Lukwangule
Senior Member
- May 25, 2009
- 157
- 2
NI yowe la mjukuu wake labda ndilo lililookoa maisha ya ajuza mwenye miaka kati ya 90 na100 anayejulikana kama Sophia Makubo ambaye mtu mmoja mkatili kutoka kubiterere alimvamia nyumbani kwake na kumkata kwa panga miguu yake yote miwili.
Yowe la mjukuu huyo hata hivyo lilichelewa kuokoa miguu ya ajuza huyo ingawa mvamiaji naye alitwangwa kisawasawa na wananchi waliotikia yowe hilo la usiku na kutolewa utumbo nje ; na kufa baada ya kufikishwa hospitalini.
Taarifa zinasema ajuza huyo alikumbwa na mkasa huo mwishoni mwa wiki nyumbani kwake Ngerengere kata ya Sirari tarafa ya Inchugu wilayani Tarime Mkoani Mara.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Costantine Massawe alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 27 mwaka huu na ajuza huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya Tarime.
Yowe la mjukuu huyo hata hivyo lilichelewa kuokoa miguu ya ajuza huyo ingawa mvamiaji naye alitwangwa kisawasawa na wananchi waliotikia yowe hilo la usiku na kutolewa utumbo nje ; na kufa baada ya kufikishwa hospitalini.
Taarifa zinasema ajuza huyo alikumbwa na mkasa huo mwishoni mwa wiki nyumbani kwake Ngerengere kata ya Sirari tarafa ya Inchugu wilayani Tarime Mkoani Mara.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Costantine Massawe alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 27 mwaka huu na ajuza huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya Tarime.