Tiba ya harufu mbaya ya kinywa

Tiba ya harufu mbaya ya kinywa

Naomba msaada nimetumia dawa na hospitali zote kupata suluhu ya harufu mbaya ya kinywa. Naswaki vizuri ulimi, meno na kwa dawa mpaka za 50k.

Nimetumia karafuu, tangawizi na aina nyingine za madawa ya dukani na asili ila changamoto ipo pale pale nikiongea na mtu anakimbilia kushika pua na kugeuza uso

Naomba msaada wadau. Changamoto inanikosesha raha.
Shida iko tumboni kwako,we unatibu mdomoni
 
Jaribu HOME MADE MEDICINE hii itakusaidia katakata vitunguu maji vikubwa vitatu, vikate vidogo kisha viweke kwenye jar lenye mfuniko lenye ujazo wa nusu Lita kisa weka asali kujaza jar hilo. Tumia vijiko vitatu vya chakula kutwa mara tatu itakusaidia.
 
Nenda kwa dentist. Tatizo mnapenda kujifanyia diagnosis wenyewe.
 
Naomba msaada nimetumia dawa na hospitali zote kupata suluhu ya harufu mbaya ya kinywa. Naswaki vizuri ulimi, meno na kwa dawa mpaka za 50k.

Nimetumia karafuu, tangawizi na aina nyingine za madawa ya dukani na asili ila changamoto ipo pale pale nikiongea na mtu anakimbilia kushika pua na kugeuza uso

Naomba msaada wadau. Changamoto inanikosesha raha.
Bacteria, au kuna stones zipo kwenye Kuta za koromeo mwanzoni zinatoaga harufu Kali ya ajabu kama usipozitoa then kitu kingine ni fizi kutoa dam ile dam ikibak mdomon ikikaa muda flan inaanza kutoa harufu mbaya
 
Back
Top Bottom