GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Wanabodi, Maandiko ya historia kwenye vitabu mbalimbali yanaonyesha kuna kizazi hapa duniani cha wanaisrael kiliahidiwa nchi ya ahadi na ahadi ikatimizwa, Ingawa safari kuelekea nchi ya ahadi ilikuwa na misukosuko kwa wanaisrael wachache walifika nchi ya ahadi.
Uchaguzi wa serikali za mitaa kwa CCM kuamua kimabavu kuwaweka viongozi wa mitaa ili watuongoze kinguvu imetimia, Hali hii ilisubiriwa na wengi baada ya uchaguzi wa 2015 sasa imetimia
Wananchi Tanzania sasa tegemeeni neema na maendeleo makubwa kuelekea chama kimoja cha CCM.
Dodoma Itakuwa kama New York City, Hili jiji ifikapo 2020 Itakuwa sehemu ya kuigizia filamu na kutoa series au episode mbalimbali.
Wabunge wa Chama kimoja CCM ifikapo 2020 watapigania kila Mtanzania apokee pesa taslimu bure bila kufanya kazi yeyote ile
Hakuna haja ya kufanya kazi kwani serikali ya chama kimoja itatoa chakula, mavazi, mboga na matunda kwa kila Mtanzania, Hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kufurahia uchaguzi ambao tutakuwa na chama kimoja
Wabunge wa chama kimoja ndio Think Tank wa Taifa kwani ifikapo 2020 watapata idea na mawazo mapya ya kuendesha nchi. Hapo awali akili zao zilichoshwa na hali ya ushindani katika kugombea hivyo kuwa na mawazo mafupi
Nchi ya ahadi iliyohubiriwa tangu uhuru sasa inakwenda kutimia, kutakuwa na shule za serikali tu ifikapo 2020
Biashara zitafanywa na serikali tu ifikapo 2020.
Makampuni mengi binafsi yatahodhiwa na serikali tu kwa kupokwa toka kwa watu binafsi
Tunapounga mkono juhudi pia tujiandae kisaikolojia kuporwa mali zetu na ni nani atakayekusemea?
Uchaguzi wa serikali za mitaa kwa CCM kuamua kimabavu kuwaweka viongozi wa mitaa ili watuongoze kinguvu imetimia, Hali hii ilisubiriwa na wengi baada ya uchaguzi wa 2015 sasa imetimia
Wananchi Tanzania sasa tegemeeni neema na maendeleo makubwa kuelekea chama kimoja cha CCM.
Dodoma Itakuwa kama New York City, Hili jiji ifikapo 2020 Itakuwa sehemu ya kuigizia filamu na kutoa series au episode mbalimbali.
Wabunge wa Chama kimoja CCM ifikapo 2020 watapigania kila Mtanzania apokee pesa taslimu bure bila kufanya kazi yeyote ile
Hakuna haja ya kufanya kazi kwani serikali ya chama kimoja itatoa chakula, mavazi, mboga na matunda kwa kila Mtanzania, Hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kufurahia uchaguzi ambao tutakuwa na chama kimoja
Wabunge wa chama kimoja ndio Think Tank wa Taifa kwani ifikapo 2020 watapata idea na mawazo mapya ya kuendesha nchi. Hapo awali akili zao zilichoshwa na hali ya ushindani katika kugombea hivyo kuwa na mawazo mafupi
Nchi ya ahadi iliyohubiriwa tangu uhuru sasa inakwenda kutimia, kutakuwa na shule za serikali tu ifikapo 2020
Biashara zitafanywa na serikali tu ifikapo 2020.
Makampuni mengi binafsi yatahodhiwa na serikali tu kwa kupokwa toka kwa watu binafsi
Tunapounga mkono juhudi pia tujiandae kisaikolojia kuporwa mali zetu na ni nani atakayekusemea?