Captain-Chui
Member
- Dec 11, 2014
- 80
- 49
Tanzania ni nchi ya kula. Ukipewa nafasi unakula. Watazania wengi ni mafisadi kila mmoja kwa nafasi yake. Cha msingi wewe hakikisha tu kwamba hukamatwi. Ukikamatwa utaathibiwa, sio kwa sababu umeiba bali ni kwa sababu umefanya uzembe ukakamatwa. Professor Tibaijuka amefanya uzembe akakamatika. Kwa hiyo inabidi aadhibiwe atolewe kafara kuwafumba macho wananchi. Wenzake wajanja wlichukua pesa cash kwenye mifuko ya rambo na magunia na kufuta ushahidi. Yeye Prof Tibaijuka anajianika anafungua account kuweka ushahidi wazi. Inaonekana huyu prof ana akili tu za darasani, lakini akili za kifisadi ni sifuri.