Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,335
- 24,230
Asante mkuu kwa kuonyesha ukweli.Wanabodi,
Karibuni katika mada hii ya "thinking aloud" ambayo ni moja ya mada zangu za abstracts ya hypothetical situations, kumaanisha ni mada ya kufikirika tuu lakini inafikirisha, na sio lazima hiki kitu kiwe ni kweli, au ni sisi jf, lakini likitokea jambo lilasemwa humu, likajadiliwa, kisha vyombo vya maamuzi vilatoa maagizo au kufikia maamuzi kuhusu jambo hilo kwa jinsi ile ile lilivyojadiliwa humu jf, kama zilivyo baadhi ya zile mada zangu za "the voices from within", ambazo nyingine ni kweli hutokea na nyingine hazitokei, zinapotokea, hata kama the cause sio sisi, lakini kama tumepigia kelele jambo fulani, tukashauri na kisha hatua zikachukuliwa, tuna haki kabisa ya kujipongeza kuwa tulichangia.
Thinking Aloud ni Nini?
Thinking Aloud ni Kufikiri kwa sauti, kwa kawaida kufikiri kunafanyika kwenye part of brain, ubongo, responsible for thinking ambapo tangu binadamu anazaliwa, ile tuu kuvuta hewa ya kwanza baada tuu ya kutoka tumboni kwa mama, huo ndio mwanzo wa binadamu kujitegemea, kabla ya hapo, kiumbe huyo akiwa tumboni, kila kitu alimtegemea mama aliyembeba miezi 9.
Kwa vile mimi ni mtu wa ma story, kwa wale walio busy, ama wasio na time na ma story, to cut the long story short, mnaweza kuishia hapa na kujump kule mwisho. Wale wa mastory mnaweza kuendelea hapa
Mada hii nimefikia, by thinking aloud kuhusu the role of JF kwenye maendeleo ya taifa letu, na kujikuta ninatoa hongera kwa JF na wana jf kwa mawazo chanya ambayo yanalisaidia sana taifa, letu la Tanzania, kwasababu kuna mtu, au kuna watu, "Atakuwa Anaingia JF in Person na Kutusoma !", na kisha to make sense of mawazo ya wana jf humu, na kisha kuyafanyia kazi, kwa kuchukua hatua stahiki, hivyo kwa kulijua hili, natoa wito kwa mwaka 2021, sisi wana jf, lets be more responsible, kwa kuwa more focused kwenye baadhi ya mada au hoja zinazo husu maslahi ya taifa, tuwe more focused, more strategically na more critical, using critical thinking, tunamsaidia sana huyu jamaa na kulisaidia sana taifa, ingawa huwa hasemi au hawasemi, lakini wanasoma na kuyafanyia kazi baada ya maoni yetu humu na hoja zetu humu, hivyo baadhi ya vitu tunavyo vipigia kelele humu, for nothing, ni kelele for something, na kiukweli jf itabarikiwa sana na sisi wana jf pia tutabarikiwa!, big up kubwa sana kwa Mkuu Max na team yake, big up sisi wana jf wote in our totality.
Japo kuna mitandao mingi ya kijamii ambayo inaibua hoja mbalimbali kila dakika kama Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, LinkedIn etc, hakuna mtandao ambao unafanya mijadala na uchambuzi wa issues kama jf, hivyo kitu kikiibuka Twitter au YouTube, kina pata more weight na momentum kama kitajadiliwa humu jf na matokeo chanya ni kuona mawazo ya wana jf yanavyofanyiwa kazi, hivyo jf kujikuta tunatimiza wajibu wetu kwa ama kulisaidia kulijenga taifa kwa kutoa mawazo constructive kulisaidia taifa, au kuliponya taifa kwa kuangazia madudu yanayofanyika as whistleblowers, na hata kwenye ukosoaji wa viongozi wetu na serikali yetu unaofanywa kwa constructive criticism, unalisaidia taifa. Big Up sana wana jf for this.
Kufuatia kinywaji ninachokata, Joni Mtembezi, ni kikali ila stimu zake ni short lived, ukipiga, huchelewi kuzimika, ila pia stimu hazichelewi keisha, hivyo zikiisha lazima utaamka, utasikia kiu due to nausea, unapata maji, na ndipo unaendelea kulala the normal sleep. Wakati ukiwa kwenye usingizi wa Joni Mtembezi, Cognitive brain inakuwa at complete rest, relaxed na hakuna hata kuota.
Hivyo nilipoamka usingizi umekata, nikajikuta nashika simu janja yangu na kuperlus mitandaoni, nikaanzia Twitter kuzisoma za moto zilizopakuliwa kutoka jikoni, nikaenda YouTube, nikaenda Facebook, nikaenda LinkedIn na kutembelea several blogs na mwisho nikashuka jf.
Nilipoanza kuifikiri hii mitandao nikajikuta hakuna mtandao unakata issues za kitaifa kama jf, na nikiangalia impact ya baadhi ya hoja za nguvu za humu jf zenye nguvu za hoja, nikajikuta nashawishika kuwa hata naniliu mwenyewe in person, atakuwa anaingia humu jf na kutusoma, na kufuatia hoja za humu, zinamuingia na anachukua hatua.
Naomba nisiende kwenye hoja specific na hatua specific zilizochukuliwa kufuatia hoja za jf, maadam hata wenyewe hawasemi, naomba na mimi nisiseme ila sisi baadhi yenu tuliojaliwa jicho la tatu na the sixth sense, tunaona, naomba itoshe kusema kuwa jf we are just doing a very good job, for this country na wahusika wanajua, wanaona, wanasikia na wanazifanyia kazi hoja za jf ikiwemo kuchukua hatua stahiki.
Big up sana kwa jf wote, hata wale watema pumba, maana hata hizo pumba ni chakula cha kuku, anayakula kuku mtamu, huo utamu wa nyama ya kuku unatokana na pumba alizokula!.
Big up sana kwa jf wote, jf is power to reckon with!.
Paskali
Ni vizuri viongozi kupata mambo yanayotokea mitaani au hata kwenye taasisi, mapema kabla habari hazijavalishwa nguo na watendaji wahusika.
Kuzivalisha nguo habari, badala ya kuzifikisha zikiwa uchi au raw kama wanavyosema waswahili wa London, kunasaidia kufichua uhalisia wa habari zenyewe.
Hapa nampongeza sana Maxence Mello na jopo lake la JF maana wanatenda haki kwa umma wa kiTanzania.
Member humu akisema kuna mapungufu mahali, hiyo habari ikaonwa na kiongozi, na hatua stahiki kuchukuliwa, mbona sasa si ndiyo kuisaidia serikali moja kwa moja?
Kwa wenzetu habari ni mhimili wa nne.