TFF ya Malinzi Imepoteza Uhalali wa Kutawala Muhula wa Pili

Baba Kiki

JF-Expert Member
May 31, 2012
1,544
943
1.Hii ni TFF pekee iliyotukumbusha kuwa bado
kuna viini vya ukabila nchi hii ambapo viongozi wakuu wa chombo hiki pamoja na asilimia kubwa ya wadau wengine ni wahaya.
Sitaki kuamini kuwa hii ni bahati mbaya na kimsingi ni kinyume cha misingi ya utawala bora hata kama wateuliwa wana vigezo

2. Hii ndio TFF pekee inayofanya maamuzi kwa kupiga ramli na ubashiri au kura wakati kanuni ziko wazi! Kesi za kuamuliwa kwa siku moja kama kanuni inazingatiwa, inaweza kuchukua majuma au miezi ilimradi ipindishwe au kuangalia upepo unavumaje. Rejea kesi za Geita na Polisi Tabora, Simba vs Kagera, Simba vs Azam kuhusu mkataba wa Singano,n.k. Kielelezo cha ubabaishaji TFF leo inaweza kuamua hivi, kesho ikaamua tofauti ktk jambo hilohilo! So huwezi kujua kosa ni lipi na haki ni ipi

3. Hii ndio TFF ambayo vyombo vyote vinaweza kukaa kwa pamoja kuamua jambo moja! Huelewi hasa ni chombo gani linachofanya maamuzi. Ktk sakata la Simba na pointi 3 za Kagera kikao cha rufaa kimehusisha Bodi ya Ligi, Kamati ya Masaa 72, Sekretarieti na Kamati ya nidhamu! Ajabu kabisa

4. Hii ndio TFF ambayo viongozi wake hasa Malinzi ameamua kufungia kila mtu anayempinga. TFF haina uvumilivu kwa wakosoaji wake. Iko tayari kutumia kinachoitwa kanuni pale tu zinapoainisha hukumu kwa wanaokosoa tu. Angetile alitumbuliwa siku moja baada ya Malinzi kuingia madarakani, Ndumbaro kafungiwa miaka 7, Muro, Manara na naamini wengi watafuata kama kuna atayempinga Malinzi. Hebu jiulize kwani watu zamani kipindi cha Ndolanga na Tenga walikuwa hawakosei? Kwa nini ni kipindi hiki tu ndio kila ukosoaji unaambatana na kufungiwa?

4. Ndio TFF iliyokumbwa na tuhuma kubwa kabisa za rushwa na upangaji matokeo ambapo viongozi wakuu wamehusishwa moja kwa moja na rushwa kiasi cha kuchunguzwa na TAKUKURU na baadhi kupandishwa mahakamani hata kama mtu anaweza kushinda kesi lkn wahenga walisema panapofuka moshi......

5. Ndio TFF ambayo kamati zake ni mbovu kiasi kuwa kamati inaweza kuendesha kikao bila kujali akidi au kushirikisha wajumbe ambao hawaruhusiwi! Hii ni kwa mujibu wa Katibu Mkuu Mwesiga alipoelezea 'uhuni' uliofanywa na Kamati ya Masaa 72 iliyoamua kuipa pointi 3 Simba kama ni kweli.Hii si habari nzuri kwa utawala wa soka.

Kwa sababu hizi na nyingine nyingi Malinzi asipewe kura kutawala muhula ujao, aliyofanya kwa miaka 4 inatosha na kubwa atakumbukwa kwa kufanya vizuri kuiandaa Serengeti Boys lakini hana cha kujivunia katika utawala na usimamizi wa soka. Wajumbe bila kujali itikadi za Usimba na Uyanga, au maslahi binafsi hasa wale wajumbe walioandaliwa kumpigia kura chondechonde utendeeni haki mpira wa nchi hii. Piga chini!!!
 
Pamoja na Serengeti boys,kingine ni kwamba amekuwa akiandaa marefa wengi vijana kwa ajili ya kutumika katika vizazi vijavyo.
Masomo ya refereeing ameyapa sana kipaumbele.
Hata Yule dogo alichezesha kwa umakini mechi ya Serengeti boys na Ghana pale Taifa.

Upendeleo wa ukanda au kabila,siyo ishu,ishu ni utendaji.
Hilo huwa lipo kila Mahali.
Hata mwanajeshi akichaguliwa nafasi kubwa,ataangalia wanajeshi wenzake wenye uwezo wa hayo majukumu.. Kati ya wengi wengine wenye uwezo,na labda hawafahamu ama hata kama anawafahamu ,basi kuchelea kupishana kimtazamo au kutoendana na kasi yake
 
Nilishangaa sana kujua kuwa hakutaka kuachia uenyekiti wa mkoa baada ya kupata urais was TFF! Hana washauri?
 
Wewe ulitakaje....ukiwa unafungwa upewe wewe point tatu... Mbumbumbu kabisa
 
Pamoja na Serengeti boys,kingine ni kwamba amekuwa akiandaa marefa wengi vijana kwa ajili ya kutumika katika vizazi vijavyo.
Masomo ya refereeing ameyapa sana kipaumbele.
Hata Yule dogo alichezesha kwa umakini mechi ya Serengeti boys na Ghana pale Taifa.

Upendeleo wa ukanda au kabila,siyo ishu,ishu ni utendaji.
Hilo huwa lipo kila Mahali.
Hata mwanajeshi akichaguliwa nafasi kubwa,ataangalia wanajeshi wenzake wenye uwezo wa hayo majukumu.. Kati ya wengi wengine wenye uwezo,na labda hawafahamu ama hata kama anawafahamu ,basi kuchelea kupishana kimtazamo au kutoendana na kasi yake

Naungana na wewe kwenye masomo ya urefarii na mwamuzi unayemzungumzia yule dogo namkubali sana.
Lakini utakubaliana na mimi kuwa kwa ujumla kiwango cha uamuzi kwenye mechi nyingi chini ya Malinzi imekuwa pasua kichwa sana.

Napingana na wewe kwenye suala la upendeleo wa ukanda, au ukabila na kusema eti issue ni utendaji.
Utendaji ni kitu subjective wakati mwingine na kwa mfano ukiwa na mkeo ofisini utendaji wake unaweza usiupime vizuri hasa kama mna maelewano mazuri. Lakini pia kitendo cha kufikiRia watu wa kabila lako kwanza ni dalili mbaya hasa upendeleo.

Viongozi wetu wakuu wa nchi wakati mwingine waliacha kuchagua watu wa makabila yao sio kuwa hawakuwa competent lakini kujaribu kuwa fair.
 
Nilishangaa sana kujua kuwa hakutaka kuachia uenyekiti wa mkoa baada ya kupata urais was TFF! Hana washauri?


Washauri wanaomzunguka wengi ni wahaya, kwa hiyo wana same taste ktk uongozi, ndio maana wao wanaona sawa tu.
 
Pole najua ni povu la points za kagera,mpira uwanjani na sio mezani


Ungefanya vzr zaidi kama ungeshughulisha ubongo wako kujadili hoja zangu badala ya kuendeleza ramli za akina malinzi.
Suala hapa ni kanuni = mchakato = matokeo.

Povu la mashabiki litaendelea na liko kila sehemu duniani lakni mifumo ya haki inawafanya watu waamini kuwa haki inaweza kutendeka.
 
TFF inahitakiwa ibadilike maana baadhi ya maamuzi yao yanaua soka la Tanzania kwa kweli.
 
Mezani Fc a.k.a Mbeleko Fc acheni kumwaga mapovu,mpira unachezwa uwanjani sio kwenye meza na mdomoni. Naiomba T.O.C wawape nafasi ili Mwakani mtuwakilishe kimataifa kwenye michezo ya Olimpic kupitia mpira wa meza,nadhani hapo kiu yenu ya kushiriki michuano ya Kimataifa itakata.
 
1.Hii ni TFF pekee iliyotukumbusha kuwa bado
kuna viini vya ukabila nchi hii ambapo viongozi wakuu wa chombo hiki pamoja na asilimia kubwa ya wadau wengine ni wahaya.
Sitaki kuamini kuwa hii ni bahati mbaya na kimsingi ni kinyume cha misingi ya utawala bora hata kama wateuliwa wana vigezo

2. Hii ndio TFF pekee inayofanya maamuzi kwa kupiga ramli na ubashiri au kura wakati kanuni ziko wazi! Kesi za kuamuliwa kwa siku moja kama kanuni inazingatiwa, inaweza kuchukua majuma au miezi ilimradi ipindishwe au kuangalia upepo unavumaje. Rejea kesi za Geita na Polisi Tabora, Simba vs Kagera, Simba vs Azam kuhusu mkataba wa Singano,n.k. Kielelezo cha ubabaishaji TFF leo inaweza kuamua hivi, kesho ikaamua tofauti ktk jambo hilohilo! So huwezi kujua kosa ni lipi na haki ni ipi

3. Hii ndio TFF ambayo vyombo vyote vinaweza kukaa kwa pamoja kuamua jambo moja! Huelewi hasa ni chombo gani linachofanya maamuzi. Ktk sakata la Simba na pointi 3 za Kagera kikao cha rufaa kimehusisha Bodi ya Ligi, Kamati ya Masaa 72, Sekretarieti na Kamati ya nidhamu! Ajabu kabisa

4. Hii ndio TFF ambayo viongozi wake hasa Malinzi ameamua kufungia kila mtu anayempinga. TFF haina uvumilivu kwa wakosoaji wake. Iko tayari kutumia kinachoitwa kanuni pale tu zinapoainisha hukumu kwa wanaokosoa tu. Angetile alitumbuliwa siku moja baada ya Malinzi kuingia madarakani, Ndumbaro kafungiwa miaka 7, Muro, Manara na naamini wengi watafuata kama kuna atayempinga Malinzi. Hebu jiulize kwani watu zamani kipindi cha Ndolanga na Tenga walikuwa hawakosei? Kwa nini ni kipindi hiki tu ndio kila ukosoaji unaambatana na kufungiwa?

4. Ndio TFF iliyokumbwa na tuhuma kubwa kabisa za rushwa na upangaji matokeo ambapo viongozi wakuu wamehusishwa moja kwa moja na rushwa kiasi cha kuchunguzwa na TAKUKURU na baadhi kupandishwa mahakamani hata kama mtu anaweza kushinda kesi lkn wahenga walisema panapofuka moshi......

5. Ndio TFF ambayo kamati zake ni mbovu kiasi kuwa kamati inaweza kuendesha kikao bila kujali akidi au kushirikisha wajumbe ambao hawaruhusiwi! Hii ni kwa mujibu wa Katibu Mkuu Mwesiga alipoelezea 'uhuni' uliofanywa na Kamati ya Masaa 72 iliyoamua kuipa pointi 3 Simba kama ni kweli.Hii si habari nzuri kwa utawala wa soka.

Kwa sababu hizi na nyingine nyingi Malinzi asipewe kura kutawala muhula ujao, aliyofanya kwa miaka 4 inatosha na kubwa atakumbukwa kwa kufanya vizuri kuiandaa Serengeti Boys lakini hana cha kujivunia katika utawala na usimamizi wa soka. Wajumbe bila kujali itikadi za Usimba na Uyanga, au maslahi binafsi hasa wale wajumbe walioandaliwa kumpigia kura chondechonde utendeeni haki mpira wa nchi hii. Piga chini!!!
Pointless....ningekuona wa maana. Kama ungesema tuwashushe daraja la Tatu simba na yanga...Hawa ndo waharibifu wa soka letu tanzania...as long as simba na yanga kubak kwenye lig tanzania soka halitaendelea

Sent from my E2303 using JamiiForums mobile app
 
Pointless....ningekuona wa maana. Kama ungesema tuwashushe daraja la Tatu simba na yanga...Hawa ndo waharibifu wa soka letu tanzania...as long as simba na yanga kubak kwenye lig tanzania soka halitaendelea

Sent from my E2303 using JamiiForums mobile app


Kwa nini uwashushe Simba na Yanga? Kwa kosa lipi na kanuni ipi? Ulianza kusema pointless nikajua unashusha nondo kumbe unaendeleza ramli.
 
Ungefanya vzr zaidi kama ungeshughulisha ubongo wako kujadili hoja zangu badala ya kuendeleza ramli za akina malinzi.
Suala hapa ni kanuni = mchakato = matokeo.

Povu la mashabiki litaendelea na liko kila sehemu duniani lakni mifumo ya haki inawafanya watu waamini kuwa haki inaweza kutendeka.
Kwenye Kanuni hapo hapo hivi Simba walikata rufaa ndani ya wakati!!?? Kwa nini ilisikilizwa!!?? Swali la pili Hivi Simba walilipia Ada ya rufaa!!?? Mbona ilisikilizwa.... Basi Simba nao ni wahaya
 
Tatizo ukiwa shabiki wa yanga akili huwa iko pembeni kabisa.Jamaa anakosoa TFF,mtu anakuja na hoja ya point za mezani. Hoja hupingwa kwa hoja.Hivi hii TFF iliyoshusha kiwango cha timu ya taifa unawezaje kuitetea. Yaani kuwa na ligi kubwa kama hii na kutoa wawakilishi hafifi wanao tolewa kwa vipigo vya mbwa mwizi ni TFF ya kutetewa.Naona hapa kunashida kwenye ufahamu.Point za mezani hazifai lakini kama kanuni inatoa point hizo, si swala la simba pekee maana hata timu zingine ziliipoka simba point mezani.Tujaribu kujibu hoja na si vioja.
 
Back
Top Bottom