Burundi kua katika hali mbaya kuliko sisi haimaanishi tupo katika hali nzuri.
Ni kama moja kapata C mwingine F huku passing grade ni B, japo C yupo vizuri kuliko F ila bado hajapass vilevile tu. Watanzania wengi maskini wa kutupa, asilimia kubwa wanaamka hawajui hata kama watafanikisha mlo moja kwa siku, nchi ambazo tunaweza sema ni successful japo wana maskini ndio lakini bado maskini wengi hawasumbuki kwenye swala la msosi.
Tanzania na vyanzo vyote vya fresh water, sehemu ambazo hawana maji salama ya kunywa ni nyingi mno, kuna nchi nyingi tu wanahamu wangekua na vyanzo kama vyetu maana unakuta wana vyanzo kama asilimia 20 ya tulivyonavyo lakini wamefanikiwa ku-supply nchi nzima na maji hayakatiki 24/7. Mwanza tu pamoja na kua na Ziwa Victoria maji yanakatika karibia kila wiki, ni aibu kubwa mno. Bado tunacheza sana
Marais waliopita sisemi wamevuruga sana, wamejitahidi kadri ya uwezo na nawapongeza kwa hilo najua kuongoza nchi sio swala rahisi lakini bado walichokifanya hakitoshi kabisa.