Mkoba wa Mama
JF-Expert Member
- May 5, 2021
- 280
- 173
Magufuli alibadili baadhi ya majina ya wagombea ubunge walioshinda kura za maoni na kuteua wengine ili kuweka mambo sawa ndani ya chama na kwenye majimbo husika.
Sababu ni kwamba baadhi ya majimbo wabunge walikuwa wameyageuza kama mali yao binafsi, au kulikuwa na mpasuko mkubwa miongoni mwa wana CCM (team).
Mfano mmoja ni jimbo la Busega, kati ya Kamani na Chegeni.
Lakini kitu anachokifanya Samia kwa baadhi ya wabunge, mfano alichokifanya kwa Gwajima na Mpina, ni fitina, kwa sababu tu wameenda tofauti na anavyofikiri yeye.
Kama na Magufuli angeamua kufanya kwa fitina kama anavyofanya Samia sasa, sidhani kama Nape na Makamba wangekuwa bungeni leo. Hata Hayati Dkt. Ndugulile sidhani kama angerudi bungeni mwaka 2020, na wengine wengi tu akiwemo Gwajima mwenyewe.
NB: Samia alienda ziara Kanda ya Ziwa kupima upepo unasomekaje kuelekea Oktoba.
Sababu ni kwamba baadhi ya majimbo wabunge walikuwa wameyageuza kama mali yao binafsi, au kulikuwa na mpasuko mkubwa miongoni mwa wana CCM (team).
Mfano mmoja ni jimbo la Busega, kati ya Kamani na Chegeni.
Lakini kitu anachokifanya Samia kwa baadhi ya wabunge, mfano alichokifanya kwa Gwajima na Mpina, ni fitina, kwa sababu tu wameenda tofauti na anavyofikiri yeye.
Kama na Magufuli angeamua kufanya kwa fitina kama anavyofanya Samia sasa, sidhani kama Nape na Makamba wangekuwa bungeni leo. Hata Hayati Dkt. Ndugulile sidhani kama angerudi bungeni mwaka 2020, na wengine wengi tu akiwemo Gwajima mwenyewe.
NB: Samia alienda ziara Kanda ya Ziwa kupima upepo unasomekaje kuelekea Oktoba.