Shoctopus
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 3,435
- 1,995
Asalam aleikhoom wana JF!
Baada ya kusikia kwamba kuna mpango wa kuanzisha project kubwa ya SGR TAZARA kabla ya project aina hiyohiyo ya TRC kukamilika binafsi nilistuka sana! Hadi sasa najiuliza hivi nchi hii imelogwa na nani?
Kwasababu sikutegemea kabisa kwamba kabla ya kukamilika kwa SGR ya TRC na mradi mkubwa wa hydropower Kihansi na mingine kama bomba la mafuta la Hoima-Tanga, kwamba Tanzania ingeanzisha au hata kufikiria kubuni tena mradi mwingine usiojulikana faida yake katika mazingira ya kiuchumi sasa na siku zijazo!
Tatizo la TAZARA ni kukosa mzigo upande wa Zambia bas! Na hii ni kwasababu Zambia wana mashirika mawili ya reli: TAZARA na Zambia railways halafu reli zake ni Cape gauge.
Mzigo wa Zambia kupitia TAZARA kuja Dar es Salaam ulipungua sana baada ya utawala wa makaburu South Africa kuondoa. Lakini hata kabla ya "uhuru" wa SA sehemu ya mzigo wa Zambia umekuwa unapita Msumbiji mpaka bandari ya Beira au Maputo.
Zipo sababu nyingi na za msingi za Zambia kupitisha mzigo wake SA au Mozambique lakini nani asiyejua matatizo ya TAZARA baada ya kukosa mzigo wa Zambia? Hata mzigo wa upande wa Tanzania nako ni matatizo kutokana na ushindani wa usafiri wa barabara.
Lazima tukubaliane kwamba katika mazingira ya sasa reli haiwezi kushindana na barabara nzuri za lami.
Na hilo ndiyo litakuwa tatizo kubwa la SGR ya TRC ambayo inajengwa sambamba na meter gauge ya mkoloni ambayo lishanyan'ganywa mzigo kwa ushindani wa usafiri wa barabara!
Kwahiyo kama hali ndiyo hiyo mzigo wa SGR mpya ya TAZARA utatoka wapi?
Kwahiyo mpaka sasa hatujaona kwamba tunapigwa au tunajipiga wenyewe vita ya kiuchumi kwa kujipa jukumu la kugharamia miradi kama hii kwa kutegemea uchumi wa majirani zetu.
Tulisapoti vita vya ukombozi kusini SA, Zambia, Zimbabwe, Mozambique na Uganda kwa gharama kubwa za uchumi wetu. Matokeo yake nchi hizo baadhi wametupita kiuchumi na hawana habari na sisi!
Kenya wanayo SGR kati ya Mombasa na Nairobi; lakini inasemekana tayari iko hoi kutokana na ushindani wa usafiri wa barabara. Nenda China, USA, Europe au kokote kwenye network nzuri ya highways, biashara ya reli HAINA FAIDA. Tutaogezewa tozo tu!
Last but not least! Kutokana na vita ya Russia na Ukraine uchumi wa dunia uko hatarini na nchi kama Tz tayari bei ya mafuta inapanda kila mwezi! Badala ya kubuni white elephant lingine tupunguze mateso zaidi kwa Mtanzania.
Baada ya kusikia kwamba kuna mpango wa kuanzisha project kubwa ya SGR TAZARA kabla ya project aina hiyohiyo ya TRC kukamilika binafsi nilistuka sana! Hadi sasa najiuliza hivi nchi hii imelogwa na nani?
Kwasababu sikutegemea kabisa kwamba kabla ya kukamilika kwa SGR ya TRC na mradi mkubwa wa hydropower Kihansi na mingine kama bomba la mafuta la Hoima-Tanga, kwamba Tanzania ingeanzisha au hata kufikiria kubuni tena mradi mwingine usiojulikana faida yake katika mazingira ya kiuchumi sasa na siku zijazo!
Tatizo la TAZARA ni kukosa mzigo upande wa Zambia bas! Na hii ni kwasababu Zambia wana mashirika mawili ya reli: TAZARA na Zambia railways halafu reli zake ni Cape gauge.
Mzigo wa Zambia kupitia TAZARA kuja Dar es Salaam ulipungua sana baada ya utawala wa makaburu South Africa kuondoa. Lakini hata kabla ya "uhuru" wa SA sehemu ya mzigo wa Zambia umekuwa unapita Msumbiji mpaka bandari ya Beira au Maputo.
Zipo sababu nyingi na za msingi za Zambia kupitisha mzigo wake SA au Mozambique lakini nani asiyejua matatizo ya TAZARA baada ya kukosa mzigo wa Zambia? Hata mzigo wa upande wa Tanzania nako ni matatizo kutokana na ushindani wa usafiri wa barabara.
Lazima tukubaliane kwamba katika mazingira ya sasa reli haiwezi kushindana na barabara nzuri za lami.
Na hilo ndiyo litakuwa tatizo kubwa la SGR ya TRC ambayo inajengwa sambamba na meter gauge ya mkoloni ambayo lishanyan'ganywa mzigo kwa ushindani wa usafiri wa barabara!
Kwahiyo kama hali ndiyo hiyo mzigo wa SGR mpya ya TAZARA utatoka wapi?
Kwahiyo mpaka sasa hatujaona kwamba tunapigwa au tunajipiga wenyewe vita ya kiuchumi kwa kujipa jukumu la kugharamia miradi kama hii kwa kutegemea uchumi wa majirani zetu.
Tulisapoti vita vya ukombozi kusini SA, Zambia, Zimbabwe, Mozambique na Uganda kwa gharama kubwa za uchumi wetu. Matokeo yake nchi hizo baadhi wametupita kiuchumi na hawana habari na sisi!
Kenya wanayo SGR kati ya Mombasa na Nairobi; lakini inasemekana tayari iko hoi kutokana na ushindani wa usafiri wa barabara. Nenda China, USA, Europe au kokote kwenye network nzuri ya highways, biashara ya reli HAINA FAIDA. Tutaogezewa tozo tu!
Last but not least! Kutokana na vita ya Russia na Ukraine uchumi wa dunia uko hatarini na nchi kama Tz tayari bei ya mafuta inapanda kila mwezi! Badala ya kubuni white elephant lingine tupunguze mateso zaidi kwa Mtanzania.