Tanzania yapanda katika orodha ya timu bora FIFA

Tanzania yapanda katika orodha ya timu bora FIFA

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Shirikisho la kimataifa la soka FIFA limetoa orodha mpya ya timu bora za soka mwaka huu wa 2026.

Morocco wamepanda kwa kiwango kikubwa zaidi katika timu za wanaume wakifika hadi nafasi ya nane,licha ya kupoteza katika fainali ya michuano ya soka barani Afrika AFCON dhidi ya Senegal.

Senegal walipanda hadi kufika nafasi ya 12 kutoka nafasi ya 17 waliyopata mwaka 2024.

Mwaka jana Morocco walikuwa katika nafasi ya 11, na nafasi bora waliyowahi kushika katika orodha hiyo ya FIFA ni 10 ikiwa ni mwaka 1998.

Hata hivyo timu ya Afrika iliyowahi kuchukua nafasi bora zaidi kwenye orodha hiyo ni Nigeria iliyokuwa nafasi ya 5 Aprili mwaka 1994.

Michuano ya AFCON ya 2025 imekuwa na ushawishi mkubwa katika soka la kimataifa na hivyo kuchangia timu nyingi za Afrika kupanda orodha hiyo.

Washindi wa shaba katika dimba hilo Nigeria wameorodheshwa katika nafasi ya 26 ,Cameroon nao wako katika nafasi ya 45 nao Misri waliotolewa nusu fainali wameorodheshwa nafasi ya 31 wakiwa wamepanda kwa alama nne pia wakiwa nafasi tatu nyuma ya Algeria.

Gabon waliporomoka kwa alama nyingi hadi nafasi ya 86 baada ya kutolewa mapema kwenye dimba la Afcon.

Mabingwa wa Ulaya Hispania wanaongoza orodha hiyo mbele ya bingwa wa dunia Argentina walio nafasi ya pili.

Ufaransa ni watatu wakifuatwa na England nafasi ya 4 huku Brazil wakishikilia nafasi ya 5.

Ureno na Uholanzi wako nafasi ya sita na saba mtawalia.

Je timu za Arika Mashariki ziko wapi?

Taifa stars ya Tanzania imepanda kwa nafasi mbili na kufikia nafasi ya 110 baada ya kushamiri kwenye dimba la Afcon wakitoka hatua ya raundi ya16 mara ya kwanza kwenye historia.

Uganda nao wameshuka kwa nafasi tatu baada ya kuboronga kwenye AFCON,wameorodheshwa nafasi ya 88 baada ya kushindwa kushinda hata mechi moja kwenye michuano hiyo.

Harambee star s wa Kenya wamedorora kwenye orodha hiyo baada ya kukosa kushiriki Afcon kwa mara ya tatu,wako nafasi ya 113.
1768900224973.png
 
Back
Top Bottom