Abraham Lincolnn
JF-Expert Member
- Apr 12, 2018
- 2,499
- 4,211
Hivi huyu Mtu wa Graphics TBC amekaa tu na ameridhika kabisa na kazi yake?
Yaani hapa ndipo mwisho wa akili yake katika kudesign hata Logo tu ambayo inabeba taswira yote ya shirika kubwa la taifa kama TBC?
Hivi hawezi kujifunza hata kwa Televishen za wenzetu? Hata kama hakuna content za maana ndani ya channel lakini hata design nazo ziwe local kiasi hicho?
Maandishi font za kizamani,Rangi hazivutii.Yaani hata ile alama yao ya "MBASHARA" walivyodesign wanaona ni sawa tu? Graphics hazina mvuto kabisa.
Videographer yupo tu? Na anakula mshahara?
Tukija kwenye Sound ndiyo matatizo matupu! Volume unaweka 30 inajiongeza yenyewe mpaka 50 ukipunguza na yenyewe inarudi sifuri .Yaani tafran mara ipande mara ishuke.
Yaani likija lile litangazo la "unaangalia TBC 1" Sauti mpaka majirani wanashtuka,mpaka mtazamaji naye anashtuka kama alisinzia! Ukishika remote kupunguza sauti inarudi normal baada ya tangazo sauti inashuka kabisa hata hausikii
Matatizo madogo kama haya ni aibu kwa chombo cha Taifa! Ukiachilia mbali content zake zisizokwenda na wakati, Mfano baadhi ya vipindi na nyimbo kurudiwa rudiwa miezi mingi bila mabadiliko! Ina maana hata vituo vya watu binafsi vinaizidi serikali kwa ubora! hali ya kuwa bajeti ya serikali ni kubwa zaidi yao.
TBC mjitafakari
Yaani hapa ndipo mwisho wa akili yake katika kudesign hata Logo tu ambayo inabeba taswira yote ya shirika kubwa la taifa kama TBC?
Hivi hawezi kujifunza hata kwa Televishen za wenzetu? Hata kama hakuna content za maana ndani ya channel lakini hata design nazo ziwe local kiasi hicho?
Maandishi font za kizamani,Rangi hazivutii.Yaani hata ile alama yao ya "MBASHARA" walivyodesign wanaona ni sawa tu? Graphics hazina mvuto kabisa.
Videographer yupo tu? Na anakula mshahara?
Tukija kwenye Sound ndiyo matatizo matupu! Volume unaweka 30 inajiongeza yenyewe mpaka 50 ukipunguza na yenyewe inarudi sifuri .Yaani tafran mara ipande mara ishuke.
Yaani likija lile litangazo la "unaangalia TBC 1" Sauti mpaka majirani wanashtuka,mpaka mtazamaji naye anashtuka kama alisinzia! Ukishika remote kupunguza sauti inarudi normal baada ya tangazo sauti inashuka kabisa hata hausikii
Matatizo madogo kama haya ni aibu kwa chombo cha Taifa! Ukiachilia mbali content zake zisizokwenda na wakati, Mfano baadhi ya vipindi na nyimbo kurudiwa rudiwa miezi mingi bila mabadiliko! Ina maana hata vituo vya watu binafsi vinaizidi serikali kwa ubora! hali ya kuwa bajeti ya serikali ni kubwa zaidi yao.
TBC mjitafakari