Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limejikuta katikati ya lawama nzito baada ya kashfa ya uchaguzi wa wachezaji wa kuwakilisha taifa katika mashindano ya eFootball World Cup 25.
Yaani badala ya kuchagua mabingwa wa kweli wanaopatikana mitaani—wale wanaojulikana kwa uwezo wa ajabu kwenye PlayStation na hutembea na game pad zao—uongozi umeamua kubeba watu kwa kujuana, mnaweka watu wanaokwenda kuuza sura tu.
Ni jambo la kusikitisha kuona kuwa wachezaji walioteuliwa walishindwa kuonesha ubabe wowote katika hatua ya kufuzu, wakifanikiwa kushinda michezo mitatu pekee kati ya mechi saba, huku tukipokea vichapo vizito kutoka kwa Libya na Morocco.
Wakati huo huo, mashabiki na wadau wa michezo ya PlayStation wanashangaa ni vipi vijana wenye vipaji vikubwa kutoka maeneo kama Magomeni, Tabata, Ilala Dar es Salaam, Ngarenaro Arusha, au Dampo na Rufiji Mwanza, hawakupatiwa nafasi ya kupita ili waiwakilishe Tanzania?
Mitaani, mabingwa hawa wa eFootball huchukua timu ndogo kama Wolverhampton ama Sunderland na bado wanaweza kuwapiga mabingwa wanaotumia *Real Madrid au PSG kwa mabao mengi. Ni kiwango cha juu cha ubunifu, mbinu, na akili ya kiufundi ambacho kingeweza kuipa Tanzania heshima kubwa kimataifa.
Kwa nini TFF imeshindwa kuona dhahabu hizi mitaani? Sasa ni wakati wa kuachana na hizi mambo za kujuana na kuanza kuthamini vipaji halisi vilivyo mitaani ili taifa lisijikute tena likidhalilika. Nendeni mitaani mkakutane na Master PS wamejaa sio hawa wauza sura kwenye TV.
Yaani badala ya kuchagua mabingwa wa kweli wanaopatikana mitaani—wale wanaojulikana kwa uwezo wa ajabu kwenye PlayStation na hutembea na game pad zao—uongozi umeamua kubeba watu kwa kujuana, mnaweka watu wanaokwenda kuuza sura tu.
Wakati huo huo, mashabiki na wadau wa michezo ya PlayStation wanashangaa ni vipi vijana wenye vipaji vikubwa kutoka maeneo kama Magomeni, Tabata, Ilala Dar es Salaam, Ngarenaro Arusha, au Dampo na Rufiji Mwanza, hawakupatiwa nafasi ya kupita ili waiwakilishe Tanzania?
Mitaani, mabingwa hawa wa eFootball huchukua timu ndogo kama Wolverhampton ama Sunderland na bado wanaweza kuwapiga mabingwa wanaotumia *Real Madrid au PSG kwa mabao mengi. Ni kiwango cha juu cha ubunifu, mbinu, na akili ya kiufundi ambacho kingeweza kuipa Tanzania heshima kubwa kimataifa.
Kwa nini TFF imeshindwa kuona dhahabu hizi mitaani? Sasa ni wakati wa kuachana na hizi mambo za kujuana na kuanza kuthamini vipaji halisi vilivyo mitaani ili taifa lisijikute tena likidhalilika. Nendeni mitaani mkakutane na Master PS wamejaa sio hawa wauza sura kwenye TV.