TCU iache kukumbatia mlango moja wa kwenda mbinguni

TCU iache kukumbatia mlango moja wa kwenda mbinguni

Mligo Augustino

Senior Member
Joined
Nov 29, 2017
Posts
126
Reaction score
278
Kwanza kabisa tunawapongeza TCU kwa kazi nzuri ya kuboresha elimu ya juu nchini. Hata hivyo TCU inatakiwa kubadilika ktk sera zake kulingana na mahitaji halisi ya nchi na jamii ya wakati husika:
1.Syllabus za elimu ya juu bado zipo kizamani. Taaluma inayofundishwa vyuoni haimuandai kijana kujiajiri na kupambana na mahitaji ya nchi na dunia ya sasa. Elimu ya juu imekuwa ni ya madesa tu na kukariri. Na kipimo cha mtu kuwa msomi ni marks tu. Hili ni tatizo kubwa sana kwa usitawi wa nchi. Ndiyo maana tuna wasomi wengi wa vyeti, lakini hawawezi kutatua matatizo.
2.GPA ya 3.5 undergraduate kuwa ndo kigezo msingi cha msomi kufundisha chuo kikuu. Kigezo hiki kimechangia vijana wengi hasa waliohitimu vyuo vikuu vya serikali ambao wanauwezo mkubwa ila GPA iko chini, kushindwa kujiendeleza zaidi kwa hatua ya PhD.Matokeo yake baadhi ya kada kuna upungufu mkubwa sana wa wahadhiri.Ni wazi wahitimu wa vyuo vikuu vya binafsi hupata GPA za juu.
NACTE GPA ya kumfanya mtu afundishe vyuoni ni 3.0.Je kwa nini TCU nao ikiwa GPA ya 3.0 ili kutoa fursa kwa vijana wengi kupata hamasa ya kufanya masters degree na hatimaye PhD? Kwa sababu vyuo vya NACTE vingine vinatoa hadi PhD.Je msingi wa ubaguzi/utofauti huu ni nini?
Kuanzia mwakani haya mafuriko ya elimu bure yatahamia vyuo vikuu kwasababu kundi la kwanza la form 4 wanamaliza mwaka huu(hongera kwa serikali). Je kwa sera hii ya TCU ya kung'ng'ania GPA ya 3.5 tutafika? Wahadhiri watatoka wapi?
Pendekezo:
1.Syllabus za vyuo vikuu ziangaliwe upya na haraka ili ziendane na mahitaji ya wakati.
2.NACTE na TCU wote wawe na GPA ya msingi moja, yaani 3.0.
3.Vyuo vipewe mamlaka zaidi ya kuamua nani anafaa kuwa mwalimu wa chuo kikuu, kulingana na uwezo wake aliouonyesha wakati wa interview. Na interview iwe progressive mpaka madarasa mbele ya wanafunzi.Wahadhiri wasipimwe kwa GPA tu, bali kwa performance. Tunashudia watu wana GPA kubwa lakini akiingia darasani anahema tu na kutoka jasho. Tunajiuliza hii GPA kubwa alipateje? Wanafunzi wanahitaji mwalimu mwenye uwezo mzuri wa kufundisha, siyo mwenye GPA 5.
 
Sijakuelewa, kwani ukiwa na GPA ya chini ya 3.5 huruhusiwi kujiendeleza kusoma masters degree? Hii imeanza lini?

Au unazungumzia kua tutorial assistant?
 
hata huko vyuo vya serikali kuna wanaopata G.P.A za 4.8,acha kulalamika soma kijana
 
Inawezekana mtoa mada anatamani afundishe University ila GPA inamgomea.
 
Kwanza kabisa tunawapongeza TCU kwa kazi nzuri ya kuboresha elimu ya juu nchini. Hata hivyo TCU inatakiwa kubadilika ktk sera zake kulingana na mahitaji halisi ya nchi na jamii ya wakati husika:
1.Syllabus za elimu ya juu bado zipo kizamani. Taaluma inayofundishwa vyuoni haimuandai kijana kujiajiri na kupambana na mahitaji ya nchi na dunia ya sasa. Elimu ya juu imekuwa ni ya madesa tu na kukariri. Na kipimo cha mtu kuwa msomi ni marks tu. Hili ni tatizo kubwa sana kwa usitawi wa nchi. Ndiyo maana tuna wasomi wengi wa vyeti, lakini hawawezi kutatua matatizo.
2.GPA ya 3.5 undergraduate kuwa ndo kigezo msingi cha msomi kufundisha chuo kikuu. Kigezo hiki kimechangia vijana wengi hasa waliohitimu vyuo vikuu vya serikali ambao wanauwezo mkubwa ila GPA iko chini, kushindwa kujiendeleza zaidi kwa hatua ya PhD.Matokeo yake baadhi ya kada kuna upungufu mkubwa sana wa wahadhiri.Ni wazi wahitimu wa vyuo vikuu vya binafsi hupata GPA za juu.
NACTE GPA ya kumfanya mtu afundishe vyuoni ni 3.0.Je kwa nini TCU nao ikiwa GPA ya 3.0 ili kutoa fursa kwa vijana wengi kupata hamasa ya kufanya masters degree na hatimaye PhD? Kwa sababu vyuo vya NACTE vingine vinatoa hadi PhD.Je msingi wa ubaguzi/utofauti huu ni nini?
Kuanzia mwakani haya mafuriko ya elimu bure yatahamia vyuo vikuu kwasababu kundi la kwanza la form 4 wanamaliza mwaka huu(hongera kwa serikali). Je kwa sera hii ya TCU ya kung'ng'ania GPA ya 3.5 tutafika? Wahadhiri watatoka wapi?
Pendekezo:
1.Syllabus za vyuo vikuu ziangaliwe upya na haraka ili ziendane na mahitaji ya wakati.
2.NACTE na TCU wote wawe na GPA ya msingi moja, yaani 3.0.
3.Vyuo vipewe mamlaka zaidi ya kuamua nani anafaa kuwa mwalimu wa chuo kikuu, kulingana na uwezo wake aliouonyesha wakati wa interview. Na interview iwe progressive mpaka madarasa mbele ya wanafunzi.Wahadhiri wasipimwe kwa GPA tu, bali kwa performance. Tunashudia watu wana GPA kubwa lakini akiingia darasani anahema tu na kutoka jasho. Tunajiuliza hii GPA kubwa alipateje? Wanafunzi wanahitaji mwalimu mwenye uwezo mzuri wa kufundisha, siyo mwenye GPA 5.
Hakuna namna ingine, Marks (grades) ndio njia inayotumika kuchuja uwezo wa mwanafunzi.

Ingawa pia nakubaliana na wewe kwamba njia hii sio bora zaidi, na pia wapo wanafunzi wanye uwezo mkubwa kuliko unavyoweza kuonekana kwenye marks zao, ila hao wa aina hiyo ni wachache sana. Kwa kiwango kikubwa kile unachokiona kwenye marks mara nyingi ndio kinchoashiria uwezo wa kitaaluma wa mwanafunzi. Utaratibu huu unatumia duniani pote. Kwahiyo kama unapenda kuwa mwalimu wa chuo kikuu soma kwa bidii, hakuna njia za mkato.

Tena kwa chuo kama UDSM wanavigezo vigimu zaidi, wanataka degree ya kwanza uwe na GPA ya 3.8 na maaters uwe na 4.0.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
We kama una uwezo mkubwa basi pata 3.8 tu hapo utaonekana. Kila ngazi inavigezo vyake ambavyo anayeitaka ngazi hiyo lqzima avitimize kwanza
 
Back
Top Bottom