TCRA na simu feki

TCRA na simu feki

Kim Jo Ngil

Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
45
Reaction score
17
Simu yangu ya huawei nimenunua kwenye duka la Tigo makao makuu makumbusho. Hivyo nikawa sina wasi wasi kwamba itakuwa feki.
Ila jana nikiwa na wenzangu topic hiyo ikaanza.
Nikasema yangu haiwezi kuwa feki sababu nimeuziwa na Tigo.
Ila baada ya mabishano na kufata maelekezo ya namna ya kujua feki vipi na ya ukweli vipi.
Nikashangaa kuwa yangu ni feki.

Iweje shirika la simu kama Tigo wana bidhaa feki? TCRA wanajua hili?
 
Duh! Pole sana kama vp wafuate ukiwa na lisiti wakupe nyingine uhakikishe kuwa si feki
 
Pole sana Kim Jo Ngil. Nitumie fursa hii kukuomba unisaidie kujua namna ya kutambua simu feki. Huku shamba kupata information mara nyingine ni shida sana. Nisaidie. Unaweza hata kuni pm.
 
Sahihisha hapo juu,hiyo simu umenunua duka la tigo siyo makao makuu ya tigo. Makao makuu ya tigo hayapo makumbusho na huduma za kuuza bidhaa za tigo hazifanyiki makao makuu.

Tigo hawatengenezi simu za mkononi,wao wanatoa huduma za mawasiliano. Bidhaa km simu nao wananunua,lkn kwa bahati hiyo simu uliyonunua ina warranty ya miezi 12. Km ni kweli unachosema irudishe pale dukani na utapewa simu nyingine. Lkn lingine huenda hujui kuangalia kwa kutumia mfumo wa tcra au pengine ulikosea IMEI number. Ahsante
 
Asante kwa usahihisho. Maana yangu ni kuwa simu nimenunua Tigo na sio huawei risiti ni ya Tigo na pia wao kama watoa Huduma za mawasiliano pia wao wanauza bidhaa zake pia. Kwa hiyo simu nimenunua duka la Tigo makao makuu makumbusho. Na Tigo kama Tigo kwa nini wawe na bidhaa feki? Je walio potelewa na risiti na kweli walinunua Tigo miezi kadhaa wanafanya nini?
 
Back
Top Bottom