Diplomatician
Member
- Aug 22, 2013
- 21
- 1
Bila shaka Suala kubwa na la Msingi nchini kwetu ni kuhusu Suala la Mchakato wa Katiba Mpya.
Sisi sote ni Mashahidi kua Vyama vya Upinzani Pamoja na Wadau wengine Wenye Mapenzi Mema Na nchi Yetu wamekua Mstari wa Mbele Kutetea Mchakato wa Katiba Mpya kua Mchakato Shirikishi kwa Wananchi Wenyewe na Si Kuhodhiwa Na Chama Tawala kama Ilivyodhihirishwa Wakati wa Mjadala Wa Mswada wa Sheria inayoelekeza Jinsi gani Bunge la Katiba lipatikane na Namna nzima Ya Majadiliano Hayo.
Cha kushangaza Mwenyekiti wa TLP Mh. Augustine Mrema alibaki Peke yake Bungeni kama Mbunge wa Chama cha Upinzani akishirikiana na wabunge wa Chama Tawala kupitisha Ule Mswada wakati wa Mjadala amabapo Wabunge wenzake wa Vyama vingine vya Upinzani walitoka Nje kususia Mjadala wa Mswada wenye utata.
Kama hiyo haitoshi Siku ya Juzi,21 Sept Pale Jangwani wakati Vyama vya Siasa Vya Upinzani Na Wadau Wengine Wakitoa yao ya Moyoni Kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya Sikusikia Mwakilishi hata Mmoja akitajwa Kukiwakilisha Chama Cha TLP Hali kadhalika Kwa Upande Wa UDP hali ni ile ile,Nakumbuka kua Kama sikosei wakati wa Mjadala wa Ule mswada katika Bunge lililopita Mh. John Momose Cheyo Mb. Pekee na Mwenyekiti kutoka UDP Hakuwepo Bungeni(Kama nimekosea naomba Kusahihishwa)Lakini kutokuwepo kwake hakuzuii Chama chake kutoungana na Vyama Vingine vya Upinzani kutetea Mchakato wa Katiba Uwe Shirikishi kama Wadau wengine wenye Mapenzi Mema Wanavyotetea.
Je,Ukimya wao huo,wanatuaminisha kua Sasa UDP na TLP Si vyama vya Upinzani?
Sisi sote ni Mashahidi kua Vyama vya Upinzani Pamoja na Wadau wengine Wenye Mapenzi Mema Na nchi Yetu wamekua Mstari wa Mbele Kutetea Mchakato wa Katiba Mpya kua Mchakato Shirikishi kwa Wananchi Wenyewe na Si Kuhodhiwa Na Chama Tawala kama Ilivyodhihirishwa Wakati wa Mjadala Wa Mswada wa Sheria inayoelekeza Jinsi gani Bunge la Katiba lipatikane na Namna nzima Ya Majadiliano Hayo.
Cha kushangaza Mwenyekiti wa TLP Mh. Augustine Mrema alibaki Peke yake Bungeni kama Mbunge wa Chama cha Upinzani akishirikiana na wabunge wa Chama Tawala kupitisha Ule Mswada wakati wa Mjadala amabapo Wabunge wenzake wa Vyama vingine vya Upinzani walitoka Nje kususia Mjadala wa Mswada wenye utata.
Kama hiyo haitoshi Siku ya Juzi,21 Sept Pale Jangwani wakati Vyama vya Siasa Vya Upinzani Na Wadau Wengine Wakitoa yao ya Moyoni Kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya Sikusikia Mwakilishi hata Mmoja akitajwa Kukiwakilisha Chama Cha TLP Hali kadhalika Kwa Upande Wa UDP hali ni ile ile,Nakumbuka kua Kama sikosei wakati wa Mjadala wa Ule mswada katika Bunge lililopita Mh. John Momose Cheyo Mb. Pekee na Mwenyekiti kutoka UDP Hakuwepo Bungeni(Kama nimekosea naomba Kusahihishwa)Lakini kutokuwepo kwake hakuzuii Chama chake kutoungana na Vyama Vingine vya Upinzani kutetea Mchakato wa Katiba Uwe Shirikishi kama Wadau wengine wenye Mapenzi Mema Wanavyotetea.
Je,Ukimya wao huo,wanatuaminisha kua Sasa UDP na TLP Si vyama vya Upinzani?