TCRA mna kazi gani?

TCRA mna kazi gani?

Mnyalu Junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2012
Posts
573
Reaction score
200
Ni jambo lisilopingika na linalofahamika wazi kwamba huu ni ulimwengu wa sayansi na teknolojia. Ni mara nyingi pia unaweza sikia usemi usemao: Sasa hivi dunia ni kama kijiji.

Kukua kwa teknolojia ya kupashana habari ulimwenguni kumeleta urahisi mkubwa kwa watu kujua mambo mbalimbali yaliyopo na yanayoendelea hapa duniani.

Back to the Topic:

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) ni mamlaka iliyowekwa na yenye wajibu kisheria kusimamia masuala yote yahusuyo mawasiliano nchini Tanzania.

Cha kushangaza mamlaka hii imekuwa kimya kwa sintofahamu nyingi zinazohusu mamlaka hiyo. Kuna mambo mengi ambayo binafsi naona mamlaka hii imeshindwa kazi kama vile:

SUALA LA VING'AMUZI
Wakati wanahamasisha mchakato wa kuondoka kwenye mfumo wa analogia na kuingia mfumo wa digitali walitamka wazi ya kwamba chaneli zote za ndani ya nchi (Local Channels) zitawekwa katika ving'amuzi hivyo na zitaoneshwa bure. Chaneli za ziada ndizo zitalipiwa.

Lakini imekuwa kinyume kabisa. Kuna makampuni ya ving'amuzi yaliyowekeza hapa Tanania kama: DSTV, TING, ZUKU, AZAM, CONTINENTAL, nk ambayo kama hujalipia hata kwa vifurushi vyao vya hali ya chini basi huwezi pata chaneli hata moja ya kitanzania!

GHARAMA ZA MITANDAO YA SIMU
Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la gharama za simu pasipo taarifa kwa watumiaji wa simu za mkononi. Watu wengi tulilalamika kuhusu hili lakini wao waliweka pamba masikioni. Sijui wanagawiwaga 10%? Gharama hiyo imekuwa kubwa sana hasa kwa bando za intaneti, kwa mfano mtandao wa Vodacom hata uunge kifurushi chochote cha dakika cha siku umekuwa ukitoa MB 8 pekee!

Baadhi ya viongozi kama Januari Makamba walijifanya kusikitishwa na suala hili na wakaahidi watalishughulikia lakini imekuwa kimya. Sijui tuseme ulikuwa ni unafiki tu??

TCRA kazi imewashinda na mnafaa mlaumiwe kwa kuwabebesha watanzania wa kipato cha chini kama mimi mzigo mkubwa wa gharama kubwa za mawasiliano.


Ukitaka kujua kuwa hawa TCRA ni wanafiki na hawatekelezi majukumu yao kama walivyoainisha soma hapa:
Tovuti Kuu ya Serikali: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
 
Hakuna kinachoniuma kama gharama za Bando, japo biashara ni soko huria ila hii mitandao naona imeungana kutunyonya watanzania.

Haiwezekani bei za vifurushi ziwe Sawa kwa sasa wakati siku za nyuma kulikuwa na ushindani wa kutosha kwenye vifurushi.
 
TCRA Ni sehemu nyingine ambayo serikali hupachika watu ili wapate mishahara na kunenepeana. It is a ceremonial institution good for conferences and symposium
 
TCRA Ni sehemu nyingine ambayo serikali hupachika watu ili wapate mishahara na kunenepeana. It is a ceremonial institution good for conferences and symposium

Yaani haingii akilini kabisa. Hivi kwa mfano kampuni kubwa kama DSTV wangepewa masharti ya kwamba kama wanataka kuwekeza kwenye nchi yetu sharti waweke channels zote za kitanzania na zioneshwe bure hata km hujalipia kinyumbe na hapo wanafutiwa leseni unafikiri wangekataa?

DSTV wana make a lot of money nchini Tanzania hususani kwa channel yao ya Super Sport hivyo wasingekubali kufungiwa leseni eti kwa kutopachika Vichannel kama saba tu vya kitanzania na vikaoneshwa bure
 
Ahsante Mnyalu. Umezungumza kwa niaba yangu pia.

Hii mamlaka siyo bure; itakuwa ina maslahi binafsi kwenye haya makampuni ya simu na vilevile haya yenye ving'amzi. Inakuwaje inakaa tu kimya wakati gharama zinapanda tu kiholela?

Jana niliishiwa pozi mara nilipotaka kuunga kifurushi cha intaneti cha wiki toka airtel. Nilikuwa naamini airtel ndo wana unafui zaidi lakini nao wanazidi kubadilika. Mwanzo nilikuwa naunga kifurushi cha wiki MB800 kwa 1000/= lakini sasahivi kifurushi cha intanet cha wiki ni kuanzia 2000/= ambapo unapewa GB1

Ukienda Tigo au Voda huko ndo majanga zaidi!
 
Jamani kwenye ukweli tuuseme ukweli.
Kwa DSTV hata ikikata bado TBC waweza iangalia kama kawaida
 
Hii mamlaka siyo bure; itakuwa ina maslahi binafsi kwenye haya makampuni ya simu na vilevile haya yenye ving'amzi. Inakuwaje inakaa tu kimya wakati gharama zinapanda tu kiholela?



Jana niliishiwa pozi mara nilipotaka kuunga kifurushi cha intaneti cha wiki toka airtel. Nilikuwa naamini airtel ndo wana unafui zaidi lakini nao wanazidi kubadilika. Mwanzo nilikuwa naunga kifurushi cha wiki MB800 kwa 1000/= lakini sasahivi kifurushi cha intanet cha wiki ni kuanzia 2000/= ambapo unapewa GB1



Ukienda Tigo au Voda huko ndo majanga zaidi!


Bando langu liliisha leo, nikaenda kununua vocha ya buku nijiunge. Nimeshangaa kuona hamna kifurushi cha buku, minimum sasa ni buku mbili kwa 1gb damn it!! Huku ukijiunga kawaida unapata 10mb, iwe jero au buku..pathetic toka kwa mitandao ya simu. Huku wengine wanafanya dunia iwe kiganjani, Tanzania tunataka kurudu karne ya 20.
 
Jamani kwenye ukweli tuuseme ukweli.
Kwa DSTV hata ikikata bado TBC waweza iangalia kama kawaida

Mbona huwa haionyeshi ITV wala Chanel ten hafu mitandao ya simu sio AIRTEL voda tigo kila siku wanapandisha gharama bila kujali uchumi wa vwananchi walio wengi kama si wizi ni nini au hawataki Watanzania wapate habari kipindi cha uchaguzi, ndo wanajitungia sheria za ajabu inachosha sana huu wizi usio jali Watanzania, ingawa wamepewa dhamana ya kutumikia wananchi.
 
Bando langu liliisha leo, nikaenda kununua vocha ya buku nijiunge. Nimeshangaa kuona hamna kifurushi cha buku, minimum sasa ni buku mbili kwa 1gb damn it!! Huku ukijiunga kawaida unapata 10mb, iwe jero au buku..pathetic toka kwa mitandao ya simu. Huku wengine wanafanya dunia iwe kiganjani, Tanzania tunataka kurudu karne ya 20.

Wana agenda ya watu wasipate habari solutions zao ni kukomoa Watanzania kwa kupandisha vifurushi wakati dunia imekua kijiji badala kuturahisishia maisha wao pamoja na watoa waamuzi wanazidi kunyonya hata kidogo tulicho nacho.
 
Jamani kwenye ukweli tuuseme ukweli.
Kwa DSTV hata ikikata bado TBC waweza iangalia kama kawaida

Tunataka ITV, CAPITAL, EATV, CH10, STARTV, CLOUDS, TBC2 nazo tuzipate bure ndan ya DsTV coz ndo ahadi yao TCRA
 
Hata azam nao usipolipia local channels hawaonyeshi , tcra wapo kwa maslahi yao tu, unaweza kununua kifurushi cha wiki kwenye simu, kati ya siku saba za wiki , siku mbili mtandao haupatikani lakini kwa kuwa Hakuna mtetezi wa mteja, mteja atapata pungufu ya makubaliano.
Kweli TCRA haina meno, hawatimizi majukumu yao.
 
Hakuna kinachoniuma kama gharama za Bando, japo biashara ni soko huria ila hii mitandao naona imeungana kutunyonya watanzania.

Haiwezekani bei za vifurushi ziwe Sawa kwa sasa wakati siku za nyuma kulikuwa na ushindani wa kutosha kwenye vifurushi.

Uchaguzi unakaribia mccm Tunahitaji pesa za kampeni
 
Tcra mm naona wapo wapo tuu hizi kero nyng za mitandao kuibia watumiaji kwani wao hawajui kama hawajui? Voda ssa ukiweka let say 5000 haujapiga cm wala huna ktu unachokilipia ukijisahau kama masaa kadhaa usijiunge kupiga wala usinunue bandle,ukitaka kujiunga utaona imebaki hela ndogo, ukiwapigia kuwa naomba taharifa kabla cjatuma ka line kenu wanasema matatizo ya mitandao then baada ya muda unakuta 5000 tena,ukipiga hesabu tupo wangapi tunaoibiwa daily bila kufahamu ni wengi sana.ujambazi ni ujambazi uwe wa siraha au wa mitandao inakuaje tcra mpo kimya au hamna vitendea kazi vya kujua haya? Na kama ilo ndio kwa nn isivunjwe tuu tujue hakuna tcra.
 
Hawa wezi wa dk na vifurushi tigo na voda na gharama kubadilika wanavyotaka bila hata kuihusisha tcra nadhani ni makampuni yanayopata super profit sana na kodi wanalipa kiduchu, watanzania tup busy na vocha kila dakika.wangevunja hii tcra waunde chombo kingine cha kisasa na watu wachache sio hawa,IGP Mangu na huu ni ujambazi ila hawatumii siraha wanaotusimamia hawana uwezo wa kuwakamata.kwani police aina ingine ya ujambazi huwa hamushughuki nao kama huu..
 
Jamani kwenye ukweli tuuseme ukweli.
Kwa DSTV hata ikikata bado TBC waweza iangalia kama kawaida

We acha uongo wewe, unatumia DSTv gani? kwenye DSTV usipolipia chanel zinazoonekana ni zile za kichina basi CCTV tu.
 
Hebu tuiangalie hata Exchange Rate ya US Dollar ni shilingi ngapi tuache tu kulalamimika hapa zaidi ya tatizo.
CCM OYEE
 
Tunataka ITV, CAPITAL, EATV, CH10, STARTV, CLOUDS, TBC2 nazo tuzipate bure ndan ya DsTV coz ndo ahadi yao TCRA

Kwanini usiende ofisini kwa TCRA ukawauliza kwanini hawajatimiza ahadi yao?

We acha uongo wewe, unatumia DSTv gani? kwenye DSTV usipolipia chanel zinazoonekana ni zile za kichina basi CCTV tu.

Kwani kuna DSTV ngapi hapa Afrika?

kama haujui kitu pita tuu si lazima kuchangia mkuu, umeongea uongo.

Sina sababu ya kusema uongo, kama watumia premium jaribu utaona kuwa usipolipia bado TBC itakuwa inafanya kazi
 
Back
Top Bottom