamezidi kutoza kodi sana ,juzi nimetoa gari limenunuliwa kwa £500 lakini hadi linatolewa kodi tu inafika £4000 sasa hapo kweli watu watashindwa kukwepa kodi jamani,yani kodi ya gari inazidi gharala za kununua gari+ usafiri wa gari kutoka nje,+gharama za bandari+ pesa ya agent kweli kwa namna hii watu wasikwepe kodi ?hapo bado Ami nao hawajafanya yao bado usumbufu huko pia ,sijui calculata waliweka ya nini.
 
Back
Top Bottom