Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,306
- 271,601
Manispaa ya Temeke pamoja na mambo mengine inakusanya ushuru unaoitwa Service Levy kwa Wafanyabiasha karibu wote wenye leseni za biashara, Yaani Pamoja na kulipia leseni mjasiriamali anatakiwa pia kulipia tozo hiyo, Hii ni mbali na kodi ya TRA, USHURU WA TAKA unaofikia hadi elfu 6 kwa mwezi, Pamoja na Tozo ya Ulinzi. Service levy kwa wafanyabiashara wasio na EFD ni kati ya elfu 60 na elfu 80 kwa mwaka.
Haya ndiyo Mapito ya Wafanyabiashara wa Temeke, na huu ndio mrejesho wa Timu yetu ya Uchunguzi ambayo imesambaa Kuanzia Buza hadi Mtoni Mtongani.
Kitu kingine Kipya ambacho kimegunduliwa ni kwamba Tozo ya Service levy kwa Mfanyabiashara mwenye mashine ya EFD ni Tofauti huyu Ndiye anayekomolewa zaidi, Wachunguzi wetu wanadokeza kwamba wenye hizo machine halali za kodi wanatozwa service levy kila baada ya miezi 3, na wanatozwa kiwango kwa kukatwa % kadhaa kutokana na mauzo yao, kwa maana nyingine tozo hii inaweza kuzidi hata kodi ya TRA kwa mwaka.
Hili jambo linapaswa kurekebishwa haraka ili kuweka usawa, Hii ni kwa sababu hakuna mfanyabiashara yeyote anayeweza kulipa kile ambacho hana, Haitawezekana abadan!
Timu yetu imeagizwa kuonana na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ili atoe Ufafanuzi na achukue hatua kabla mambo hayajaharibika zaidi
Muhimu: Hatupingi watu kulipa kodi, Bali tunachopinga ni kulipishwa kodi kuzidi hata mitaji ya biashara zenyewe.
Haya ndiyo Mapito ya Wafanyabiashara wa Temeke, na huu ndio mrejesho wa Timu yetu ya Uchunguzi ambayo imesambaa Kuanzia Buza hadi Mtoni Mtongani.
Kitu kingine Kipya ambacho kimegunduliwa ni kwamba Tozo ya Service levy kwa Mfanyabiashara mwenye mashine ya EFD ni Tofauti huyu Ndiye anayekomolewa zaidi, Wachunguzi wetu wanadokeza kwamba wenye hizo machine halali za kodi wanatozwa service levy kila baada ya miezi 3, na wanatozwa kiwango kwa kukatwa % kadhaa kutokana na mauzo yao, kwa maana nyingine tozo hii inaweza kuzidi hata kodi ya TRA kwa mwaka.
Hili jambo linapaswa kurekebishwa haraka ili kuweka usawa, Hii ni kwa sababu hakuna mfanyabiashara yeyote anayeweza kulipa kile ambacho hana, Haitawezekana abadan!
Timu yetu imeagizwa kuonana na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ili atoe Ufafanuzi na achukue hatua kabla mambo hayajaharibika zaidi
Muhimu: Hatupingi watu kulipa kodi, Bali tunachopinga ni kulipishwa kodi kuzidi hata mitaji ya biashara zenyewe.