Tatizo la foleni dar

Tatizo la foleni dar

Danvis

Member
Joined
Apr 27, 2012
Posts
15
Reaction score
1
Je? SEREKALI IFANYEJE ILI IWEZE KUPUNGUZA FOLENI DAR BILA KUTUMIA FEDHA YA MWANACHI WAKE YA KODI.
 
Foleni itapungua pale tu public transport itakapokua imara na si vipanya na costa kutumika.kutumia kodi haiepukiki maana ndicho chanzo peke cha mapato ya serekali. Mimi nashahuli kujengwe public parking maeneo kama ubungu, mwenge,Tazara,na kurasini kisha kuwekwe mageti ili anaetaka kuingia mjini ni kigari chake alipie kiasi kama elfu 20 kupita kwenye geti hilo au apaki gari apande bus. Utaona jinsi msongamano mjini utapungua na mapato kuongezeka.
 
Punguza mchecheto,Rejea ahadi za mcheza ngoma Flyovers zinakuja!
 
Hakuna nia ya dhati katika kutatua hili tuombe MUNGU na tufanye jitihada za hali na mali CDM washike hatamu then matatizo kama haya yatakuwa historia. We need change! we need to overhaul the entire system. However for this to happen its me and you! it can be done just play your part.
 
Kuna reli inatoka town Hadi ubungo, Kama kungekuwa na dhamira ya kweli kuondoa msongamano hiyo reli ingefanya kazi ya kusafirisha abiria pamoja na ile ya maeneo ya pugu na gongo la mboto. Ingejengwa miundombinu ya kuwezesha matumizi ya reli na kununua mabehewa na kuanzisha usafiri wa treni kutoka katikati ya jiji hadi maeneo ya pembezoni. Maeneo mengine ungeangaliwa usafiri kwa njia ya bahari kuelekea maeneo ya kunduchi na kuendelea, naaminitungetatua tatizo la msongamano kwa kiasi kikubwa
 
Ukiwa Uko barabarani unakutana na Vioja Vingi!! Sometimes Kuna mahali taa zinaruhusu na mtu/dereva anachukua zaidi ya seconde Ishirini (20) kuondoka!! Kwa nchi za wenzetu hili ni kosa Kubwa!! Kwani taa Huongozwa under timed based na kitendo cha kufanya delay unaaribu utaratibu mzima!! Kosa Hili Hujulikana kama OBSTRUCTION!! and you are supposed to be penalised!! Sasa unakuta polisi wapo na Wamekaa kwenye Junction/INTERSECTION na hawaoni hili ni Tatizo na ni kosa kisheria!! Taa zinaruhusu FOR 60 seconds Yanapita magari 8 TU!! Huu ni uzembe wa madereva Husika!! Watu wanatakiwa wawe Sharp wanapokuwa Barabarani, Sio unajiendeshea kama unaingia Nyumbani kwako!!
Naomba Vyombo Husika Viweke Tahadhari ya kuonyesha minimum speed Mtu anatakiwa Kupita kwenye Intersection ili kupata Maximum Traffic flow!! Say 60 seconds 40 Vehicles!! at least practical!! Hili Ni tatizo na linanisikitisha sana!!

POLISI AMKENI MTATUE TATIZO HILI NAJUA HAMLIJUI HILI!!
 
hakuna lolote litakalowezekana kama ccm bado itakuwa madarakani. tutajadili hadi tutachoka, majibu hayapo hadi sisiemu wang'oke. ccm ni kizuizi cha maendeleo tz. viongozi wake mambumbumbu, hawana vision na taifa hili, kilichobaki kwao ni kulindana, kupambana wao kwa wao na kujali maslahi ya watu wachache...wananchi na maendeleo ya nchi yamewekwa pembeni.
 
Foleni itapungua pale tu public transport itakapokua imara na si vipanya na costa kutumika.kutumia kodi haiepukiki maana ndicho chanzo peke cha mapato ya serekali. Mimi nashahuli kujengwe public parking maeneo kama ubungu, mwenge,Tazara,na kurasini kisha kuwekwe mageti ili anaetaka kuingia mjini ni kigari chake alipie kiasi kama elfu 20 kupita kwenye geti hilo au apaki gari apande bus. Utaona jinsi msongamano mjini utapungua na mapato kuongezeka.
Nakuonea huruma! Foleni inasababisha na mipangilio mibovu ya mtawanyiko wa ofisi na masoko. asubuhi magari yanajipnga kuelekea sehemu moja. na jioni kurudi kwa shida.
Mi naamini kama wizara , mabenki yange tawanywa, kungekuwa na unafuu. Tatizo wizara zote ziko eneo moja, Soko la kariakoo kila mfanya biashara anahangaika kwenda k/koo, unadhani magari yanaki wapi? Tatizo sio public transport, bali ni location ya eneo moja na kila mtu anahangaika kwenda kupata huduma
 
Nakuonea huruma! Foleni inasababisha na mipangilio mibovu ya mtawanyiko wa ofisi na masoko. asubuhi magari yanajipnga kuelekea sehemu moja. na jioni kurudi
kwa shida.
Mi naamini kama wizara , mabenki yange tawanywa, kungekuwa na unafuu. Tatizo wizara zote ziko eneo moja, Soko la kariakoo kila mfanya biashara anahangaika kwenda k/koo, unadhani magari yanaki wapi? Tatizo sio public transport, bali ni location ya eneo moja na kila mtu anahangaika kwenda kupata huduma

Nakubaliana na wewe katika hoja ya location lakini ukubari pia kuwa kutokana na tatizo la public transport kila mtu anatamani kuwa na gari na hivyo msongamano kuongezeka. Kama kukitokea parking za uhakika zenye usalama na kisha public transport yenye uhakika msongamano utaisha hata kabla ya kurelocate offices. Flyovers si suluhisho hata kidogo.
 
Back
Top Bottom