Moja kati ya mambo yenye gharama kubwa kwenye utangazaji TV ni kuonyesha tukio moja kwa moja (live). Ndio maana hata kwenye mechi za kimataifa zionyeshwazo moja kwa moja, wakati wa mapumziko huwa hakuonyweshi kinachotokea uwanjani. Ndio maana vituo vingi vya TV hasa kwa nchi zinazoendelea hushindwa kununua haki za kurusha matangazo ya aina hiyo.Kwa hivyo tukio lolote la moja kwa moja mara nyingi hutegemea wadhamini kufidia gharama hizo. Udhamini nao hutegemea mvuto wa tukio linalotaka kuonyeshwa. Kama meachi za Stars hazina mvuto,TBC watalazimika kubeba matangazo hayo wao wenyewe. Inaweza kuwa ni sehemu ya wajibu wao kwa jamii kama Shirika (corporate social responsibility). Lakini umma ukizowea hivyo, TBC watalazimika kugharimika kwenye kila mechi ya Stars. Wema hautakiwi kuzidi uwezo.