Then who is coming next?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
73,832
151,900
Ilianza Mv. Mbeya, tukaziba masikio. Ikaja Mv. Bukoba tukafumba macho. Sasa limetukuta la Spice Islander. Tunatafuta mchawi, tumeacha kuziba ufa ili majanga yasitokee tena. Kuna baadhi ya watu wametiwa ndani kwa kuzembea hadi ajali ikatokea Nungwi. Tunafurahia sana, lakini tumesahau kuwa kuwafunga na kuwatia ndani hakutokomesha ajali za majini.
Najiuliza, hili sakata likipoa tutarajie nani atazama? Je ni Mv. Victoria au Mv. Lihemba yenye zaidi ya miaka mia majini?
Je tumejiandaa vipi kuhakikisha kuwa roho na nafsi zisizo na hatia zitasalimika?
Wito wangu: mamlaka zibadilishje namna yao ya uendeshaji wa shughuli za majini.
Watendaji wamebobea kwa rushwa ndogo za chips kuku bia bia.
Hii ni aibu inayoangamiza taifa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom