Tanzania usipofisadi serikalini - adhabu ni hii

salosalo

JF-Expert Member
Jun 7, 2012
596
278
Kwa muda mrefu watanzania tumekuwa na tabia ya kusifu uovu unapofanyika.... sasa imekwenda hadi makazini. mtu akiajiriwa serikalini kwenye nafasi yoyote yenye mianya ya kuiba au kufisadi bila kufanya hivyo anatukanwa kila aina ya tusi na watz wenzake wanao mzunguka. Zaidi wale waliowahi kushika nafasi za namna hiyo serikalini bila utajiri mpaka kustaafu,wamekuwa wakinyooshewa vidole na kuambiwa Ugoigoi wao ndo uliowaponza.

Lakini kwa wale waliopata kuliibia taifa(kufisadi) kwa namna yoyote wanaitwa wajaja, kwamba huyo sio boya kama maboya wengine. Maneno haya yanazungumzwa mbele ya watoto wanaokua. Wanajegwa kwa kuamini kuwa kuibia serikali ndio ujanja, kinyume na hapo ni uboya. Kumbe naomba jamii tubadilike, tuanye kusifu uchafu huku tukidhani tunajenga kumbe tunabomoa. Tena watu wakiwa kazini ukawazuia kuiba mali ya umma basi watakuundia mikasa ili ufukuzwe kazini kwa madai kuwa unaweka jam. Kwa serikalini kama wanamamlaka kubwa basi maramoja utahamishwa kituo cha kazi.

Nashauri vita dhidi ya ufisadi ianzie nyumbani kwetu. Wazee wa busara semeni kitu hapa....
 
Aisee! We kumbe umeliona hili! Hii ndio halihalisi ndugu yangu. Hata wale wanaodai kuwa niwapambanaji wa ufisadi na wao ofisini kwao ni hayohayo,kifupi maadili hakuna. Nikweli kuwa vita ianzie nyumbani na kwenye taasisi za dini ili angalau watu wamwogope Mungu.
 
Nasikia usipoiba serikali unaonekana bonge la *****.....iliwezekana kutokuiba kipindi cha nyerere tu
 
ni waziri gani au mbunge gani ambe hajaibia serkali?
tuwapime kabla hawajawa na vyeo walivo navyo walikuwaje?
serikalini huko kuna allowance kibao zonatolewa bila hata kufanya kazi
hata mini nipata hizo nachukua kwanini niobakie maskini kama sera ya chama ni ya kuchukua chak mapema?
kama ulaji upo na uwezekano wa kula upo kwanini nife njaa? lol
 
Nafikiri ifike mahali watanzania wapate madarasa ya uadilifu...ethics courses labda itasaidia lakini ianzie nyumbani toka mtoto mdogo afundishwe juu ya ubaya wa tamaa na rushwa na pia afundishwe kufikiria wengine na kuchukia ubinafsi....hasa unapokuwa na nafasi katika nchi hii. Kwa hawa walioko madarakani sasa nafikiri sijui tumechelewa ila kwa kweli tunahitaji kuwa na uelewa wa nini ni maadili ya kazi...
 
Watanzania wanapoomba kazi huwa hawajali mshahara atakaopewa bali marupuprupu na hasahasa fursa za dili (wizi) kwenye kazi husika.

Wivu ulio wa haki ,kutenda haki na kutowakatisha tamaa watenda haki ndiko kutakakotuokoa.SERIKALI ITIMIZE WAJIBU WAKE WA KUBORESHA MASILAHI YA WAFANYAKAZI NA KUPUNGUZA TOFAUTI ZA MISHAHARA.

Inatia kinyaa kusikia sisi 30 tunaweza kulipwa na mfanyakazi mwenzetu wa serikali na bado akabakiwa na fungu la kutosha.
 
Yani hii kitu ya kutumia mianya kujinufaisha imeshaingia kwenye damu ya watu wasiopenda kuangalia mbali,
Hapa ofisini kuna mwanafunzi kapewa nafasi ya mafunzo kwa vitendo (field) ameshaanza kubeba rim paper za ofisi ya serikali kwa manufaa yake binafsi, Taifa la leo hilo.
 
Aisee! We kumbe umeliona hili! Hii ndio halihalisi ndugu yangu. Hata wale wanaodai kuwa niwapambanaji wa ufisadi na wao ofisini kwao ni hayohayo,kifupi maadili hakuna. Nikweli kuwa vita ianzie nyumbani na kwenye taasisi za dini ili angalau watu wamwogope Mungu.

Umenena la kunena Mja
 
Nasikia usipoiba serikali unaonekana bonge la *****.....iliwezekana kutokuiba kipindi cha nyerere tu

Ni kweli ndugu yangu. Na kama kunawaliopata kuiba kipindi hicho, basi hawakupata kutumia mali hizo za wizi mpaka Mauti ilipowakuta la sivyo basi wanazitumia sasa. Maana wakati huo adhabu aliyoipata yeyote aliyebainika kuiba ilitosha sana kuwaogopesha wengine kufuata nyayo hizo mbaya. Big up Nyerere
 
ni waziri gani au mbunge gani ambe hajaibia serkali?
tuwapime kabla hawajawa na vyeo walivo navyo walikuwaje?
serikalini huko kuna allowance kibao zonatolewa bila hata kufanya kazi
hata mini nipata hizo nachukua kwanini niobakie maskini kama sera ya chama ni ya kuchukua chak mapema?
kama ulaji upo na uwezekano wa kula upo kwanini nife njaa? lol

mkubwa usemalo ni ukweli mtupu, lakini tunako kwenda hao wanaochukua chao mapema watalia juani baada ya kuchumia kivurini
 
Nafikiri ifike mahali watanzania wapate madarasa ya uadilifu...ethics courses labda itasaidia lakini ianzie nyumbani toka mtoto mdogo afundishwe juu ya ubaya wa tamaa na rushwa na pia afundishwe kufikiria wengine na kuchukia ubinafsi....hasa unapokuwa na nafasi katika nchi hii. Kwa hawa walioko madarakani sasa nafikiri sijui tumechelewa ila kwa kweli tunahitaji kuwa na uelewa wa nini ni maadili ya kazi...

Zote pointi kaka ila hiyo ya blue imenigusa kipekee sana. Walioko madarakana hata wale wanaosubiri madaraka nje hawafai. Sasa najiuliza hawa watoto zetu watafundishwa Maadili/uadilifu na nani? au labda tanzie hapoo..
 
Tanzania bila wizi inawezekana.

Kweli mkubwa ila nadhani mvua hii inatuloanisha kwasababu paa lake linavuja. Tutahangaika sana kujenga kuta zinazobomoka kwa kuloana bila ukomu isipokuwa pale tutakapo ziba na kuezeka vizuri paa. Ninamaanisha ninacho kisema
 
Watanzania wanapoomba kazi huwa hawajali mshahara atakaopewa bali marupuprupu na hasahasa fursa za dili (wizi) kwenye kazi husika.

Wivu ulio wa haki ,kutenda haki na kutowakatisha tamaa watenda haki ndiko kutakakotuokoa.SERIKALI ITIMIZE WAJIBU WAKE WA KUBORESHA MASILAHI YA WAFANYAKAZI NA KUPUNGUZA TOFAUTI ZA MISHAHARA.

Inatia kinyaa kusikia sisi 30 tunaweza kulipwa na mfanyakazi mwenzetu wa serikali na bado akabakiwa na fungu la kutosha.

Ndugu Fije, umenena kweli tupu.
Siku hizi wanaita DILI kama ulivyosema, sio wizi tena. Mfano mzuri we fuatilia pesa za Radar zilizokuwa zimeibwa jinsi zinavyotajwa bungeni na popote serikalini. Zimepewa jina zuri sijapata kuona
 
Yani hii kitu ya kutumia mianya kujinufaisha imeshaingia kwenye damu ya watu wasiopenda kuangalia mbali,
Hapa ofisini kuna mwanafunzi kapewa nafasi ya mafunzo kwa vitendo (field) ameshaanza kubeba rim paper za ofisi ya serikali kwa manufaa yake binafsi, Taifa la leo hilo.
Dah, imenibidi nicheke kidogo. Wewe umejua kuwa hilo ni kosa kama makosa mengine. Leo anabeba ream paper 7bu ndio ana-access nazo, akiendamahali akawa na access na mamillion ya pesa mwendo ndio huohuo. Mkanye tafadhali
 
Nasikia usipoiba serikali unaonekana bonge la *****.....iliwezekana kutokuiba kipindi cha nyerere tu

Nani kakudanganya? Mbowe karithi mali ya kutoka wapi? Uliza lile jengo kwenye bar yake limepatikanaje na baba'ke alikuwa na wadhifa gani Serikalini?
 
Nani kakudanganya? Mbowe karithi mali ya kutoka wapi? Uliza lile jengo kwenye bar yake limepatikanaje na baba'ke alikuwa na wadhifa gani Serikalini?

Tupo hapa kujuzana yale tusio yajua.. Tafdhali tuambe ilipatikanaje na wadhiwa wa baba yake ulikuwa upi?
 
Nafikiri ifike mahali watanzania wapate madarasa ya uadilifu...ethics courses labda itasaidia lakini ianzie nyumbani toka mtoto mdogo afundishwe juu ya ubaya wa tamaa na rushwa na pia afundishwe kufikiria wengine na kuchukia ubinafsi....hasa unapokuwa na nafasi katika nchi hii. Kwa hawa walioko madarakani sasa nafikiri sijui tumechelewa ila kwa kweli tunahitaji kuwa na uelewa wa nini ni maadili ya kazi...
Mkuu,
Hii nadhani itakuwa ngumu kidogo. Mimi nakumbuka nilipokuwa mdogo(6-7yrs) huko kipindi cha nyuma nilikuwa nikipita jikoni nyumbani na kukuta nyama inachemshwa nilikuwa nanyakua Kama paka jizi na kukimbilia uwani kula..bila kujali nilikuwa naihujumu familia yetu,huku lawama zote zikienda kwa dada (house girl) kwamba ndiye aliyekuwa akifanya ufisadi wa mboga. Arobaini zangu zilifika nikakamatwa na mfupa uwani,nikatandikwa na fimbo ya mpera na tabia ya uhujumu mboga ikakomea hapo.

Kwa hiyo kuna uwezekano kabisa hivi vitabia tunavyo tokea utoto. Inahuzunisha lakini ndio ukweli.
 
mafisadi sio serikalini tu, hata kwenye sekta binafsi. nilikuwa na kiduka changu cha dawa baridi nimemuweka mdada aniuzie nikienda kazini anaenda kkoo anachukua dawa zake ndio anauza hapo dukani zangu haziuziki mpaka nikafunga duka ndio jirani akaja kunipa hiyo siri. ukienda posta kwenye maduka ya wahindi wauzaji wanakwambia hii bidhaa inauzwa 300000,lakini nenda pale mlangoni umpe mlinzi 150000 na bidhaa utaikuta hapohapo! ukikaa ofisini unaletewa saa ya 300000 unaambiwa lete 150000, ukiuliza imetoka wapi unaambiwa imeibiwa airport! usiache mafundi wakutengenezee matofali wakati haupo watabadilisha ratio bila kujali ubora utajijua mwenyewe na nyumba yako
hayo ni machache niliyokutana nayo, sasa niambieni tunaanzia wapi kurekebisha hii hali!!
 
Back
Top Bottom