Tanzia ya Mzee Jumbe na yaliyomo katika kitabu cha ujasusi wa kidola na kiuchumi

Yericko Nyerere, Mbona hapo kwa Alhaj Aboud Jumbe umeeleza kwa mkato tu kwamba alisema kama ndio hivyo Muungano uvunjike, Je yeye alikosa nini hadhi kuvuliwa Wadhifa wake wa Urais wa SMZ?
 
Sijui nani kaniloga mie kwa uvivu yaani hata sijasoma nikamaliza nimechokea katikati! natamani mtu a summary then mie nimeze tu
 
Mimi napenda kujua zile makala za kiroboto tape/mkanda wa kiroboto zilikuwa zikirushwa na radio sauti ya zanzibar kila siku baada ya taarifa ya habari ya saa 1 usiku zikiikashifu serekali ya jamuhuri.

1. Kwa nini mzee Jumbe alikuwa anaruhusu ziendee kurushwa?
2. Jumbe (R.I.P) nini kilisababisha kuvuliwa nyadhifa zake zote.
 
Hee tunaaminishwa Nyerere alikua kiongozi mbabe sana ,Sasa huyu Karume sijui alikua nini !
 
That's what I believe mkuu...pamoja na mapungufu take.. Uvumilivu wake na busara zake dhidi ya mikingamo ya karume ilisaidia kuendelea kuwepo muungano
Kina yericko wana agenda ya siri na mjomba wao zaidi ni ubinafsi maana mzee nyerere hakuwapa muda ndugu zake wajitajilishe kupitia mgongo wake. Halafu ukichukulia baba yake yericko alalikua mjanja ktk biashara. Jk alitaifisha mpaka shughuli za wadogo zake. Musoma hotels baba ya yericko alikua mwanahisa dabaga farm kaka yake Joseph pia alitendwa hivyo sitashangaa jericko kuponda uongozi wa mwalimu
 
Yericko anadalalia kitabu chake na anataka kutuaminisha alichoandika ktk kitabu chake siyo propaganda ila za wenzake ni propaganda
 
Nadhani mkono wa bara ulikuwepo katika kifo cha Mzee Karume japo kilikaa kwa kisasi zaidi ya yanayoelezewa kuwepo kwa njama za mapinduzi. Uwepo wa Karume Senior kwa miaka zaidi hata ya 5 kuanzia kipindi kile kungevunja muungano kabisaa. Ilikuwa ni rahisi kumbana Abdu Jumbe kuliko mwanzilishi wa Mapinduzi Zanzibar. Ili kuipata Tanzania ya sasa kifo yaliyotokea Zanzibar ilibidi yatokee..ni mtazamo wangu tu. Mzee jumbe na msimamo wa serikali 3 na muungano wa kimkataba ndio ulimfikisha hapo alipofikia..mji Mwema kigamboniii...

Ili kuwa ni rahisi narudia kwa Mwalimu J. Nyerere kumbana Mzee jumbe kuliko kumweka chini Mzee Karume maana alikuwa ni Mzanzibar wa kweli..
 
Mzee wa copy and paste, usisahau kilipia tangazo jf
 
mzee jumbe apate pumziko la millele ametimiza wajibu wake ,kwa jamii ,pia nikupongeze yericko nyerere kwa ukusanyaji huu wa historia ya masuala ya nchi yetu ,tuna wasomi wengi ila wewe umeonyesha mfano wa pekee kwa kuandika si kuhadithia ,
 
Miaka nenda rudi tumekuwa tunasikia nyerere aliua karumue kumbe sio, mleta uzi umetufungua sana, maan huu uzi ni real sio fake, ungekuwa fake ungekuwa unajicontradict sana pia usingekuwa mrefu.
 
Nitakuwa wa mwisho kusoma hiki kitabu sababu kimendikwa na mtu amabaye hana tabiaa ya kusema ukweli mara nyingi. Sasa nitaamini vipi yaliyoandikwa humo kama ni ya kweli?? Je katika kitabu chako ulitoa wapi hizi information? Umehadithiwa au kuna mahali zimeandikwa au umeamua tu kutoa version ya story yako?
 
Shukrani kwa hadith yako nzuri lkn kuna vitu ambavyo cjavielewa unaposema karume alikuwa amsikilkzi nyerere unatumia vigezo gani? Kwani Zanzibar baada ya kupata uhuru iliungana na tanzania kwa malengo yapi? Na kwann Raisvwa Tanganyika wakati huo yeye tu ndo asikilizwe?
Halafu tuambie lini Zanziber ilikuwa koloni la t@nganyika?
Halafu inasemekana uyo kiongozi ambae ulikuwa wewe unayepeda asikilizwe yeye ndo aliongoza kwa kuua watu ikiwamo pamoja na kumuua karume na sokoine? Sasa huo uvumilivu na subira aliokuwa nazo ni zip?
 
Umesema utakuwa wa mwisho kukisoma, amini kuwa binadamu wanaozungumza kiswahili hivi sana wapo milioni 407,sasa mpaka sasa nimeuza nakala miatano tu, hivyo vumilia mpaka wafike milioni 406 ndipo nitajibu maswali yako ili ielewe na kisha kukisom hiki kitabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…