Televisheni ya Taifa (TBC) inayoendeshwa kwa kodi za wananchi imeshindwa kuwahudumia watanzania kutokana na kupunguza masafa yake(signal). Sasa hivi TBC inaonwa na watu wachache hapa nchini. Televisheni nyingi za watu binafsi zinawafikia watu wengi ikilinganishwa na TBC. Hata Msumbiji wametushinda maana hadi sisi tunaoishi kanda ya ziwa tunaona chaneli zao vizuri kwa kutumia madishi hata yale madogo. TBC hamuoni aibu?