Tanzania Project 2035

Dennis Robert Shughuru

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2024
Posts
4,125
Reaction score
6,141
TANZANIA PROJECT 2035
VISION
  1. Tanzania kuwa nchi yenye uchumi mkubwa Afrika kufikia mwaka 2070's in term of GDP na PPP
  2. Tanzania kuwa nchi yenye uchumi mkubwa duniani kufikia mwaka 2100's in term of GDP na PPP
MISSION
Nilitangaza nia ya kuwa Rais wa Tanzania 29/6/2024 kwa mara ya kwanza, kwa kipindi chote hicho nimepata feedback nyingi ila kikubwa kuna mambo mengi sana nimejifunza unatakiwa uanze safari ndo update experience, ukosee ndo ujifunze

Ķwanini sitagombea Urais mwaka 2025 na mwaka 2030 lazima nielezee ili kuondoa ile sintofahamu labda huyu anafuta umaarufu, labda huyu kachanganyikiwa natakiwa nionyeshe destination yangu ni lini, unapoanza safari yeyote lazima uelezee unapoishia
  • Siko eligible kugombea nafasi ya urais sababu nimezaliwa 2 dec 1991, kwa hiyo sikidhi matakwa ya katiba ya Tanzania
  • Mimi sijulikani (I am no body here in Tanzania) hasa kwenye mambo ya uongozi kwa hiyo ninakazi kubwa sana ya kufanya ili kuprove kwa watu kwamba nina kitu ambacho kitawasaidia na kuniamini kuwa Rais wa Tanzania
  • Naamini character yangu kuanzia mwaka 2025 mpaka 2035 ndo itakayoamua either niaminiwe kuwa Rais wa Tanzania or nionekane mtu wa ajabu na hovyo
Niko eligible mwaka 2035
Mwaka huu mimi nina miaka 33, (2/dec/1991)-kwa hiyo mwaka 2035 ndo ntakua eligible kugombea urais

NICHAGULIWA MWAKA 2035 NA KUWA RAIS YAFUATAYO NI MAMBO NTAKAYOYAFANYA YAKO MENGI ILA HAYA MANNE NDO YA MUHIMU SANA
👇👇👇👇👇👇👇👇
A)-Mabadiliko ya Katiba na baadhi ya mapendekezo yanayotakiwa kuwepo kwenye katiba
  1. Msajili wa vyama vya siasa kutokuchaguliwa na Rais bali na vyama vya siasa vitakaa na kuamua namna ya kumchagua msajili wa vyama vya siasa kazi ya Rais ni kumuapisha
  2. DPP kuchaguliwa na wananchi na hatikwi kuwa na historia ya kuwa affiliate na chama chochote na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania. Na pia kutaanzishwa shirika la upelelezi wa makosa ya jinai tofauti na jeshi la polisi na litakuwa chini ya DPP.
  3. Jaji mkuu kuchaguliwa na wananchi hatakiwi kuwa affliated na chama chochote-Majaji wa mahakama kuu kutochaguliwa na Rais bali na mchakato wa ndani wa mahakama kazi ya Rais ni kuwaapisha na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania
  4. Majaji wa mahakama kuu kutochaguliwa na Rais bali ni kupitia mchakato wa ndani wa mahakama
  5. Rais atateua mabalozi, mawaziri, mkuu wa majeshi (CDF), mkuu wa jeshi la polisi (IGP), mkuu wa usalama wa Taifa, na mabosi kwenye mashirika ya serikali
  6. Hakutakuwa na makamu wa Rais badala yake kutakuwa na waziri mkuu asiyekuwa na jimbo, na kama Rais akitokea bara basi waziri mkuu atatokea zanzibar)
  7. Mawaziri kutokua wabunge, wizara kuwa 18 (mawaziri wawili kutoka pemba na wawili kutoka unguja jumla wanne) na kutokuwa na naibu waziri, kutakuwa na waziri na katibu mkuu
  8. Deni la taifa kukaguliwa na CAG ili kujua namna lilivyotumika, baada ya kuisoma atamkabidhi Rais na Dpp
  9. Mtoto akizaliwa Tanzania na wazazi ambao wanaishi kimagendo hatapata uraia wa Tanzania wa kuzaliwa
  10. Mkuu wa takukuru kuchaguliwa na wananchi na hatakiwi kuwa affiliate na chama chochote, na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania
  11. Mkaguzi wa miradi ya serikali huyu atakua anachagulia na wananchi na atakua ni engeineer na atakagua miradi yote iliyofanywa na kutathmini kama inaendana na thamani ya fedha iliyotengwa na inaubora uliokusudiwa na hatakuwa eligible kugombea Urais akimaliza mda wake
  12. Mbunge ni lazima aishi kwenye jimbo lake sio haki hata kidogo na ni ukatili mkubwa sana mbunge tunakuchagua alafu unaenda kuishi dar jimboni unakuja kama mtaliiMawaziri kutokuwa wabunge sababu mawaziri wengi wanapwaya kwenye majimbo yao
  13. Hakutakuwa na wabunge wa kuteuliwa na Rais na viti maalumu, wabunge wote watachaguliwa na wananchi
  14. Nafasi ya Mkurugenzi wa wilaya itafutwa na majukumu yake atapewa mbunge
  15. Waziri mkuu, DPP, jaji mkuu, mkuu wa TAKUKURU, mkaguzi wa miradi ya serikali hawa hawatakuwa eligible kugombea nafasi ya Urais
  16. Rais akifia madarakani kutaitishwa snap election ya kumchagua Rais mpya ndani ya miezi sita-bunge litamchagua mtu wa kukaimu nafasi ya Urais mpaka pale atakapochaguliwa-aliyekaimu hatarusiwa kugombea nafasi ya urais-na kabla ya mwaka mmoja wa uchaguzi basi aliyechaguliwa na bunge atamalizia mpaka uchaguzi mwigine na hatakuwa eligible kugombea
  17. Uchaguzi mkuu wa viongozi wa kisiasa utafanyika kila baada ya miaka 5 na inayogawanyika na tano ukitoa snap election
  18. Rais aliyeshindwa uchaguzi anaweza akagombea tena uchaguzi mwingine
  19. Rais anaweza shtakiwa, waziri mkuu anaweza shtakiwa
  20. Uchaguzi wa viongozi ambao sio wa kisiasa utafanyika miaka miwili baada ya uchaguzi wa viongozi wa kisiasa
  21. Mshindi wa pili kwenye uchaguzi wa viongozi wa kisiasa wa Rais basi atakua kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni
  22. Baada ya uchaguzi kutaka na mda wa miezi miwili ya kukabidhi ofisi kwa serikali inayoondoka madarakani-Rais mpya ataapishwa baada ya miezi miwili kupita
  23. Wakuu wa mikoa kuchaguliwa na wananchi
  24. Spika wa bunge atachaguliwa na wananchi na wakati wa uchaguzi atakuwa na makamu wake, na spika akifariki makamu watakaimu na ndani ya siku mia moja utafanyika uchaguzi wa kuchagua spika mwingine, spika na makamu wa spika ni mtu ambaye hana historia ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa
  25. Mchakato ndani ya vyama waamuzi wa mwisho ni wanachama wagombea hata wawe 100 wote watapigiwa kura na wanachama wa chama husika ambao ni hai kwenye uchaguzi wa ndani
  26. Mchakato wa kumpata Rais wa ndani utafanyika kwa kupigiwa kura za wanachama wa chama husika kwenye kila mkoa na sio kuteuliwa na kikundi cha watu wachache
  27. Kutakuwa na chaguzi mbili;- ya Urais, wabunge na madiwani na utafanyika kwenye miaka inayogawanyika na 5, baada ya miaka 2 kupita uchaguzi mkuu kutafanyika uchaguzi wa wakuu wa mikoa, DPP, JAJI MKUU, MKUU WA TAKUKURU, SPIKA WA BUNGE, MKAGUZI WA UBORA WA MIRADI YA SERIKALI, na wenyeviti wa mtaa
  28. Mgombea anayeshika nafasi ya pili kwenye ucbaguzi wa Rais basi atakua ndo kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni
  29. Vyombo vya habari kuwa huru hata kuikosoa serikali
  30. Vyuo vikuu kurusiwa kufanya midahalo na kuikosoa serikali pale wanapoona imekosea
  31. Kubadilisha jina la fedha ya Tanzania kutoka shilingi na kuwa Tanzanite.
  32. Usalama wa Taifa wa sasa utaendelea kulinda viongozi wote wa Tanzania, kutaanzishwa Tanzania Economic Intelligence kulinda viwanda, na rasilimali za Tanzania.
  33. Mikataba yote iwe wazi hasa mapato yanayopatikana, ajira itakazotoa na kama kuna ulazima wa kuwapa foreigner na ijadiliwe bungeni na ni kosa la jinai kiongozi kusign mkataba wa siri- akifanya hivyo akimaliza mda wake atashtakiwa
  34. Ndoa ni kati ya mume na mke na sio vinginevyo
  35. Wagombea nafasi zote za uongozi kuanzia uenyekiti ni sharti wawe na elimu ya degree na kuendelea
  36. Ni lazima kila anayejenga kufuata mipango miji, na nikosa kujenga mahali bila kufuata masterplan
  37. Uraia wa nchi mbili utarusiwa-ila ambaye ana-uraia wa nchi mbili hatarusiwa kugombea nafasi yeyote ya kuchaguliwa na wananchi, na hatarusiwa kumiliki zaidi ya ekari moja ndani ya ardhi ya Tanzania
  38. Kutakua na uhuru wa kuongea na ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuzuia uhuru wa maoni
  39. Rais na serikali iliyoko madarakani haina mamlaka ya kuvunja bunge
  40. Bunge hata likiwa na wabunge wapinzani wengi kuliko wabunge wa chama tawala, wabunge wa upinzani hawana mamlaka ya kumtoa Rais aliyeko madarakani
  41. Kama bunge likiwa na wabunge wa upinzani wengi zaidi ya chama tawala serikali iliyoko madarakani itahitaji kura za asilimia 25 wa wabunge kupitisha budget tu na sio mambo mengine
  42. Kazi za serikali ikiwemo safari za viongozi hazitakiwi kugharamiwa na watu binafsi bali na kodi tu za wananchi kama hili likifanyika basi Rais, mkuu wa mkoa, waziri, mbunge aliyefanya hivyo atakuwa na kesi ya kujibu ya kutumia madaraka vibaya, anarusiwa kufanya hivyo kwa safari zake binafsi ambazo sio za serikali
  43. Kampuni ya Rais, mbunge, waziri, mkuu wa mkoa, na wake zao haitakiwi kupewa tender za serikali
  44. Mradi wowote ukifanywa chini ya kiwango, usipomaliziwa kwa mda, kampuni iliyopewa itashtakiwa kwa kosa la jinai
  45. Serikali zitakuwa mbili- serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na serikali ya mapinduzi ya zanzibar
  46. Ndugu, na watoto wa serikali kutokufanya majukumu ya serikali
B)-Moja ya mkakati ntakaofanya ni kuhakikisha nchi inaongeza mapato kwa sababu wigo wa mapato ya sasa ni mdogo sana ili tuweze kuendelea lazima kama nchi tuwe na uwezo wa kukusanya zaidi ya usd billion 100 kwa kuanzia na kwa haraka sana na kuwa na uchumi ambao unazalisha nikimaanisha productive
  1. Petrochemical plant itakuwa powered na gesi asilia
  2. Crude oil refinery itakuwa powered na gesi asilia
  3. Natural gas refinery itakuwa powered na gesi asilia
  4. Glass smelter (include fiberglass) itakuwa powered na gesi asilia
  5. Steel smelter itakuwa powered na makaa ya mawe
  6. Nickel smelter itakuwa powered na makaa ya mawe
  7. Copper smelter itakuwa powered na gesi asilia
  8. Nobium powder itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
  9. PCB fabrication itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
  10. Aluminium smelter itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
  11. Silicon wafer and semiconductor itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
  12. Spinning powered itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
  13. Large estate of natural rubber farm hii inatumika kuzalishia matairi ya gari, soli za viatu, condom na gloves za hospitalini
  14. Rear earth refining itakuwa powered na umeme unaozalishwa na gesi asilia
👆👆👆👆👆👆
Uwepo wa hizo smelter na refining hapo juu utavutia wawekezaji wengi sana wa viwanda vya secondary

C)-Space colonization
  1. Develop artificial ozone layer of different planet
  2. Activate fusion activities of inactive star
  3. Exploit natural satellite waves so as it can be used to facilitate communication
D)-Population projection
  1. Ifikapo mwaka 2050 lengo ni kuhakikisha Tanzania inakuwa na watu million 100
  2. Ifikapo mwaka 2100 lengo ni Tanzania kuwa na watu million 170+
E)-Nchi nzima kupimwa na kila kata watakuwa na hardcopy ya 3d masterplan ya kata husika au kijiji husika, hakuna atakayejenga bila kufuata utaratibu
  1. Kuwa na unique urban planning ambayo haitapatikana sehemu yeyote ile duniani
  2. Kuwa na unique architecture ambayo haitapatikana sehemu yeyote ile duniani
  3. Sehemu za watembea kwa miguu, na parking kupigwa paving naamini baada ya miaka 20 mpaka 30 hakutakuwa na vumbi maeneo yote ya mijini-kama wengine wameweza hata sisi tunaweza

F)-Kujenga scheme za umwagiliaji kubwa na za kisasa
  1. Ngano
  2. Alizeti & mchikichi
  3. Mpunga
  4. Natural Rubber
  5. Pamba
  6. Mahindi
G)-Umeme
Kuzalisha megawatts 1,000,000+ za umeme
  1. Unit moja ya umeme kuuziwa wananchi Tanzanite 20 unit 1
  2. Unit moja ya umeme kwa wenye biashara maduka Tanzanite 15 Unit 1
  3. Unit moja ya umeme kwa wenye viwanda Tanzanite 10 Unit 1
H)- Mabadiliko ya kodi
  1. VAT kuwa 4%
  2. Individual Income tax 6%
  3. Corporate tax 8%
  4. Property tax 5%
  5. Capital gain tax 5%
I)- Kuongeza wigo mpana wa masomo ya kingereza shule za msingi za serikali kutoka moja mpaka manne,
  1. Hesabu kufundishwa kwa kingereza
  2. Science kufundishwa kwa kingereza
  3. Computer kufundishwa kwa kingereza
  4. Na kingereza kama somo
sio sawa kwenye nchi moja kuna watoto wa watu fulani wanasoma shule zenye wigo mpana wa masomo ya kingereza ilihali wengine wanasoma kwenye shule zenye wigo mdogo sana wa masomo kingereza
  • Mtihani kwenye shule za msingi za serikali na private utakuwa mmoja kama ilivyo kwa form four, ila hautakuwa sawa na International school
J)- Kuongeza masomo yafuatayo kwenye elimu ya secondary
  1. Programming language
  2. Graphics design
  3. Udereva wa magari yote (madogo, makubwa na scania na yale yanayotumika viwanda kama forklift, na kwenye sehemu za ujenzi kama grader)
  4. Office (advanced excel, word, & PowerPoint)
K)-Dawa kutengenezwa hapa Tanzania from scratch
  1. Zifahamu njia zitumikazo kutengeneza hizi dawa zinazouzwa pharmacy
  2. Kupredict protein mutation
  3. Amino acid sequence rules
  4. Kurudisha extinction animals
Karibuni
 
Mawazo Yako ni """UTOPIA PARKWAYS""" NIKUHAKIKISHIE RAISI AKIINGIA MADARAKANI WANACHO WAZA NI NEXT ELECTION...

Mh. Raisi wetu ajayee nikupongeze gentleman na nikupe moyoo SANAAAAAA tuna Imani Na wewe
Ni ukweli waliopo hawana mbinu za kuitoa nchi hapa ilipo, inahitajika fikra mpya ambayo haijawa compromise
 
Leo uko na point achana na kukosoa Yale mavitabu ya wazungu
 
Kujenga smelter na refinery
  1. Natural gas refinery
  2. Petrochemical plant
  3. Aluminium smelter
  4. Crude oil refinery
  5. Rear earth refining
  6. Copper smelter
  7. Steel smelter
  8. Glass smelter
  9. Paper and pulp
 
Mkaguzi wa miradi ya serikali huyu atakua anachagulia na wananchi na atakua ni engeineer na atakagua miradi yote iliyofanywa na kutathmini kama inaendana na thamani ya fedha iliyotengwa na inaubora uliokusudiwa na hatakuwa eligible kugombea Urais akimaliza mda wake
 

Tanzania hatuamini kwenye mipango ya mda mrefu na kuipigania- ukweli ni kwamba wachache watakuelewa kwa sababu mipango yetu ni ya kila siku na sio ya miaka 10
 

Nikiwa Rais watu hawatembea juu ya ardhi, watatembea HEWANI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…