Kuchasoni Kuchawangu
JF-Expert Member
- Aug 21, 2012
- 623
- 378
Kama matumizi yako kwa mwezi yanazidi unit 75 unatakiwa kuwa tariff 1, unit ambazo zinazodi unalipia Tsh 350 kwa unit.
Andika barua ufike ofisi ya TANESCO uliyokaribu nayo ukiomba kubadilishiwa Tariff.
Unaweza kujieidhisha kwa kuangalia kwenye risiti yako ya kununulia umeme inaonesha tariff uliyopo.
Pia unapounganishiwa umeme automatic unakuwa Tariff 1, Tariff 4 unaenda baada ya kuwa umeomba ndio unapelekwa.
Nafikiri ulishawahi kuomba kubadilishiwa Tariff? Kama bado angalia upo Tariff gani kwanza.
Mkuu asante sana kwa ufafanuzi wako unaoutoa hapa jukwaani. Lakini ukitaka kubadilisha kutoka T1 kwenda T4 kwa wale tunaonunua umeme kupitia mitandao ya simu unaambiwa uende na risti ya miezi sita nyuma ndo ushughulikiwe. Wakati umbali wa kwenda ofisi ya tanesco ni sawa na kulipia service charge miezi miwili. Ukitaka haraka utaombwa pesa hii imekaaje mkuu.