TCRA vs maudhui ya bure FTA vs maudhui ya kulipia

TCRA vs maudhui ya bure FTA vs maudhui ya kulipia

Kremme

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
471
Reaction score
496
Nimeona haja nimimi pia kudadavua huu mvutano baina ya
TCRA (Mdhibiti aka serikali)
Visimbusi vya kuonyesha maudhui ya Umma ( ie TING, continental, ZUKU)
Visimbusi vya kulipia ( Dstv, Azam pay etc)
Local channels ie ITV, Channel ten, Clouds

UTANGULIZI
TCRA hutoa leseni kwa kila kundi kutegemea na maudhui husika.

LOCAL CHANNEL
Hizi hazimiliki king'amuzi bali huwa na maudhui ya umma(kuonyeshwa bure) huyapeleka kwenye visimbusi kwa makubaliano maalum ie kuna monthly charge za kuilipa visimbusi kama director wa TiNG alivyoelezea.
Hizi local channels hufaidika zaidi kwa matangazo.

MGOGORO:
Ni baada ya visimbusi vya kulipia kuanza kukiuka mikitaba; hapa ishu si kulipisha FTA Channels ishu ni kutotakiwa kuzionyesha HATA KAMA WANGEFANYA BUREE yaani bando likiisha ziiendelee kuonekana, bado ni ukiukwaji.
In short Hawatakiwi kuonyesha local channel kabisa regardless wanatoza ama free.
Hawakushinda zabuni hiyo, walioshinda ni hao wa upande wa pili ambayo ndo waliilalamikia TCRA.
Huenda visimbusi vya kulipia vilishawishiea na wateja wao.
Kisheria Visimbusi vilivyoshinda kuonyesha maudhui ya bure, vina haki ya kulalamika na ni haki pia kwa channel za local kuondolewa kwenye maudhui ya kulipia.

HITIMISHO:
Kama wa maudhui ya kulipia wanataka kuonyesha na maudhui ya bure ya local channel ni vyema waongee meza moja na wenzao wa maudhui ya bure, huyu TCRA yeye awe tu kama msikilizaji. Ie AZAM/DSTV wawe wanalipa percent fulani kwa TING/CONTINENTAL kwa ajili ya local channel kuonekana.
Local Channel wafuate utaratibu, hawaruhusi channels zao kuingizwa kwenye visimbusi vya kulipia. Na wala wasiwasumbue AZAM/DSTV.
AZAM/DSTV zingatieni masharti ya Leseni zenu.



Ni hayo tu.
 
Ila pamoja na sheria na mikataba.. lakini Hekima na Busara iongoze.
 
Hakuna cha sheria wala nini lengo kufunga vyombo vya habari na wanahabari wasitowe habari kuelimisha umma

Kama nikatiba au sheria huyu aliezuwia vyama vyasiasa kufanya siasa anawajibishwa vipi?
 
Mie naona chenga tu, tangu drama hili limeanza mpaka sasa sielewi chochote, hata mleta mada pia sijamuelewa
Kuna hili neno "maudhui" linavyotumiwa na kurudiwarudiwa hata katika sentensi zisizohusika kwenye sakata hili naona kama ndiyo linavuruga zaidi uelewa wa wengi.
 
Siwazime na ving'amuzi vyenyewe tu,hii nchi inachosha leo naskia tena natakiwa kumiliki line moja inachosha.Ukiamka hujui kuna nn kitakuja kesho ni mashaka tu,aaah fanyeni mnachotaka.
 
Mie naona chenga tu, tangu drama hili limeanza mpaka sasa sielewi chochote, hata mleta mada pia sijamuelewa
visumbuzi vya ting na continental pekee ndivyo vina haki ya kuonyesha local channels.. wengine ni wezi, mpk iwe vinginevyo.
 
Back
Top Bottom