MNAFU
Member
- Jan 16, 2014
- 99
- 24
Ninaandika kwa masikitiko kwani naona kama Kampuni hii ya Tigo haitajirekebisha katika kutatua Matatizo ya kimitandao yanapojitokeza basi Sisi wateja tunaweza kuiogopa Kampuni hii kutumia Huduma zake.
Tarehe 09/06/2015 majira ya saa 4 asubuhi nilihamisha kiasi cha shs. 2,500,000/= toka akaunti yangu ya Tigopesa kwenda benki ya NMB. Fedha ilitoka katika akaunti yangu ya tigopesa na nikapata message. Kwa Bahati mbaya haikwenda ktk akaunti ya NMB na haijaingia hadi Leo, siku ya 3.
Lengo ilikuwa kuweka fedha hiyo benki kuniwezesha kufanya biashara fulani muhimu. Niliisubiria hiyo fedha siku hiyo lakini wapi hadi biashara niliyotaka kufanya ikafa. Kiukweli Tigo wamenipa hasara kubwa!
Hiyo ni tisa, kumi umekuwa ni fedha hiyo kurudishwa Kwenye akaunti yangu ya tigopesa au basi iwekwe Kwenye akaunti! Pesa imepotea! Na haijulikani imepotea wapi??? AIBU SANA.
Siku Ile ya tukio niliwapigia customer care Mara kadhaa ambapo kwanza walisema ni kweli wameona tatizo na litafanyiwa kazi ndani ya saa 24. Nikasubiri muda huo ukaisha, Jana nikapiga Simu tena nikapewa Ahadi nyingi, siku ukaisha. Leo tena Nimepiga Simu nikapewa stori hiyo hiyo. Leo ni siku ya 3.
Najua Watu wa tigo mpo humu. Na kwa nini Hata hamna special thread humu? Wenzenu Vodacom wanayo. Na Pia wana special group email ambayo ukiandika wanafanyia kazi. Mbona nyinyi hamna?
Wakuu naomba ushauri Wenu nifanyeje kuipata Pesa yangu?
Wapi napoweza peleka lalamiko langu likashughulikiwa haraka?
Tarehe 09/06/2015 majira ya saa 4 asubuhi nilihamisha kiasi cha shs. 2,500,000/= toka akaunti yangu ya Tigopesa kwenda benki ya NMB. Fedha ilitoka katika akaunti yangu ya tigopesa na nikapata message. Kwa Bahati mbaya haikwenda ktk akaunti ya NMB na haijaingia hadi Leo, siku ya 3.
Lengo ilikuwa kuweka fedha hiyo benki kuniwezesha kufanya biashara fulani muhimu. Niliisubiria hiyo fedha siku hiyo lakini wapi hadi biashara niliyotaka kufanya ikafa. Kiukweli Tigo wamenipa hasara kubwa!
Hiyo ni tisa, kumi umekuwa ni fedha hiyo kurudishwa Kwenye akaunti yangu ya tigopesa au basi iwekwe Kwenye akaunti! Pesa imepotea! Na haijulikani imepotea wapi??? AIBU SANA.
Siku Ile ya tukio niliwapigia customer care Mara kadhaa ambapo kwanza walisema ni kweli wameona tatizo na litafanyiwa kazi ndani ya saa 24. Nikasubiri muda huo ukaisha, Jana nikapiga Simu tena nikapewa Ahadi nyingi, siku ukaisha. Leo tena Nimepiga Simu nikapewa stori hiyo hiyo. Leo ni siku ya 3.
Najua Watu wa tigo mpo humu. Na kwa nini Hata hamna special thread humu? Wenzenu Vodacom wanayo. Na Pia wana special group email ambayo ukiandika wanafanyia kazi. Mbona nyinyi hamna?
Wakuu naomba ushauri Wenu nifanyeje kuipata Pesa yangu?
Wapi napoweza peleka lalamiko langu likashughulikiwa haraka?