Tatizo la ugumba kwa wanawake na wanaume

May 30, 2017
10
8
ab7419607c4779f9dc80607cfd81434e.jpg



Nimeona nielekeze hili kwa faida mada hizi zitakuja mfululizo kwa faida



TATIZO LA UGUMBA

Ugumba kama linatibika nimeona ni bora nielezee hapa kwa faida ya wote huenda hata wewe au ndugu yako unasumbuliwa na tatizo hili, kwa kifupi tatizo hili ni kubwa sana kwa wanawake na wanaume takriban 30%_40%ya tatizo hili la Ugumba linawakumba wanaume na 40%_50% huwakumba wanawake wakati 10%-30% zilzobak ya tatizo hili husababishwa kwa pamoja na matatzo Kati ya mwanamme na mwanamke,
UNAJUA MAANA YA UGUMBA??
Ugumba ni Ile hali ya mwanamme /mwanamke kupoteza uwezo wa kutungisha au kubeba mimba
~hii kwa mwanaume tunasema anashindwa kutungisha mimba ilhal anakutana kimwili na mkewe pasipo kutumia condom na mkewe pia hatumii vizuizi vya mimba, Hali huwa hivi kwa upande wa mwanamke naye huwa anashindwa kubeba mimba ilhal hatumii dawa za Uzazi wa mpango ambapo pia anakutana na mumewe Bila Kinga ila anashindwa kupata ujauzito
~katika familia 5 zinazofanya mapenzi katika wakati muafaka wa OVULATION wakiwa na malengo ya kupata mtoto ni familia moja tu ndiyo inafanikiwa kupata mtoto,
~kuna aina mbil za Ugumba ambazo ni ÷
(1)PRIMARY INFERTILITY ~hii ni aina ya kwanza ya Ugumba ambayo yenyewe inawahusisha watu ambao hawakuwahi kubahatika kupata mtoto hata mmoja yan mwanaume anajitahid kutungisha mimba huku mwenza wake akiwa hatumii kizuizi mimba Lakin hafankiw na huku pia mwanamke anajitahid kubeba mimba ilhal hatumii dawa za Uzazi wa mpango Lakin hafankiw
(2)SECONDARY INFERTILITY ~hii ni aina ya Ugumba ambayo hutokea baadae yani ni baada ya mwanamke/mwanamme kuzaa/kuzalisha Mara Moja maishani mwao na hawafanikiwi kupata mtoto mwingne
VISABABISHI/VYANZO VYA UGUMBA
~kuna Vyanzo vingi sana vinavyosababisha Ugumba, vifuatavyo ni Vyanzo vya Ugumba
UTOAJI WA MIMBA
TATIZO LA HORMONE IMBALANCE (kutokuwa na uwiano mzuri wa homoni kwa mwanamke)
MATUMIZI YA DAWA/SINDANO ZA UZAZI WA MPANGO
KUUGUA UGONJWA WA FANGASI UKENI KWA MUDA MREFU (VAGINAL CANDIDIASIS)
KULEGEA KWA SHINGO YA KIZAZI
KUWA NA MSONGO WA MAWAZO
MATATIZO YA UZAZI OVARIES KUSHINDWA KUTOA MAYAI
KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI MATUMIZI YA POMBE/BANGI /SIGARA NI HATARI
KUTOKWA NA UCHAFU SEHEMU ZA SIRI WENYE HARUFU MBAYA
KUSUMBULIWA NA MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA HEDHI KWA MUDA MREFU
KUPATA MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA NA KUWA NA MAUMIVU MAKALI CHINI YA KITOVU KWA MUDA MREFU
MWILI KUWA MNENE KUPITA KIAS
KUWA NA MAGONJWA YA ZINAA, KAMA KISONONO, PID, GONO NK
MWANAUME KUWA NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
KUZIBA KWA MIRIJA YA KUPITISHIA MANII
KUWA NA MBEGU CHACHE (uchache wa shahawa)
DALILI ZA UGUMBA
kutokushika mimba katika siku za hatari
siku zako za hedhi kutokua katika mpangilio yani zinapishana na kubadilka tarehe kila wakati
kupata Maumivu makali chini ya tumbo Mara kwa Mara
mwili kuwa na manyoya kifuani au kuwa na ndevu nyingi
kushindwa kushiriki tendo la ndoa/kutokufurahia tendo la ndoa kwasababu unapata maumivu makali
kutokuwa na MSISIMKO
kupata Maumivu makali chini ya kitovu upande wa kulia au kushoto kwa ndani
kutokuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa Zaidi ya Mara moja
uume kushindwa kusimama
kufika Kileleni mapema
kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa
MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA
~Matibabu ya Ugumba huhusisha wenzi wote wawili na yanahtaji uvumilvu na uelewa kwasababu yanaweza kuchukua muda mrefu kuona matokeo, matibabu haya hufanyika kwa kuangalia majibu kutoka ktk vipimo mbalimbali ambapo pia hujumuisha upasuaj na dawa pia ni vizuri mtu kujikinga na tatizo hili kutokana na athari zake kuwa kubwa, njia ya kujiknga na tatizo hili ni ÷
kuondoa mawazo
kujikinga na magonjwa mbalmbal kama vile fangas, uti nk
acha kutumia dawa za Uzaz wa mpango
jitahd uwe unachuguza vizuri afya yako
mwanaume acha kutumia viagra na dawa za kemikal
jiepushe na kansa na kisukar
zingatia afya bora kwa kula mlo kamili
punguza mwili
acha kutumia dawa za kulevya na unywaji wa pombe
MADHARA YA UGUMBA
Huondoa Amani katika mahusiano
huleta majuto, huzuni na hasira
husababisha mawazo na kuhatarisha afya yako.....kwa faida ya wengi share post hii
 
Asante muelimishaji, ila ningependa utoe ufafanuzi juu ya vyanzo vya ugumba yaan mfano. Kuumwa tumbo la prd ni mechanism gan hapo inasababisha kutopata mimba?
 
Hayo madawa nishakunywa nishapoteza pesa,sasa nimebaki nasibiri menopause. Sijiumbui tena,,labda za bure
 
Sijawahi kutoa,,niiwahi kuzaa akafariki
Pole,usikate tamaa ndugu Mwenyezi Mungu atakupa tu hiyo furaha,

Kuna page ndakuwekea link hapo chini ni ya insta ni ya mambo ya uzazi utaipitia,harafu ukiona poa utanishtua pm nikuombee link ya group la whatsapp la mambo ya uzazi watu ni wengi wenye shida kama yako wanafanya kupewa dondoo mbili tatu kuhusiana na hilo kuna madokta pia,hilo group ni free
(@reproductive_health_solution) • Instagram photos and videos
 
Pole,usikate tamaa ndugu Mwenyezi Mungu atakupa tu hiyo furaha,

Kuna page ndakuwekea link hapo chini ni ya insta ni ya mambo ya uzazi utaipitia,harafu ukiona poa utanishtua pm nikuombee link ya group la whatsapp la mambo ya uzazi watu ni wengi wenye shida kama yako wanafanya kupewa dondoo mbili tatu kuhusiana na hilo kuna madokta pia,hilo group ni free
(@reproductive_health_solution) • Instagram photos and videos
Ahsante,, hao ni wauza Dawa,,kama hao walishanilia tu pesa yangu,. Sitaki nishakubaliana na hali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom