Tenga anaua soka la Tanzania

Tenga anaua soka la Tanzania

BITTY NGUZO

Member
Joined
May 26, 2009
Posts
32
Reaction score
4
Asalaa alkhum wanajamvini,
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia utendaji kazi wa Rais wa TFF Ledger Chilla Tenga nimegundua kuwa hanajipya katika kuleta mabadiliko ya soka la Tanzania na hata kuiongoza TFF.Najiuliza kwanini yeye anang'ang'ania kuendesha ligi wakati timu zinataka ligi iendeshwa na kampuni?Mpaka hapo ninashaka kuwa TFF wamekuwa wanafaidika na ligi hiyo ndio maana wanakataa isiendeshwe na kampuni sababu watakosa mshiko.Kwa mtindo huu namshauri ili kulinda heshima yake na kuepusha migogoro ya soka la Tanzania ni bora asigombee tena nafasi hiyo katika uchaguzi ujao kwa sababu ameudhihirishia umma kuwa hawezi kuongoza soka.
 
Kaka nakuunga mkono jana wametangaza wakikifuta kichuo cha kukuza kipacha cha pale TFF anafanya nn,yupo kukusanya mapato na pesa zinazotolewa na wafadhili timu ya taifa inapokuwa kambini,kama chama cha soka kinashindwa kuendeleza soka la vijana kinafanya nn,kinasubili nn,na kipo kwa ajili gani,kafeli kuendesha mpira aondoke
 
[h=2]Wednesday, November 14, 2012[/h][h=3]BARUA YA WAZI KUTOAK KWA WADAU WA SOKA KWENDA TENGA KWA UKIUKWAJI WA KATIBA YA TFF[/h]




Bwana Leodger Chilla Tenga
Rais wa TFF


Ndugu Tenga,


YAH: UKIUKWAJI WA KATIBA YA TFF


Sisi wadau wa mpira wa miguu Tanzania tunakuandikia barua hii tukiwa na uchungu mkubwa kuhusu mwenendo wa uongozi wako. Ulipoingia madarakani kwa mara ya kwanza Golden Tulip tarehe 27 Desemba 2004 ulitoa matumaini makubwa kuhusu kuleta mabadiliko makubwa katika uendeshaji wa
 
mpira wetu. Pamoja na mapungufu mengi yaliyojitokeza ndani ya miaka minane ya uongozi wako haya mawili tutakayoyaeleza hapa chini hayawezi kufumbiwa macho na wanaoutakia mema mpira wa Tanzania.

1. Kupitisha muda wa uongozi wako bila kibali cha mkutano mkuu.
Mkutano mkuu uliokuingiza madarakani ulifanyika siku ya Jumapili tarehe 14 Desemba 2008. Kifungu 33(1) cha Katiba ya TFF kinatamka kuwa kipindi cha uongozi ni miaka minne tu. Hivyo ukomo wa uongozi wako na kamati yako ya utendaji ni saa sita za usiku tarehe 13 Desemba 2012. Aidha kifungu cha 10(1) cha kanuni za uchaguzi wa TFF kinatamka kuwa tangazo la uchaguzi litatolewa siku 40 kabla ya uchaguzi. Kwa mantiki hii kamati yako ya uchaguzi ilitakiwa itangaze tarehe ya uchaguzi siku ya Jumatatu tarehe 05 Novemba 2012 au kabla ya hapo. Leo ni tarehe 13 Novemba 2012 na ofisi yako iko kimya! Hii haikubaliki, haiwezekani ujiongezee muda wa uongozi bila kibali cha Mkutano Mkuu. Tutawaomba wajumbe wa Mkutano Mkuu wakuadhibu kwa kosa hili la ukiukwaji wa Katiba. Pamoja na mapungufu haya ni vyema ukatufahamisha uchaguzi umepanga ufanyike lini au unasubiri wajumbe wa mkutano mkuu wakulazimishe kwa maandishi?


2. Kufuta nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais wa TFF
Yapo maneno yanasemwa eti uongozi wako unataka kufuta nafasi ya pili ya Makamu wa Rais wa TFF kinyemela. Kama tuhuma hizi ni za kweli tunaoma tukukumbushe yafuatayo:
2.1.1 Nafasi ya makamu wa pili wa Rais wa TFF iko ndani ya Katiba ya TFF kifungu 31(1)
2.1.2 Kifungu cha katiba 30(1) kinatamka wazi kuwa ni mkutano mkuu pekee wenye mamlaka ya kubadili Katiba ya TFF. Hivyo hakuna njia mbadala ya kubadili Katiba ya TFF.
2.1.3 Kifungu cha Katiba 30(2) kinatamka kuwa tangazo lolote la nia ya kubadili Katiba ya TFF litatolewa siku 45 kabla ya mkutano mkuu. Uongozi wako utawezaje kutoa tangazo hili ndani ya kipindi cha uongozi wako kilichobakia?
2.1.4 Kifungu cha Katiba 30(6) kinatamka kuwa ombi la kubadili katiba litapigiwa kura NDANI YA MKUTANO MKUU na ili lipite theluthi mbili ya wajumbe sharti iridhie. Zingatia utashi huu wa Katiba.


Bwana Tenga kama kweli wazo hili lipo basi achana nalo, usijidhalilishe kwa kukiuka Katiba iliyokuweka madarakani. Nafasi za uongozi katika uchaguzi ujao zitangazwe kwa mujibu wa Katiba iliyokuweka madarakani. Kama kuna umuhimu wa kubadili Katia hakuna uharaka wowote, subiri awamu ijayo ifanyie kazi wazo hilo, awamu ambayo huenda wewe mwenyewe ukaingoza pia kama ukigombea tena.


Tunasubiri majibu ya hoja zetu za majibu haya tunaomba uwajulishe watanzania wote.


Nakala ya barua hii tunawapelekea wajumbe wote wa Mkutano Mkuu kwa taarifa.


Ni sisi kwa niaba ya wadau wa mpira wa Tanzania.
 
kila mtu anaingia TFF kwa nia mbili kubwa.
Kwanza ni kula, pili ni daraja kwenda kwenye siasa.
Ili Tanzania tufanikiwe, ni lazima tuachane na mambo haya ya uroho wa madaraka, wizi na kutumia mpira kama daraja la kuingilia kwenye siasa.
 
kila mtu anaingia TFF kwa nia mbili kubwa.
Kwanza ni kula, pili ni daraja kwenda kwenye siasa.
Ili Tanzania tufanikiwe, ni lazima tuachane na mambo haya ya uroho wa madaraka, wizi na kutumia mpira kama daraja la kuingilia kwenye siasa.


mkuu una ndoto za awa watu kubadilika na kuacha uroho wa madaraka?
 
ndo uwezo wake wa kuongoza ulipoishia hapo, angekuwa ni mwenye kuelewa angeachia ngazi mwenyewe ili kuepuka aibu lakin kwa sababu amejaa tamaa na hajui ukubwa wa heshima kupotea KAMWE hataachia ngazi wala kujiudhuru
 
Naomba tutengeneze kitu hapa chenye kufanana na balance sheet,upande wa kushoto tujaze mambo mazuri aliyoweza kuyafanya na upande wa kulia tujaze mapungufu na madhaifu yake and then tuangalie upande upi nimzito zaidi na ndipo tupate conclusion.
 
mpira wa Tanzania umetawaliwa na mfumo wa kisiasa mno
 
Tenga ameshasema hatogombea tena na hawezi kubadili maamuzi yake. Vuteni subira kwani si mrefu ataachia ngazi kisha mrekebishe hayo mapungufu yake maana inaonekana kila anayetaka kurithi kiti chake anakuja na bla bla bla nyingi

Kwa wapenda michezo wote ni lazima tuwe macho na kina Michael Wambura ambao wanataka uongozi kwa gharama yoyote ile wakati system ilishawakataa kutokana na madudu waliyoyafanya huko nyuma. Ukija ukichunguza walio nyuma ya waraka huu utakuta ndo hao hao kina Wambura. Ni bora tuweke mifugo ituongoze kuliko watu wa type ya Wambura,Ndolanga na Rage.
 
Nakuunga mkonbo Mkuu,TFF ni waoga sana na haa hawatki kuona watu wenye misimamo wakitua ndani ya TFF,ndio maana unaona hata hivi sasa wanavyofanya kwenye chaguzi za mikoa na vyama vingine shiriki,wanafuta wanavyotaka ama kuwaondoa wale watu ambao wao wanaamini kwamba ni watu wenye misimamo ya ukweli na wa ni ya dhati ktika kuleta mapinduzi ya soka.

Nikupe mifano michache tu hapa,wamebadili Katiba ya TFF na hasa kwenye kipengele cha elimu na hapa sio kwamba nataka kuwatetea wale watu wanaowaita kwamba hawana elimu,hapana!!!!!!,lakini ni uoga tu wa kuwaogopa wakina Abdalah Bulembo na wenzake wengi tu ambao ni watu wanaofahamika kwamba wana hoja na hasa linapofika kitu kinachoitwa maslahi ya wachezaji ama vyama vya michezo vya mikoa!!!!!

Kibaya zaidi hawahawa TFF wamefikia hatua ya kuingilia hadi chaguzi za mikoa na kuwaondoa watu wenye misimamo mikali na ambao wanaona kwamba kwa namna moja ama nyingine wanaweza kuwasababishia kasheshe huko ndani ya TFF na hawa jamaa ni hatari kwelikweli kwa sababu mkoa ambao wanaona kwamba kuna vichwa vingi vimeingia vya hatari na si kambi yao itakayohakikisha mtu wao atakayegombea anashinda wako tayari kuahirisha uchaguzi hata siku ya uchaguzi,mfano tabora,Rukwa na kwingineko!!

Unajua kila kitu na wakati wake,safari hii watu wenye uelewa na msuala ya mpira na wenye uwezo wa kuhoji maswali walijitokeza kwa wingi sana kuwania nafasi za uongozi ndani ya vyama vya mpira wa miguu huku wengi wakiwa wamelenga kwenda kufanya mabadiliko makubwa wakati wa uchaguzi wa viongozi wa TFF ikiwa ni sanjri na kuhoji maswali tata yaliyoko TFF.

Jamaa walipogundua hilo wameamua kuharibu chaguzi nyingi za mikoa mfano tu jana wamezuia kwa mara ya pili uchaguzi wa viongozi wa waamuzi FRAT kwa sababu tu watu wao hawana uhakika wa kushinda na ndivyo ilivyoonyesha baada ya wajumbe wa FRAT kukaidi agizo la kuzuiwa kufanya uchaguzi na kufanya uchaguzi wao.

leo hii wanakuja na CAF imesema masuala ya marekebisho ya katiba,kanini uchaguzi usifanyike halafu hayao masuala ya marekebisho ya uchaguzi yatafanywa na uongozi utakaochaguliwa???!!!!,hivi hapa kuna logioc ya kusababisha uchaguzi uahirishwe hadi mwezi wa pili mwakani,au ndio wanataka FIFA iingize zile shilingi Milioni 800 za kila mwaka kwa ajili ya maendeleo ya soka nchini wazitafune kwa mara ya mwisho,au zitumike kuwahonga wajumbe????!!!!

Jamani watu wamekuwa wakilalamika sana juu ya masuala ya UFISADI!!!!!!!!!UFISADI hauko CCM tu hata ndani ya TFF hebu fikiria FIFA wanaleta kila mwaka shilingi milioni 800 kwa ajili ya maendeleo ya soka halafu leo hii bingwa anapatiwa shilingi milioni 40!!!!!!!!!!!!!!!Aibu iliyoje ndugu zangu???????!!.

VODACOM wametoa zaidi ya shilingi Bilioni 1.4 kila mwaka halfu bingwa anapatiwa shilingi milioni 40,jamani eeeeeeeeeee inauma sana!!!!!!,pamoja na kwamba sina masters ya Accountat lakini kuna hesabu ya harakaharaka ukiifanya hapa unagundua kamba ni kwa nini wakina Tenga wanadaiwa kumiliki Magorofa Dar????!!!!!!!,wanafanya kazi ya kugawana tu fedha za wachezaji,haiwezekani zaidi ya shilingi Bilioni 2 wanapata kila mwaka kutoka FIFA NA VODACOM Tanzania washindwe kuinua mpira wa Tanzania,ni wazi kwamba haingii akilini,lakini waswahili walinena kwamba siku za mwizi ni 40,tayari Arobaini yao imefika kikubwa hapa ni kuapa nguvu tu hawa wapambanaji waliojipambanua kupambana nao.

kwa leo ngoja niishie hapa lakini naamini nitapata muda mwingine wa kutiririka zaidi kwa sababu nina data zao za kutosha,na ukitaka kuamini hili ninalolisema,mchunguzeni Mwakalebela alivyo tajiri au hata Tenga mwenyewe aliingia na shati moja siku ile pale kwenye ukumbi wa Golden Tulip leo anamiliki zaidi ya magorofa matatu Dar!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom