kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Wako Wazanzibar ambao wanadhani hali yao ya maisha itaboreka kama wakijitenga kutoka bara, mimi sidhani kama itakuwa hivyo. Tangu 1964 ya Muungano, Zanzibar ilipewa fursa ya kipekee ndani ya muungano ya kujiamulia mambo yake mengi yenyewe bila ya kuingiliwa na serikali kuu wala watu wa Tanganyika.
Wazanzibar sio wengi ukilinganisha na wakazi wa Wilaya za Bara sebuse mikoa.
Kutokana na hali ya kijografia ya Zanzibar ningetarajia Zanzibar ingekuwa kitovu cha uvuvi, usafiri majini na bandari kubwa nchini na Africa Mashariki lakini hili halikutokea na wala halitokei. Ukiwauliza wanasingizia Muungano.
Wako busy na Zanzibar ni nchi, Zanzibar ni nchi kila siku na siku zote. Wazanzibar hawataki nchi bali wanachotaka wao ni maisha mazuri kiuchumi, na hii ndiyo inayosababisha wazanzibar wengi wametawanyikia Tanganyika, Dubai, UK, Emirates, n.k kutafuta uchumi.
Viongozi wa Zanzibar badala ya kununua meli kubwa za uvuvi na usafiri na usafirishaji wanatumia hela nyingi kugharamia Ikulu, Mikoa mingi(vijimikoa), Wilaya nyingi(vijiwilaya), Tarafa, Kata na vijiji.
Zanzibar inagharamia bunge na baraza la wawakilishi. Zanzibar ilitakiwa kujiendesha kama jimbo/mkoa maalum ndani ya Tanzania kwa kivuli cha Muungano na sio nchi ili kupunguza gharama zake za uendeshaji kama vimulimuli, mabenzi, kutunza wastaafu, mishahara ya Rais na mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya na watumishi wengine ndani ya kivuli cha "Zanzibar ni Nchi".
Hata kama Zanzibar itajitenga, hali ya maisha ya wananchi wake haitaboreka kama inavyodhaniwa, badala yake Zanzibar itakuwa lango kuu la uhalifu kama vile biashara ya madawa ya kulevya, ushoga, na ugaidi.
Kwasababu sioni kitu chochote kinachosababishwa na Muungano kinachoifanya Zanzibar isiwe na meli na viwanda vya mazao ya uvuvi, isiwe na meli za usafiri na usafirishaji, isiwe mzalishaji mkuu wa karafuu na mbata duniani.
Badala yake Bakhessa ndiye mwenye meli za uhakika zinazotoka na kuingia Zanzibar.
Zanzibar Oyeee!!
Wazanzibar sio wengi ukilinganisha na wakazi wa Wilaya za Bara sebuse mikoa.
Kutokana na hali ya kijografia ya Zanzibar ningetarajia Zanzibar ingekuwa kitovu cha uvuvi, usafiri majini na bandari kubwa nchini na Africa Mashariki lakini hili halikutokea na wala halitokei. Ukiwauliza wanasingizia Muungano.
Wako busy na Zanzibar ni nchi, Zanzibar ni nchi kila siku na siku zote. Wazanzibar hawataki nchi bali wanachotaka wao ni maisha mazuri kiuchumi, na hii ndiyo inayosababisha wazanzibar wengi wametawanyikia Tanganyika, Dubai, UK, Emirates, n.k kutafuta uchumi.
Viongozi wa Zanzibar badala ya kununua meli kubwa za uvuvi na usafiri na usafirishaji wanatumia hela nyingi kugharamia Ikulu, Mikoa mingi(vijimikoa), Wilaya nyingi(vijiwilaya), Tarafa, Kata na vijiji.
Zanzibar inagharamia bunge na baraza la wawakilishi. Zanzibar ilitakiwa kujiendesha kama jimbo/mkoa maalum ndani ya Tanzania kwa kivuli cha Muungano na sio nchi ili kupunguza gharama zake za uendeshaji kama vimulimuli, mabenzi, kutunza wastaafu, mishahara ya Rais na mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya na watumishi wengine ndani ya kivuli cha "Zanzibar ni Nchi".
Hata kama Zanzibar itajitenga, hali ya maisha ya wananchi wake haitaboreka kama inavyodhaniwa, badala yake Zanzibar itakuwa lango kuu la uhalifu kama vile biashara ya madawa ya kulevya, ushoga, na ugaidi.
Kwasababu sioni kitu chochote kinachosababishwa na Muungano kinachoifanya Zanzibar isiwe na meli na viwanda vya mazao ya uvuvi, isiwe na meli za usafiri na usafirishaji, isiwe mzalishaji mkuu wa karafuu na mbata duniani.
Badala yake Bakhessa ndiye mwenye meli za uhakika zinazotoka na kuingia Zanzibar.
Zanzibar Oyeee!!