Prisoner 46664
JF-Expert Member
- Dec 18, 2010
- 1,948
- 1,238
Ni wazi kuwa sasa kutokana na ule mtikisiko dhahiri ulioonekana jijini Dar es Salaam wakati mgombea urais wa Ukawa ndugu Edward Lowassa akienda NEC kuchukua fomu za kuomba kugombea urais, serikali iliyo madarakani kupitia kwa jeshi la polisi imeanza kuweweseka na kuanza kufanya mbinu za kuhakikisha wananchi hawaoni jinsi ambavyo mgombea huyu anakubalika na hivyo kupunguza hamasa kwa wananchi wengine.
CCM daima wamekuwa ni watu wa kutumia mbinu chafu kwenye kuhakikisha wanakuwa na advantage kwenye kura hata kama ni kwa kupitia njia isiyo sahihi. Ninakumbuka wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ilivyopiga marufuku midahalo ya wagombea wake wa Ubunge pamoja na Urais kupitia TBC kwa kujua dhahiri kwamba wagombea wengi wa CCM wangeaibika mbele ya wananchi kutokana na kuwa na mengi ya kujibu kulikosababishwa na utendaji mbovu uliokwisha shuhudiwa kutoka kwao miaka mitano iliyotangulia. Waliishia kumfukuza kazi mkurugenzi wa TBC kwa kuruhusu midahalo hii jambo ambalo ni la ajabu na kibabe kuliko inavyoweza kuelezeka ikizingatiwa kuwa duniani kote midahalo ya televisheni ndio njia kubwa kuliko zote za wagombea kutangaza sera zao kwa wapiga kura.
Inashangaza kwamba miaka 55 baada ya uhuru wetu kiongozi wa upinzani na waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri yetu anazuiwa kwenda kwenye msiba ati kwa sababu amefuatana na watu wengi..kweli kabisa?!? Wakati huo huo jeshi la polisi likitangaza kupigwa marufuku maandamano ya wananchi kumsindikiza mgombea kuchukua au kurudisha fomu za urais au kuomba ridhaa ya kugombea kwa wananchi. Ni wazi haya yote yanafanyika ili kuwaficha wananchi ukweli kwamba mgombea wa CCM hakubaliki na watu wengi ili kurahisisha mipango ya kuiba kura ifikapo Octoba.
Mimi nadhani wakati umefika sasa kwa viongozi wa Ukawa kukuna vichwa na kuhakikisha wanatumia magumu haya kujiongezea umaarufu zaidi. Nitatoa mfano. Wakati EL aliposimamishwa na kuzuiwa kwenda kwenye msiba jana mchana, ilikuwa ni nafasi nzuri ya kusimama bila kuchelewa na kutoa hotuba yenye msisimko ya kuwakumbusha wananchi jinsi kitendo hiki kilicho cha ajabu na fedheha kubwa kinavyosimamiwa na uongozi wa juu wa CCM ili kumlinda kiongozi wasiyemtaka. Viongozi wa Ukawa inapasa sasa kutembea na vipasa sauti popote waendapo ili elimu hii ya uraia iweze kutolewa papo kwa papo kwa wananchi na kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni kuwezesha wananchi wengine waone.
Wakati wa urudishaji fomu za NEC ninashauri kwanza itizamwe njia itakayotumiwa na mgombea wa CCM. Ikiwa hakutakuwa na maandamano kabisa basi Ukawa wanaweza kuwaandaa wananchi zaidi ya wale waliojitokeza wakati wa kuchukua fomu kuhakikisha wanasimama pembeni ya barabara karibu na ofisi za NEC na njia zote kuu atakazopita mgombea wa Ukawa ili kuhakikisha watu wanapata nafasi ya kuonesha upendo wao kwa mhe. Lowassa bila kusababisha maandamano.
Vyoyote iwavyo, kwa mbinu yoyote chafu waitumiayo CCM kupitia vyombo vya sheria na usalama kuzuia mafuriko, kuna haja ya kuitumia kwa uangamivu wao zaidi. Siasa mufilisi hazina nafasi tena kwenye nchi yetu.
Ukipewa malimao kamua juice nzuri sana ya malimao umkaribishe aliyekupa.
Victory has arrived. We are the change we had been waiting for.
CCM daima wamekuwa ni watu wa kutumia mbinu chafu kwenye kuhakikisha wanakuwa na advantage kwenye kura hata kama ni kwa kupitia njia isiyo sahihi. Ninakumbuka wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ilivyopiga marufuku midahalo ya wagombea wake wa Ubunge pamoja na Urais kupitia TBC kwa kujua dhahiri kwamba wagombea wengi wa CCM wangeaibika mbele ya wananchi kutokana na kuwa na mengi ya kujibu kulikosababishwa na utendaji mbovu uliokwisha shuhudiwa kutoka kwao miaka mitano iliyotangulia. Waliishia kumfukuza kazi mkurugenzi wa TBC kwa kuruhusu midahalo hii jambo ambalo ni la ajabu na kibabe kuliko inavyoweza kuelezeka ikizingatiwa kuwa duniani kote midahalo ya televisheni ndio njia kubwa kuliko zote za wagombea kutangaza sera zao kwa wapiga kura.
Inashangaza kwamba miaka 55 baada ya uhuru wetu kiongozi wa upinzani na waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri yetu anazuiwa kwenda kwenye msiba ati kwa sababu amefuatana na watu wengi..kweli kabisa?!? Wakati huo huo jeshi la polisi likitangaza kupigwa marufuku maandamano ya wananchi kumsindikiza mgombea kuchukua au kurudisha fomu za urais au kuomba ridhaa ya kugombea kwa wananchi. Ni wazi haya yote yanafanyika ili kuwaficha wananchi ukweli kwamba mgombea wa CCM hakubaliki na watu wengi ili kurahisisha mipango ya kuiba kura ifikapo Octoba.
Mimi nadhani wakati umefika sasa kwa viongozi wa Ukawa kukuna vichwa na kuhakikisha wanatumia magumu haya kujiongezea umaarufu zaidi. Nitatoa mfano. Wakati EL aliposimamishwa na kuzuiwa kwenda kwenye msiba jana mchana, ilikuwa ni nafasi nzuri ya kusimama bila kuchelewa na kutoa hotuba yenye msisimko ya kuwakumbusha wananchi jinsi kitendo hiki kilicho cha ajabu na fedheha kubwa kinavyosimamiwa na uongozi wa juu wa CCM ili kumlinda kiongozi wasiyemtaka. Viongozi wa Ukawa inapasa sasa kutembea na vipasa sauti popote waendapo ili elimu hii ya uraia iweze kutolewa papo kwa papo kwa wananchi na kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni kuwezesha wananchi wengine waone.
Wakati wa urudishaji fomu za NEC ninashauri kwanza itizamwe njia itakayotumiwa na mgombea wa CCM. Ikiwa hakutakuwa na maandamano kabisa basi Ukawa wanaweza kuwaandaa wananchi zaidi ya wale waliojitokeza wakati wa kuchukua fomu kuhakikisha wanasimama pembeni ya barabara karibu na ofisi za NEC na njia zote kuu atakazopita mgombea wa Ukawa ili kuhakikisha watu wanapata nafasi ya kuonesha upendo wao kwa mhe. Lowassa bila kusababisha maandamano.
Vyoyote iwavyo, kwa mbinu yoyote chafu waitumiayo CCM kupitia vyombo vya sheria na usalama kuzuia mafuriko, kuna haja ya kuitumia kwa uangamivu wao zaidi. Siasa mufilisi hazina nafasi tena kwenye nchi yetu.
Ukipewa malimao kamua juice nzuri sana ya malimao umkaribishe aliyekupa.
Victory has arrived. We are the change we had been waiting for.