Tanzania Ranked among Africa`s top three in governance!

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,424
13,040
US ranks Tanzania among Africa`s top three in governance


SOURCE: Guardian


Hivi haya ni ya kweli??? Je wanatumia vigezo gani?? Wakati mali yetu inachotwa usiku na mchana, wakati skandali za Mafisadi ndiyo zinazidi kupamba moto, hivi kweli tunaweza kuiamini hii ripoti??? Au ndiyo njia yao ya kujichotea???
 
Kazi kubwa ilifanywa na Mkapa.Halafu hawa mabeberu wakikusifia ujue kuna jambo ambalo huwa negative impacts zake ni kwa mwananchi.

Hata Dikteta Mobutu alisifiwa sana na Ufaransa.Leo hii Venezuaela na Cuba wana maendeleo makubwa mbona Us hawawasifii.Sifa zao za kizandiki zina malengo yao.

E bwana watuachie nchi yetu kwani wametumia vipimo gani vya uhakika.
 
Shilingi kila siku inaporomoka ya kenya kila kukicha inatupiga bao wao wanasema tunafanya vizuri hivi kuna unafiki mkubwa zaidi ya huu?

Balozi wao alisema kuwa hakuna budi kushughulikia mafisadi alikuwa akimaanisha kitu gani?

Mbona nchi zinazoendelea hazisifiwi?ama ni kwa wale wanaowauzia madini kwa bei poa ?
 
Yes Sir, Yes sir ndiyo siri yake.

Ukiwa "no sir" Nchi yako kila siku itakuwa bad governance
 
Kusema kweli Mkapa ameuweka uchumi wetu kwenye hali nzuri, mtu yoyote anayeufahamu uchumi lazima atakubaliana na hilo. Ukilinganisha alipoichukua nchi na alipomwachia JK unaona kabisa kuwa umechumi wa Tanzania umebadilika na unafuata sera nzuri, kama utekelezaji wake ungekuwa na mwendelezo nadhani mambo yangekuwa mazuri zaidi. Hii hata US waseme au wasiseme ukweli ni kwamba the economy was in good shape.
Kuna jambo? yes kuna jambo kwa sababu sasa hivi Tanzania imeanza kuwa na potential ya kuwa na middle class kwa hiyo wawekezaji wameanza kuona opportunity ya kuwekeza na kuchuma pesa. Hii ni common sense.
 
Nafikiri labda maana ya good governance ni kuwapa ulaji. Nchi kama Botswana na Namibia ambao wanaingia mikataba 50/50, rushwa iko chini na wanajitegemea 100% kwenye bajeti yao eti bado tumewapiga bao. Huu ni kututapeli ili wajichotee dhahabu yetu. May be ndiyo sababu nchi zilizotajwa ni zile zinazozalisha Dhahabu kwa wingi Africa. Hata wakiangalia Mafanikio ya awamu ya BWM bado hatustahili hiyo ranking.
 
Labda wangeorodhesha vigezo vilivyotumika hapa ningeweza kuwaelewa na hata hivyo sijui kam kun vigezo vyovyote vya kiuchumi ambavyo vingeiweka tz top 3.

There must be something very wrong.
 
Hawa wanataka wapewe sehemu waweke kituo chao cha kijeshi. Vinginevyo hiyo conclusion yao ni ZERO!
 
Ukiona hivyo kweli kuna kitu wanakitaka wakianza na kutupaka mafuta kwenye mgongo wa chupa. Tafiti zao zimeshaonyesha kuwa majibu ya Dr. Watson yana ukweli hivyo watatumia hiyo tafiti kujichukulia wanachotaka,

YES SIR.
 
...good governance my ass,mwaka wa saba huu nafuatilia mirathi ya baba sijapata hata ndululu,kila siku file halipo oooh mara mzee fisadi wa kusign hayupo,tunasubiri report ya mwisho kazini kwake,tunaomba uje wiki ijayo tutakuwa tumemaliza oooh choroko,maharage,mbaazi..wapumbavu sana hawa!
 
That's why i said they must be upto something? Waache mchezo wao wa kizandiki,good governance ili hali ufisadi una Mizizi.

This guy's must must be crazy na mtu mwenye akili alienda shule akakubaliana nao basi Mzimu wa Chifu Mangungo bado unatuandama.
 
Wameshajua Wadanganyika wanapenda sifa za kijinga ndo maana wanaanza kupaka mafuta kulainisha kidogo kabla hawajaanza kubandua ki-ulaini.
 
Common sense.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…