JAYJAY
JF-Expert Member
- Oct 31, 2008
- 7,291
- 7,235
Leo mchana nilikuwa sina salio kabisa kwenye simu ,nikamuomba jamaa yangu akanitumia 250, muda mfupi nikapokea sms kutoka namba 15556 ya msimu wa dhahabu na clouds Fm huku nikitaarifiwa na hiyo sms kuwa nitaendelea kutumiwa meseji zaidi msimu wa fiesta. Nikakumbuka juzi j3 ninilipokea sms inayohusiana na suala hilohilo lakini sikuijibu, kwa kuwa mwaka 2007 walikula sana salio langu kwa mtindo huo hivyo tangu wakati huo sijawahi kujibu tena sms za aina hiyo. Ikanibidi niangalie salio nikakuta imebaki 100, yaani wamekula 150, nikashangaa sana kwa sababu sijajiunga na huduma hiyo vipi wale salio langu. Kupiga customer care naambiwa kuongea na mhusika nitalipa sh. 50 kwa kila simu ikanibidi nipige maana nilikuwa na hasira sana, kupiga namba ambayo nilipewa simu inaita halafu inakuwa kama imepokelewa simu inahesabu muda lakini muhusika haongei, ikabidi nikate simu, kucheki salio imebaki 50. Jamaa mmoja akanishauri nitume neno "ondoa" kwenda ile namba iliyonitumia sms nikajibiwa na sms nyingine ya pushmobile kuwa nitaondolewa kwenye huduma hiyo baada ya masaa 24, yaani mpaka sasa naogopa kuweka salio kwa hofu kuwa jamaa wanaweza kunitumia sms nyingine na kuendelea kula salio langu. Hivi wandugu kuna namna naweza fanya hawa wezi warudishe salio langu? Na haiwezekani mamlaka husika kuzuia kutumiana matangazo ya aina hii au ndio vigezo na masharti yamezingatiwa mara tu unapojiunga na mtandao husika?