Tatizo la umeme Tanzania

Tatizo la umeme Tanzania

thirteen06

Senior Member
Joined
May 17, 2021
Posts
137
Reaction score
120
Moja kati ya maeneo katika nchi yetu ambayo yanayotumia umeme kutoka nchi jirani Ni wilaya ya bukoba mkoani kagera.

Wilaya hii hupokea umeme kutoka nchi jirani ya uganda. Ni nadra Sana kusikia umeme unakatika katika maeneo haya ambayo umeme wake unatokea nchi jirani ya uganda na hata ukikatika Basi Ni kwa muda mfupi Sana utarejea. Labda tujaribu kujifunza kwa wenzetu wa Uganda wamewezaje?

Huduma nyingi za kiserikali hutegemea umeme, hospitali, mashirika ya serikali, binafsi, TRA, huduma za zakawaida za kila siku, biashara ,viwanda Yani taja vyote muhimu kwa ustawi wa nchi.

Tusubiri stiegler's gorge? Maendeleo yanatusubiri? Isije kuwa stiegler's gorge ikakamilika tukaendelea kuwa na shida ile ile maana tuliamini gesi itakuwa suluhu lakini tatizo nililelile.
 
Tatizo Ni wenye dhamana wanafanya udalali wa umeme.
Wanauza jenerata..Kwa Sasa idadi kubwa ya contena zenye jenereta zinaingia nchini
 
Ni aibu kwa jiji kama dar kitovu cha uchumi Tanzania kuwa na tatizo la umeme mikoani sawa ila dar inasikitisha sana kila mtu anajipigania mwenyewe kwenye hii nchi.
 
Ni aibu kwa jiji kama dar kitovu cha uchumi Tanzania kuwa na tatizo la umeme mikoani sawa ila dar inasikitisha sana kila mtu anajipigania mwenyewe kwenye hii nchi.
Mkuu mikoa yote inaihitaji labda useme kipaumbele Cha Kwanza kiwe kwenye most populated area, lakini mikoa yote inaumuhimu wa uihitaji ule ule kwakuwa huduma zinazohitaji umeme mikoani na dar Ni almost the same.
 
Back
Top Bottom