DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Tottenham Hotspur imemtangaza kocha Thomas Frank kuwa meneja wake mkuu kuchukua mikoba ya Age Postecoglou aliyetimuliwa hivi karibuni baada ya kuiongoza timu hiyo kutwaa taji la Europa League.
Frank ambaye alikuwa anainoa Brentford, anajiunga na Spurs kwa mkataba wa miaka mitatu baada ya kukubali ofa aliyowekewa mezani.
“Kwa Thomas tumemteua miongoni mwa makocha wakuu wabunifu na wanaopiga sana hatua kwenye mechi.
“Ana rekodi isiyoacha shaka katika kuendeleza mchezaji na kikosi na tunatazamia aiongoze timu wakati tunajiandaa na msimu ulio mbele,” amesema msemaji wa Spurs.
Mkurugenzi wa soka wa Brentford, Phil Giles ametoa shukrani kwa Frank kwa mchango alioipa klabu hiyo ambayo aliipandisha daraja 2021.
source:Mwanaspoti
Frank ambaye alikuwa anainoa Brentford, anajiunga na Spurs kwa mkataba wa miaka mitatu baada ya kukubali ofa aliyowekewa mezani.
“Kwa Thomas tumemteua miongoni mwa makocha wakuu wabunifu na wanaopiga sana hatua kwenye mechi.
“Ana rekodi isiyoacha shaka katika kuendeleza mchezaji na kikosi na tunatazamia aiongoze timu wakati tunajiandaa na msimu ulio mbele,” amesema msemaji wa Spurs.
Mkurugenzi wa soka wa Brentford, Phil Giles ametoa shukrani kwa Frank kwa mchango alioipa klabu hiyo ambayo aliipandisha daraja 2021.
source:Mwanaspoti